Makamba: Lowassa ni mroho wa madaraka

Makamba: Lowassa ni mroho wa madaraka

Hivi CCM imeshindwa kabisa kuilazimisha Serikali yao ipeleke mafao ya wastaafu pspf? Kazi ya chama ni nini?

Hao pspf sashivi wameshindwa kabisa, Ukiwapigia simu wanaweza wasipokee siku nzima, siku wakipokea unapewa majibu ya mkatao tu.
Na ukifanikiwa kuunganishwa na watu wa uhasibu, angalau wao ndio wanakupa majibu ya hali ilivyo kwenye file la mtu wenu. Kwamba hazina haijapeleka makato, ila unaweza kuwasiliana na CUSTOMER CARE MANAGER, yeye atajua namna ya kushughulikia madai yenu kwa haraka.

Tatizo sasa, ni namna ya kumpata huyo Customer Care Manager, mara uambiwe hayupo ofisini, mara uambiwe simu yake inaita tu bila majibu. Jamani tufanyeje sasa sisi watu wa huku mbali, na ndugu yetu ni mahututi? BACK TANZANIA

Kutafuta Haki ya kuchaguliwa imekuwa uroho anatafuta mabadiliko aliyoyakosa ndani ya ccm haki yake ya kuchaguliwa ameikosa ccm anaitafuta nje ya ccm ndio atumii mda mwingi kwa maneno mengi yasiyo na tija ni kuomba kura tu
 
Chadema kama kweli wanataka mabadiliko wangeganya fair election kumpata mgombea wa urais
lakin uhuni wa yule dj maarufu aitwaye mbowe ndio ulitawala pale kwenye mchakato

Pili
kama chadema wanataka mabafiliko waanze na katiba yao wenyewe isiyofuata misingi ya kidemokrasia na inayopingana na katiba ya nchi(Article 107A) inayoipa mamlaka mahakama kutoa uamuzi wa mwsho katika kutoa haki lakin katiba ya chadema ukishtak chama mahakaman umekwenda maji
Muulize zito kabwe

ccm kulikuwa na fair election
 
Aliyekuwa mgombea Urais wa CCM ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya chama hicho, Januari Makamba, jana alimshukia mgombea urais kwa tiketi ya Ukawa, Edward Lowassa kwamba ni mroho wa madaraka.

Makamba alitoa kauli hiyo katika viwanja vya Barafu mjini Dodoma wakati akimnadi mgombea ubunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Anthony Mavunde. January alisema kuwa Lowassa ameivuruga demokrasia ndani ya Chadema na kupeleka mizengwe itakayokiua chama hicho na umoja wao.

“Yale siyo mabadiliko kama wanavyojinadi bali ni uroho wa madaraka kwa mtu mwenye uroho na chama chenye uroho, lakini hawezi na hawawezi kushika madaraka ya kuongoza nchi,” alisema Makamba.

Alisema kinachoendelea kwa vyama vinavyounda Ukawa ni maigizo na siyo mabadiliko ya kweli kwa sababu mgombea urais ametoka CCM na Sera za CCM na mgombea mwenza ametoka CUF na sera za huko, hivyo hawawezi kuungana kwa pamoja kwa sababu hawajui nini maana ya kile wanachogombea.

Hata hivyo, Makamba alikiri kuwa uchaguzi wa mwaka huu ni mgumu kuliko uchaguzi wowote uliowahi kutokea katika mfumo wa vyama vingi na akawataka wana CCM kujiandaa kikamilifu.

Alisema CCM kinapaswa kuwa makini na imara wakati wote ili kutoyumba na wakifanya hivyo watajikuta wanapata mchanganyiko ambao utaleta shida katika maendeleo.

Kwa upande wake mgombea ubunge Mavunde alijipachika jina la Mr Makao akisema lazima ataipelekea Dodoma hadhi ya kweli katika kufikia makao ambayo yamekuwa yakisemwa kama hisani.

Mavunde aliomba wananchi kumwamini na kumpa nafasi hiyo kwani ana uhakika kwa miaka mitano ataifanya Dodoma kupaa kiuchumi huku akisema atashughulika na watu wenye kipato cha chini pamoja na kumaliza migogoro ya ardhi.

Chanzo: Mwananchi

kifo cha ccm kimekalibia maana hawa jamaa kwenye majukwaa hawana xera zaid ni vijembe tyu kama waimba taarabu na kuukwel mwaka huu kampen kwa ccm zimekuw ngumu maana hawana jipya kwa wananchi mm nilitegemea kumsikia magufuli akusema ccm imejenga viwanda 1000 ambavyo vimetoa ahira 100000000000 kwa wana nchi mkinipa nafasi nitaongeza vingine ili kupanua ajira kwa watanzania ange kuwa anasema ivyo naamin ukawa ingekuw kwenye wakat mgumu kwenye kampen ila xaxa utamsikia magufuli akixena ndugu zangu watanzaniia nashangaa nchi hii haina viwanda!na shangaa kuona majiz yanaiba serikalin haikamatwi nashangaa watu ni maskini yan anaingea utadhan ccm haijawah kabisa kutawala

xaxa cc kama wapenda mabadiliko ambao tunaijua vizur ccm na imeongoza kwa kipind kilefu mwaka huu tunasema ccm baaasi tumichoka wangie wengine nao waongoze na lowasa kama wao ccm hawamtaki cc wananchi ndio tushampenda nawao kama hawa uchu wa madaraka wange kaa kimya wasipige kampen tena hapo kwenye uchu ccm uchu wao umezid na wanalazimisha watu wawapende kwa kubeba wasanii weeeng utadhan wanaenda kufanya shoo za fiesta.

