Makamba kung'olewa ukatibu?

MAKAMBA.jpg


Jamani, Jamani, Jamani, mbavu zanguuuuuuuuuuuuuuuuu!!!!!
 
Makamba anafanya kazi kwa maelekezo maalumu toka kwa mwenyekiti wake Kikwete na marafiki zake Lowasa na Rostam. He is just a kikaragosi, wasimlaumu..
By the way wanalalamika sasa kwani hawakuona tangu mwanzo kuwa Makamba ni kilaza? Huu ndio unafiki wa wanasiasa wa Afrika. Uwezo wa kiongozi kuongoza unahojiwa pale anapogusa maslahi binafsi ya mtu..

Kwa sasa chama hakihitaji katibu mkuu smart. Akiwa smart atakuwa challenge kwa mweyekiti. Katibu mkuu wa Chama na Waziri mkuu wakiwa watu smart urais wa JK utakuwa mashakani (authoritywise) ni vizuri Yusuff aendelee hadi JK atakapoacha kuwa rais. Hata hivyo kwa sasa ukiangalia kwa makini unaweza kuona kuwa hakuna mwenye interest ya kuendeleza na kuimrisha chama, watu wanakitumia tu chama kwa sababu zao binafsi.
 
Sasa mzee wa vinywaji,
Hivi tukisema au kuianzisha hii Issue kuwa kubwa na kuwa huyu mzee alilipitisha au kubadilisha mapendekezo ya Bilal kwa NEC ili yawe in favor of his Son January Makamba atabisha huyo Yusuph Makamba mwenyewe??

Katibu Mkuu antaka kusaha kuwa waliwawajibisha makatibu wa wilaya ya Bukombe na kuhamishwa immediately the same night pale wagombea waliposema hawana imani na katibu wa wilaya na pia ndicho kilicho tokea kwa Mr. Mzuri pale DODOMA na kutupwa Morogoro na kushushwa cheo kwa kumsaidia KIMBISA na ndilo lilikuwa kosa lake kwani familia ya mzuri iliweka wazi wazi mjini dodoma kuwa inamsaidia kimbisa kwani watoto wa mzuri mpaka baba yao ameamishwa wao walikuwa wanaendelea msaidia kimbisa kampeni wilaya ya dodoma mjini, kila kukicha wakishida vijijini esp Hombolo.

Sasa leo makamba anasahau kusimamia katiba na mashauri yaliyopendekezwa na kuvuruga uchaguzi wa kura za maoni kwanini wana CCM wasi gome kwa hilo au kumsurubu Katibu wao Mkuu Mr.Y.Makambaaaaa?

Mkuu,

Kadi feki zilikuwepo nyingi tu na Makamba inatakiwa awajibike kwa uzembe huo.

Hizo kadi zilikuwa fake kwa maana ya kwamba hazikufuata utaratibu lakini ki ukweli ni kadi ambazo zilitoka makao makuu ya CCM kinyemela kwa lengo la kuwasaidia baadhi ya watu.

Kama kule Kyela kadi nyingi tu zilikamatwa na uchunguzi wa CCM mkoa na taifa ulibaini waliozipeleka huko lakini hakuna hatua iliyochukuliwa.

Labda wakati umefika kwa Makamba kutupwa na kumruhusu katibu mpya kuendesha uchunguzi wa kina kujua nani walihusika na kuwachukulia hatua.

Wakati watu ambao wamekuwa wakishiriki kazi za CCM miaka na miaka hawakuwa na kadi, lakini wale vijana ambao hata hawajawahi kushiriki hata mkutano mmoja wa CCM walipewa kadi kimyemela.

Makatibu wengi wa wilaya walihusika kuvuruga taratibu kwa makusaudi.

Kama CCM wanataka kusalimika 2015 wamwondoe huyu mzee na kuleta mtu mpya. Kinana angefaa zaidi kuleta utendaji mzuri ndani ya chama.

Pia makatibu wengi wa wilaya wamewekwa kwa kujuana bila kuwa na uelewo wa maana katika utendaji. CCM inahitaji restructuring kubwa ili angalau iwe tayari kwa 2015. Vinginevyo haya ya mwaka 2010 yatatokea tena 2015.
 
Yawezekana wengi hawajui umuhimu wa Makamba CCM. Akiondoka nitaumia sana. Chonde chonde CCM tubakishieni Makamba:
 
Wakimng'oa itakua busara kuu....Jamaa huwa hafikiri kabla ya kuongea.......

CCM juu ya mabaya yake yote wana busara na wamekomaa kidemokrasia huwa hawafukuzani ila mtu akishindwa huondoka mwenyewe mfano Fred Mpendazoe mzee wa CCJ, Shibuda na Kitila Mkumbo.

So at end of the day Makamba ataendelea kuwa kwenye system na mjumbe wa kudumu wa CC ya CCM.
 
Unless Mnajimu wao sheikh Yahaya atabiri kuondoka kwake ndio watamuondoa. Mie nadhani Makamba wanamuonea tuu, yanayojitokeza CCM ndio hali halisi ya chama chenyewe kwa ujumla wake sio tatizo la Makamba.
Ni kweli kabisa
 
Huyu jamaa leo atapata chakula au ataambulia patupu mlioko idodomya mtujuvye

MAKAMBA.jpg
 
Back
Top Bottom