DSN
JF-Expert Member
- Feb 2, 2011
- 2,837
- 1,674
Nimekuwa nikijiuliza mbona makampuni mengi ya kizalendo hayabadilishi majina kama yanavyofanya makampuni mengi ya kigeni yanayoendesha shughuli zake hapa nchini.Nimegundua makampuni mengi ya kigeni ni wakimbiaji wakubwa wa kulipa kodi [Tax evador].Makampuni hayo yanakimbia kulipa kodi kwa kuyafanya makampuni hayo yaonekane kama yamepata wamilki wapya,ama wakati mwingine yanajitetea kuwa hawa kutengeneza faida kipindi kilichopita.
Nani yuko ndani ya seriklali yetu ambae kazi yake kubwa ni kuakiki kwa ukweli makampuni haya ya kigeni hayatutendei michezo michafu ya kibiashara ya kubadili umilki wa kampuni.?
Natamani kujua ni jukumu la nani kujua kampuni gani imezalisha nini, imepata faida kiasi gani, na imelipa kodi kiasi gani?
zamani nilikua naona milki ya makampuni machache haswa ya migodini yakipenda kubadili umilki wa kampuni moja kwenda nyingine tena wakati mwingine bila kuiambia Serikali. Lakini mchezo huo umeingia mpaka makampuni ya kawaida ya uzalishaji na utoaji wa huduma.
Ni Jukumu la nani kuona Watanzania hawaibiwi?
Nani yuko ndani ya seriklali yetu ambae kazi yake kubwa ni kuakiki kwa ukweli makampuni haya ya kigeni hayatutendei michezo michafu ya kibiashara ya kubadili umilki wa kampuni.?
Natamani kujua ni jukumu la nani kujua kampuni gani imezalisha nini, imepata faida kiasi gani, na imelipa kodi kiasi gani?
zamani nilikua naona milki ya makampuni machache haswa ya migodini yakipenda kubadili umilki wa kampuni moja kwenda nyingine tena wakati mwingine bila kuiambia Serikali. Lakini mchezo huo umeingia mpaka makampuni ya kawaida ya uzalishaji na utoaji wa huduma.
Ni Jukumu la nani kuona Watanzania hawaibiwi?