pili wana simbelea watu kwenye maroli kama ng'ombe na wakipita barabaran trafk hawawakamati kwa kuvunja shelua za barabaran tatu kwaku toa maneno ya kashfa na kejeli kwa mgombea wa ukawa.nne mwisho wao tarehe 25/10/2015 saa nne asubuhi
 
Hatutaki kikazi cha makamba kututawala. Huyu jamaa kamaliza shule juzi juzi tuu eti sasa ni waziri. Kweli mtaisoma namba.
 
Aliekuwa Mgombea wa Urais kupitia *UKAWA 2015* amezidi kuushangaza umma kutokana na *KIU* na *UCHU* wa madaraka alionao, Leo nimeona niseme jambo kwa niaba ya Familia yangu, na baadhi ya ndugu zangu Waislamu ambao nimezungumza nao nikaona niseme jambo kidogo kwa niaba yao.

Mtakumbuka katika uchaguzi uliopita huyu *Bwana Edward* alianza kampeni zake vibaya kwa kusema safari hii Urais lazima uende kwa watu wa Kaskazini mwa Tanzania hapa tunazungumzia Wachaga, wameru, wamasai na wapare kidogo na Tanga japo sio sana, alianza kampeni kwa kutumia Mwanya wa kuwachonganisha Wachaga na watanzania na katika mapambano hayo baadhi ya Wachaga waliokuwa wanamuunga mkono *Edward* walishindwa dhidi ya watanzania walio wengi, ushahidi wa hili tunaujua na kuufahamu, ukabila huu ukawafanya wachaga, wameru, na wamasai kuonekana victims, Leo wanajuta Dhambi ya *UKABILA* waliyoifanya.

Akiwa katikati ya mwendo alibadilisha Gia na kuongeza Gia ya *UDHEHEBU*, alijaribu kuwahamasiha *WALUTHERI* kwa kuwaaminisha ni *ZAMU* yao ya kuongoza nchi, hili likawagawa *WAKRISTO* katika hili nako hakufanikiwa akaanguka mana *Mungu* hadhihakiwi, ushahidi wa hili mnajua kupitia mahubiri yake pale kanisani *KKKT.*

Pamoja na kushindwa kwa mbinu hizi, wananchi tukiwemo sisi Waislamu tulimpa *KURA* *Mhe, Dkt. John Pombe Magufuli* kuongoza nchi, lakini kilichotokea kwenye kipindi cha Mfungo wa Mwezi mtukufu wa Ramadhani kimenifanya niwaze Haya yafuatayo :-

1. Huyu *Bwana Edward* ametumia fursa ya kipindi kile cha Njaa kuchonganisha wananchi na Serikali.

2. Alitaka watumishi *HEWA* waendelee kulipwa kwa kuwa alijua baadhi ya watoto wake na marafiki zake wanahusika.

3. Alitaka pia wala *Rushwa* wakubwa wasikamatwe nadhani mnakumbuka kesi ya *MKWE* wake Bw Sioi Sumari na Harry Kitillya kamishna wa *TRA* wako ndani bado.

Lakini kama haitoshi ameanza kututumia baadhi yetu *WAISLAMU* kwa kututaka *TUMTUKANE na KUMDHALILISHA* Rais wa Nchi Mhe, *Dkt. John Pombe Magufuli* kupitia MISIKITI yetu kama alivyokuwa akimtumia Mshenga wake *Askofu GWAJIMA* kuwatukana Viongozi wa Dini na Serikali ambao hawakumuunga mkono *Edward* kumbuka mvua ya matusi kwa *Kadinali PENGO,* alimtukana sana *Mhe Jakaya Mrisho Kikwete* kwa kuwa Kikwete *ALIGOMA* Kumuunga mkono *Lowassa* Shauri ya Kashfa ya *UFISADI,* *Gwajima* mpaka kesho a naendelea kumtukana *MAKONDA* kwa kuwa tu *Makonda* alikuwa Miongoni mwa watu ambao hawakumuunga mkono *Edward.*

Sisi Waislamu Tunajua kuwa hatupaswi kuchangamana na Viongozi wa Aina hii ya kisasa wanaotumia viongozi wa Dini kuhatarisha *AMANI* ya nchi, Tunajua Askofu *Gwajima* alikuwa *MSHENGA* wa Ndoa ya *Edward* na *UKAWA* katika kugombea Urais, sasa ameona Askofu *Gwajima* Hana *MVUTO* na kama kashindwa kumng'oa *Makonda* Dar es Salaam kamwe *HATAWEZA* kumtoa *Magufuli IKULU,* sasa anatukumbuka Waislamu ameanza kutufuata na sisi.

