Habarindiyohiyo
JF-Expert Member
- Aug 11, 2008
- 263
- 13
Yule kijana msomi mchakapakazi, Amosi Makala amefanikiwa mpaka sasa kumzidi kete mpinzani wake Suleman Sadiq "Murad". Bwana Makala ambaye amefanikiwa kujijengea jina Mvomero kutokana na uadilifu wake wa kupinga ufisadi katika viwanda miwa vya Mtibwa ambao unamuhusisha pia Rais Mstaafu Benjamini Mkapa. Tofauti na mwenzake Murad, Amos Makala amekuwa akisifiwa kote vijijini kutokana na kuwa upande wa wananchi, anaeleza mchambuzi wa masuala ya kisiasa.
Hadi sasa, vita ya wazi katika majimbo ya ubunge imeanza kujitokeza katika jimbo la Mvomero, Mkoani Morogoro ambalo linaongozwa na Suleiman Sadiq 'Murad'. Katika jimbo hilo, msuguano wa wazi, unaonekana kuwa umeanza baina ya Murad na aliyekuwa Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UV-CCM) Amos Makala(Kwa sasa ni Mweka hazina wa chama hicho) ambaye alibwagwa mwaka 2005 kwa kura 540. Ukweli wa hilo umejitokeza katika ziara ya hivi karibuni aliyoifanya Makala katika maeneo mbalimbali ya nchi, ikiwemo jimbo la Mvomero. Hata hivyo, wakati Makala akieleza kufanya ziara kwa lengo la kuimarisha chama, Murad amekuwa akilalamika ziara hiyo kwa maelezo kuwa kiongozi huyo wa UV-CCM aliingia jimboni humo na kuitisha vikao vya vijana bila wenyeji kujua. Makala aliiambia Mwananchi Jumapili wiki hii kwamba, hakuvamia Mvomero kama anavyovumishiwa na wabaya wake, bali alikwenda kama sehemu ya kuimarisha chama na kusisitiza kuwa kamwe Mvomero haiwezi kuwa kisiwa. "Nilikwenda Mvomero, lakini Murad akasema nimevamia jimboni kwake, sikuvamia, nilitoa taarifa, Mvomero haiwezi kuwa kisiwa, Murad anaogopa kivuli cha uchaguzi," alisema Makala akifafanua kuhusu shutuma hizo. Hata hivyo, Murad naye kama ishara ya kujibu mapigo aliliambia Mwananchi Jumapili kwa njia ya simu jana, kwamba kwa sasa hahitaji malumbano na Makala kwani amekwisha kulifikisha suala kwa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC). Lakini Murad alithibitisha kauli yake kwamba Makala alifika katika jimbo hilo bila viongozi wengine kufahamu na kutamba kwamba yeye anatekeleza ilani ya chama kwa kaulimbiu ya nguvu, kasi na ari mpya na wala haogopi kivuli cha uchaguzi kwani hadi sasa ni mbunge na ana imani kuwa atashinda tena mwaka 2010. "Lakini labda nikueleze, sasa hivi sihitaji malumbano, hili suala nimesha likabidhi katika Halmashauri Kuu, sasa hivi natekeleza ilani kwa kasi," alisema Murad katika mahojiano yake na Gazeti la Mwananchi Jumapili.
.....ndiyohiyo
Hadi sasa, vita ya wazi katika majimbo ya ubunge imeanza kujitokeza katika jimbo la Mvomero, Mkoani Morogoro ambalo linaongozwa na Suleiman Sadiq 'Murad'. Katika jimbo hilo, msuguano wa wazi, unaonekana kuwa umeanza baina ya Murad na aliyekuwa Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UV-CCM) Amos Makala(Kwa sasa ni Mweka hazina wa chama hicho) ambaye alibwagwa mwaka 2005 kwa kura 540. Ukweli wa hilo umejitokeza katika ziara ya hivi karibuni aliyoifanya Makala katika maeneo mbalimbali ya nchi, ikiwemo jimbo la Mvomero. Hata hivyo, wakati Makala akieleza kufanya ziara kwa lengo la kuimarisha chama, Murad amekuwa akilalamika ziara hiyo kwa maelezo kuwa kiongozi huyo wa UV-CCM aliingia jimboni humo na kuitisha vikao vya vijana bila wenyeji kujua. Makala aliiambia Mwananchi Jumapili wiki hii kwamba, hakuvamia Mvomero kama anavyovumishiwa na wabaya wake, bali alikwenda kama sehemu ya kuimarisha chama na kusisitiza kuwa kamwe Mvomero haiwezi kuwa kisiwa. "Nilikwenda Mvomero, lakini Murad akasema nimevamia jimboni kwake, sikuvamia, nilitoa taarifa, Mvomero haiwezi kuwa kisiwa, Murad anaogopa kivuli cha uchaguzi," alisema Makala akifafanua kuhusu shutuma hizo. Hata hivyo, Murad naye kama ishara ya kujibu mapigo aliliambia Mwananchi Jumapili kwa njia ya simu jana, kwamba kwa sasa hahitaji malumbano na Makala kwani amekwisha kulifikisha suala kwa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC). Lakini Murad alithibitisha kauli yake kwamba Makala alifika katika jimbo hilo bila viongozi wengine kufahamu na kutamba kwamba yeye anatekeleza ilani ya chama kwa kaulimbiu ya nguvu, kasi na ari mpya na wala haogopi kivuli cha uchaguzi kwani hadi sasa ni mbunge na ana imani kuwa atashinda tena mwaka 2010. "Lakini labda nikueleze, sasa hivi sihitaji malumbano, hili suala nimesha likabidhi katika Halmashauri Kuu, sasa hivi natekeleza ilani kwa kasi," alisema Murad katika mahojiano yake na Gazeti la Mwananchi Jumapili.
.....ndiyohiyo