Herbalist Dr MziziMkavu
Platinum Member
- Feb 3, 2009
- 43,069
- 34,839
"Wakitukamata huwa wanasema kosa letu ni kufanya ukahaba, lakini tukifikishwa kortini kosa linabadilika na kuwa uzembe na uzururaji, wakati wametukamata vyumbani kwetu ," alisema Judith.
Mkuu EMT na MziziMkavu:
Hivi Sheria ya Tanzania inasemaje kuhusu "ukahaba"? maana hii quote hapo chini inaonyesha kama vile ki-sheria za Tanzania ukahaba siyo "kosa":-
Mkuu, Kifungu gani cha sheriaKufanya ukahaba ni kosa la jinai.
Mkuu, Kifungu gani cha sheria
Kenyela anautaka ukamanda wa kanda maalmu kwa nguvu sana
Kama sijakosea ni Kifungu cha 12 cha Sheria ya Makosa ya Kujamiiana.
Kifungu hiki kinafanya marekebisho kifungu cha 139 cha Kanuni za Adhabu.
Mkuu hii ni section 139 (1) (a) ya Penal Code: Any person who, procures, or attempts to procure, any person, whether male or female of whatever age, whether with or without the consent that person, to become, within or outside the United Republic of Tanzania, a prostitute. Hapa sioni wanapokataza prostitution
Mkuu EMT na Ngambo Ngali nawashukuru sana,
Nadhani the bottom line ni kuruhusu - legalize - hii biashara, maana nadhani kwanza maana ya "kahaba" haitoi nafasi kwa mahakimu kumtia hatiani huyu mtu anayekamatwa na polisi kwa hatia ya "ukahaba"...! Halafu pia nadhani na upelelezi wake ni mgumu sana...!
Hicho kifungu ulichokitaja ni moja ya vifungu vinavyo-define prostitution.
Unless kama kuna mabadiliko yaliyofanywa hivi karibuni, kifungu cha 12 cha Sheria ya Makosa ya Kujamiiana ambacho kilifuta kifungu 139 cha zamani cha Kanuni za Adhabu na ku-replace na kifungu kipya cha 139 kinasema kuwa prostitution hili ni kosa la jinai na adhabu yake ni kifungo kisichopungua miaka 10 jela na faini isiyopungua sh 100,000 na isiyozidi sh 300,000 au vyote kwa pamoja.
Mkuu EMT, najaribu kusoma kifungu 139 kama kilivyorekebishwa na sheria namba 4 ya mwaka 1998 bado sioni mahala wanapokataza. Nimeangalia chapter XIV yote sioni mahala wanapokataza, inanifanya nishawishike kuwa hakuna kosa la jinai la prostitution Tanzania.