Leo hii *Edward* anasahau Sharia ya nchi inayowaelekeza viongozi wa Dini kutumia Nyumba za ibada *MISIKITI* na *MAKANISA* kama Nyumba za ibada, badala yake *Edward* anazitumia kama uwanja wa siasa kwa kushangaa kwanini *WAISLAMU* tunampenda *Rais Magufuli* na Serikali yake, kwanini Waislamu Leo tunaelewana na dini nyingi bila vurugu, anashangaa kwanini Waislamu tunafanya ibada bila vurugu a nashangaa kwanini hakuna maandamano Mkoa wa Dar es Salaam, *BADO ANASHANGAA.*

*Edward* yeye anataka tuandamane na kuleta vurugu anataka tufanye mihadhara ya matusi na kukashifiana anataka Turudi kwenye *UAMSHO,* hivi jamani huyu ni mtu wa Aina gani?

*Edward* ameona *AMANI* ya nchi haifai mpaka anataka tumwage damu kisa tu yeye *HAJAPATA URAIS?*

Sisi Waislamu tu naona *UZALENDO* wa Mhe Rais, *Dkt. John Pombe Magufuli* katika kulinda *RASILIMALI,* mapambano dhidi ya Rushwa na uzembe Mambo ambayo hata sisi Waislamu yanapingana na vitabu vyetu vitakatifu.

*Edward Lowasa* tukukumbushe umishaambiwa na Baba wa Taifa Mwalimu *Julius Kambarage Nyerere* kuwa *HUFAI* kuwa Rais wa Nchi, Waislamu Tunajua huo wosia wa baba wa taifa na *KAMWE* hatuwezi kumgeuka na kumsaliti baba wa taifa, alishatuambia wewe *HUFAI.*

Nimalizie tu kwa kukuuliza Haya Maswali hapa :-

1. Hivi huoni *Magufuli* alituletea Mfalme wa Morocco ambae ametukumbuka na sisi Waislamu kwa kuamua kutujengea msikiti mkubwa sana wa kimataifa ambao utakuwa mkubwa Afrika Mashariki?

2. Mteule wa Rais, ambae ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam *Mhe Paul Makonda* anajenga *MAKAO MAKUU YA BAKWATA* jambo ambalo halijawai kufanyika tangu *UISLAMU* umeingia Tanzania!

3. Hivi *Edward* huoni katika mwezi wa ramadhani unaomalizika waumini wa Dini ya Kiislamu Mkoa wa Dar es Salaam tunavyopata upendeleo wa Serikali ya Mkoa, Unashangaa *Dar es Salaam* kukaa kimya?

Hivi *Edward* Unakumbuka kuwa aliewahi kukwambia *HUFAI* kuwa Rais mwaka 2013, ndie anaeongoza huu Mkoa?.

Sisi Waislamu hatuwezi kuiangusha serikali ya awamu ya tano mana hata mali na viwanja vyetu vilivyoporwa sasa vimeanza kurejeshwa katika utawala huu wa Mhe Rais, *Dkt. John Pombe Magufuli.*

Kazi yetu kubwa kwa sasa ni Kumuombea kwa *Allah* Mhe Rais, *Dkt. John Pombe Magufuli* na Serikali yake yote *Allah* awafanyie *WEPESI* katika kutekeleza majukumu yao na kutuletea maendeleo, tunakuomba usitupatie pipi za pemende uku ukijua ndani yake umeweka madawa ya kulevya na kupumbaza akili, kwa sasa tuko mstari wa mbele katika mapambano ya ulinzi wa *RASILIMALI* zetu wewe unataka kutuondoa kwenye Huu mjadala muhimu wa ulinzi wa *RASILIMALI* zetu.

Mwisho tunamuomba Mhe Rais, *Dkt. John Pombe Magufuli* akishamaliza na kwenye Madini, arudi na kwenye *RICHMOND* kuna kiporo kimebakia hapo mana Tunajua *MUHUSIKA* Mkuu bado upo.

Nawatakia sikukuu njema ya Eid Alfitr.

*Khamis hussein* *Mwinchande*
*Lushoto, Tanga,*
*Tanzania.*
*27/06/2017*
 
Sidhani kama mtoa post usingizi umekuacha salama,au kama umeoa basi usiku ulopita umenyimwa unyumba.
 
Angekuwa mroho wa madaraka asingejiuzulu uwaziri mkuu kirahisi vile angeng'ang'ana tu !! ( ndio tabia ya waroho wa madaraka )
 
Back
Top Bottom