Duh! watu wanafanyia harusi mikopo hapo Bongo wewe uko wapi?
Mkuu mtu aliyekopa benki ili akafanyie harusi kimsingi hana busara.
Na hela hiyo ni ya kiwango cha chini kabisa na si ajabu haizidi milioni 10 hadi 20.
Ujenzi wa nyumba kwa mtaji wa mkopo wa benki uuyo mdudu mwingine kabisa!
Ndio maana nimekuvuta sasa tuongee basics za mitaji kutikana na mikopo ya benki.
NHC katika miradi yake ya Morrocco,Kawe na Victoria imekopa mabilioni toka muungano wa mabenki zaidi ya kumi ili kupata mtaji.
Sasa fikiria matatizo ya fiscal policies za mikopo.
Dhamana ya mikopo hiyo ikoje?
Na riba ya mikopo hiyo ikoje?
Upande wa pili, end product kwa customer.
Nyumba moja katika hiyo miradi inauzwa kati ya milioni 250 hadi 350.
Wangapi wanaiweza bei hiyo.
Hata kama unit moja, nyumba ya vyumba 3 utainunua na kuikodisha kwa tshs milioni moja kwa mwezi, itakuchukua zaidi ya miaka 24 kurudisha hiyo hela!
Ndio maana nasema scenario ya US huwezi kulinganisha na mazingira ya bongo.
Ingekuwa rahisi kujenga , hayo makampuni ya US na benki zao waje tu hapa bongo ambapo kuna uhaba mkubwa sana wa nyumba za bei rahisi.