Makamba Asema TTCL Sasa ya Watanzania!

Makamba Asema TTCL Sasa ya Watanzania!

K-Boko

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2013
Posts
697
Reaction score
218
Waziri January Makamba analiambia Bunge hivi sasa kuwa TTCL sasa imerejeshwa kwenye mikono ya Umma baada ya serikali kununua hisa zilizokuwa zikimilikiwa na mwekezaji Airtel (35%). Nadhani ni jambo jema sana!
 
TTCL walihujumiwa sana.......Mfano mpaka leo wana minara ya kurushia mawasiliano lakini hawatakiwi kurusha ili waweze kuuza simu za mikononi, kama siyo kuhujumiwa ni nini?............
 
Wamenunua kiasi gani? Hawakawii kutengeneza ka escrow kengine hao.
Waweke wazi hiyo ni mali ya umma lazima tujue ili ikibidi tuwapongeze kwa haki
 
Hilo ni jambo jema na neema kwa watanzania kwani lina maslahi kwa umma.
 
Waziri January Makamba analiambia Bunge hivi sasa kuwa TTCL sasa imerejeshwa kwenye mikono ya Umma baada ya serikali kununua hisa zilizokuwa zikimilikiwa na mwekezaji Airtel (35%). Nadhani ni jambo jema sana!

Wait a second, Huyu mwekezaji aliuziwa hizi hisa asilimia 35 bila ya yeye kulipa fedha za mauzo ya hisa hadi leo hii. Mbaya zaidi alitumia resources za TTCL kwa miaka nenda rudi kwa manufaa yake binafsi.

Je, huyu mwekezaji alilipa fedha alizotakiwa kulipa ili kumilikishwa asilimia 35 ya TTCL?Kama alilipa, Serikali inaweza kutueleza amelipa lini,na kupitia valuation gani?

kama hayo hayakufanyika,Kwa nini serikali implipe huyu mwekezaji hewa fedha za hisa alizopewa bila kuzilipa?Na kama wamefanya hivyo wamelipa kwa huyu mwekezaji kiasi gani?

TTCL tumeambiwa ina negative equity, kwa nini kampuni yenye negative equity itoe pesa kumlipa mbia ambaye ni sehemu na sababu ya hiyo negative equity(provided alilipia hisa zake).

Something is not right here.

I sincerely hope Makamba was misquoted.
 
natamani muwekezaji achukue jumla hili shirika, TANESCO, BOT etc.
 
Wait a second, Huyu mwekezaji aliuziwa hizi hisa asilimia 35 bila ya yeye kulipa fedha za mauzo ya hisa hadi leo hii. Mbaya zaidi alitumia resources za TTCL kwa miaka nenda rudi kwa manufaa yake binafsi.

Je, huyu mwekezaji alilipa fedha alizotakiwa kulipa ili kumilikishwa asilimia 35 ya TTCL?Kama alilipa, Serikali inaweza kutueleza amelipa lini,na kupitia valuation gani?

kama hayo hayakufanyika,Kwa nini serikali implipe huyu mwekezaji hewa fedha za hisa alizopewa bila kuzilipa?Na kama wamefanya hivyo wamelipa kwa huyu mwekezaji kiasi gani?

TTCL tumeambiwa ina negative equity, kwa nini kampuni yenye negative equity itoe pesa kumlipa mbia ambaye ni sehemu na sababu ya hiyo negative equity(provided alilipia hisa zake).

Something is not right here.

I sincerely hope Makamba was misquoted.

Moderators nawaomba muipandishe hii pale juu kama muendelezo wa hoja aliyoleta Original Poster.

Kuna mambo mengi yanahitaji ufafanuzi kwenye hii transaction.
 
TTCL....BOT...TANESCO...IPTL...NBC....UDA...RICHMOND👉 DOWANS 👉 SYMBIONS, ATCL...Yameiangusha sana nchii hii...BANDARI YA DAR ilitutia loss uncountable...ila sasa inachechemea..but itaanza wizi tena...TAZARA inafufuka kidogo kidogo...!!!!

HAYO HAPO JUU YANGEWEZA KUWA KAMA NHC ya leo....tungekuwa mbali sana.....kwani NHC nayo ilikuwa in coma...sasa imezinduka...!!!

Tujiulize yote haya ni KWANN TUNA FELI HV...!!?


WATU HAWANA UZALENDO....uwizi, ufisadi umetawala

So NI NGUMU SANA KUENDELEA IF MINDSET ZA WALIO MADARAKANI WAKO KIUWIZI UWIZI NA UFISADI....!!!!
 
Waziri January Makamba analiambia Bunge hivi sasa kuwa TTCL sasa imerejeshwa kwenye mikono ya Umma baada ya serikali kununua hisa zilizokuwa zikimilikiwa na mwekezaji Airtel (35%). Nadhani ni jambo jema sana!

Kama kampuni imefilisika thamani ya hizo hisa inapatikana vipi? Kama Serikali imeilipa Airtel kununua hiza za kampuni ambayo ni mufilisi huu nao ni ufisadi wa mchana kweupe
 
Mwaka huu tutasikia cement inauzwa shilingi za Tanzania 1675.50/=
 
Waziri January Makamba analiambia Bunge hivi sasa kuwa TTCL sasa imerejeshwa kwenye mikono ya Umma baada ya serikali kununua hisa zilizokuwa zikimilikiwa na mwekezaji Airtel (35%). Nadhani ni jambo jema sana!
Linakuwaje jambo jema hapo. Hili shirika lilikuwa letu asilimia 100 na hatukusaidiwa na mtu kulianzisha. Wajanja wakawapa watu wa nje bure. Wamechuma na kwa rasilimali zetu wakaanzisha airtel ambayo nayo wametuibia. Sasa wanatuuzia kilicho chetu na tunashangilia!
 
Hilo ni jambo jema na neema kwa watanzania kwani lina maslahi kwa umma.
Kweli wajinga ndo waliwao! Umethibitishaje kuwa anayoyasema January Ni ya kweli? Kwanini TTCL haikurudishwa mikononi kwa wananchi miaka 10 iliyopita au basi angalau mwaka jana? Kwanini 2015?
 
chonde chonde; uchaguzi umekaribia. tuwakumbushe wanetu na wake zetu juu ya hii janja ya nyani.
 
Back
Top Bottom