ipogolo
JF-Expert Member
- Aug 15, 2011
- 6,275
- 5,961
Wanabodi,
Kama ni kweli Ngwajima ana waumini wasiopungua elfu sabini na wanaenda kanisani mara mbili kwa wiki basi Ngwajima anaingiza zaidi ya bilioni tatu kwa mwaka (makadirio ya chini kabisa)
NI HIVI:
Tufanye kila muumini wake hutoa sadaka ya sh. 500 tu-hiyo ni flat rate, ina include waliotoa elfu kumi, waliotoa sh mia na wasio toa kabisa.
Hivyo basi kwa siku moja kwa waumini 70,000 wakitoa sh 500 ni sawa na sh milioni 35. Kwa wiki wanaenda mara mbili hivyo ni sawa na sh milioni 70.
Kama kwa wiki anaingiza milioni 70, je kwa mwezi anaingiza kiasi gani? Uki cross multiplication utapata milioni 280
Kama kwa mwezi anaingiza milioni 280, je kwa mwaka anaingiza kiasi gani? uki cross tena multiplication utapata bilioni 3 na milioni 360. Sasa piga hesabu kwa miaka yote aliyotoa huduma ameingiza sh ngapi?
Kwa mantiki hiyo pesa aliyonunulia Hummer aliipata ndani ya mwezi mmoja tu.
Achilia mbali fungu la kumi na pesa mbali mbali anazopewa kama zawadi, hapo tumepiga hesabu ya sadaka tu.
NAMALIZIA, Biblia inasema "vya madhabahuni vitaliwa na wamadhabahuni" full stop.
Posted by: MCHUNGUZI HURU (Associate Professor)
Mzee hao waumini 70,000 walijiunga wote siku moja? Ninadhani alianza kidogo kidogo.
Watu 70,000 Ni idadi kubwa sana ya watu kukutana Mara moja kanisani. Kumbuka Uwanja wa Taifa unakadiriwa kumeza watazamaji waliokaa 60,000.
Halafu. hizo sadaka hutumika kwa matumizi mbali mbali kila siku iendayo kwa Mungu.
Last edited by a moderator: