tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 23,074
- 20,615
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, mahakama wilayani Bunda zimeshindwa kufanya kazi baada ya makada wa CCM wanaokabiliwa na tuhuma mbalimbali za ufisadi kuwatisha mahakimu wanaohudumu ktk mahakama hizo.
Mahakimu hao wameogopa kufungua mahakama na kuwahudumia wananchi baada ya kupokea vitisho vya kuuawa na watuhumiwa hao wa ufisadi. Kabla ya kuamua kusitisha huduma kwa wananchi, mahakimu hao walifanyiwa vurugu wakiwa mahakamani na kuponea chupuchupu kuumizwa.
Mahakimu wote mkoani Mara wameapa kuwaunga mkono wenzao na wanataka uchunguzi ufanyike ili kuwakamata na kuwachukulia hatua makada hao; na pia wameomba mahakimu wapewe ulinzi wa polisi vinginevyo hawatafanya kazi ng'o.
Mtuhumiwa mkuu katika kadhia hii ya vitisho kwa mahakimu ni mbunge (ambaye hakutajwa jina) akishirikiana na makada kadhaa wa CCM wanaotuhumiwa kwa tuhuma za ufisadi.
Source: ITV
MAONI YANGU:
Naona sasa makada hawa wamefika hatua mbaya sana. Kitendo cha mafisadi kuwatisha mahakimu ni cha hatari sana. Tunapaswa kuwalaani watu hawa.
Mahakimu hao wameogopa kufungua mahakama na kuwahudumia wananchi baada ya kupokea vitisho vya kuuawa na watuhumiwa hao wa ufisadi. Kabla ya kuamua kusitisha huduma kwa wananchi, mahakimu hao walifanyiwa vurugu wakiwa mahakamani na kuponea chupuchupu kuumizwa.
Mahakimu wote mkoani Mara wameapa kuwaunga mkono wenzao na wanataka uchunguzi ufanyike ili kuwakamata na kuwachukulia hatua makada hao; na pia wameomba mahakimu wapewe ulinzi wa polisi vinginevyo hawatafanya kazi ng'o.
Mtuhumiwa mkuu katika kadhia hii ya vitisho kwa mahakimu ni mbunge (ambaye hakutajwa jina) akishirikiana na makada kadhaa wa CCM wanaotuhumiwa kwa tuhuma za ufisadi.
Source: ITV
MAONI YANGU:
Naona sasa makada hawa wamefika hatua mbaya sana. Kitendo cha mafisadi kuwatisha mahakimu ni cha hatari sana. Tunapaswa kuwalaani watu hawa.