Mahakama yetu imedumazwa na CCM au ina Majaji wenye uwezo hafifu?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
17,871
33,236
Kwenye bandiko hili pale litakapotumika neno Jaji au Majaji ndiyo itajumuisha pia na mahakimu toka mahakama za mwanzo mpaka Mkoa.

Sisi kama Taifa tumerithi mfumo wa kale na maarufu zaidi wa kuwa na serikali ya kijamhuri (Republic). Ndani ya mfumo huo kunakuwa kuna mgawanyo wa kimadaraka kati ya matawi matatu yanayounda serikali, yaani Bunge, Mahakama na Utawala.

Kwa mfumo huo matawi mawil ya Bunge na Utawala huongozwa na wanasiasa wakati tawi la Mahakama huongozwa na Majaji wanaoteuliwa pia na wanasiasa. Kinadharia matawi haya matatu hutakiwa kuwa huru na kila tawi kuwa na uwezo fulani wa kusimamia msawaziko wa tawi Jingine.

Kwa Tanzania inaonekana kuwa Mahakama yetu inaendeshwa zaidi kwa kufuata matakwa ya tawi la Utawala na hata wanasiasa waliomo kwenye tawi la utawala wakati fulani hugoma kutekeleza maamuzi ya Mahakama na mahakama huwa inakaa kimya.

Wengi wetu tuna uzowefu kwamba jambo la kisiasa likipelekwa kwenye mahakama zetu kama liko kinyume na maslahi makubwa na tawi la Utawala ama chama kilichoko madarakani, basi mahakama hushindwa kufanya maamuzi kwa wakati ama ikifanya maamuzi ni lazima yaegemee upande wa Watawala au chama kilichoko madarakani yaani CCM.

Kuanzia uamuzi wa Mgombea binafsi mpaka Ubunge wa Lissu kule Singida Mashariki na sasa kesi ya Wabunge 19 wa CHADEMA, bado mtu wa kawaida kabisa mtaani anashangaa ni kwa nini jambo la wazi kama la hao wabunge linaweza kuchukua zaidi ya miaka 3 kuamuliwa.

Nimeandika makala haya baada ya kusisimuliwa na Uamuzi wa Mahakama Kuu ya Pakistan kutangaza kwamba kukamatwa kwa kiongozi wa chama cha siasa cha Pakistan Tehreek-e-Insaf (PTI) Imran Khan, kuwa kulikuwa batili.

Yaani Khan kakamatwa Jumanne na leo Mahakama Kuu inatoa uamuzi kwamba kukamatwa kwake ni batili, kwa Tanzania inawezekana kweli? Mahakama zetu linapokuja suala dhidi ya watawala ama CCM huwa haina uwezo wa kufanya maamuzi kwa wakati.
 
Tanzania hakuna mahakama, bali kuna majengo ya mahakama yanayoendeshwa na Makada wa CCM. Kesi ya uchaguzi nafasi ya urais hapo Kenya imefanyika ndani ya muda mfupi, na hukumu imeshatoka, lakini hapa hii ya Covid 19 ni porojo tupu.

Haya ni madhara ya kuwa na chama kimoja kukaa madarakani muda mrefu kwa shuruti, matokeo yake mifumo yote inageuka kuwa dhaifu.
 
Hakimu kama yule aliye pandishwa kuwa Jaji na Magu simply kwa kuandika hukumu Kiswahili na sio kwa
weledi wake unadhani ikija kesi ya aliye mteua kutakuwa na haki.
Na kwa nchi sitashangaa kutumia Kiswahili kwani Kiingereza lugha ya sheria ni shida kwake.
 
Hakimu kama yule aliye pandishwa kuwa Jaji na Magu simply kwa kuandika hukumu Kiswahili na sio kwa
weledi wake unadhani ikija kesi ya aliye mteua kutakuwa na haki.
Na kwa nchi sitashangaa kutumia Kiswahili kwani Kiingereza lugha ya sheria ni shida kwake.
Kwa ivo ni ngumu sana kwa mfumo wa mahakama kufanya kazi zake kwa weledi,
 
Hakimu kama yule aliye pandishwa kuwa Jaji na Magu simply kwa kuandika hukumu Kiswahili na sio kwa
weledi wake unadhani ikija kesi ya aliye mteua kutakuwa na haki.
Na kwa nchi sitashangaa kutumia Kiswahili kwani Kiingereza lugha ya sheria ni shida kwake.
Bora huyo aliye pandishwa kwa kuandika lugha yetu ya kiswahili kwenye kutoa haki ya mtanzania mwwnzake kuliko wale wanao jifanya wazungu na kutuzingua na kizungu Chao.

Weledi wa Jaji sio kujua kuandika kizungu bali ni kujua Sheria, ndio maana sisi wananchi wa Tanzania tunazitaka mahakama zetu zitoa haki za wananchi kwa lugha ya kiswahili sio kiingereza.
 
Kwenye bandiko hili pale litakapotumika neno Jaji au Majaji ndiyo itajumuisha pia na mahakimu toka mahakama za mwanzo mpaka Mkoa.

Sisi kama Taifa tumerithi mfumo wa kale na maarufu zaidi wa kuwa na serikali ya kijamhuri (Republic). Ndani ya mfumo huo kunakuwa kuna mgawanyo wa kimadaraka kati ya matawi matatu yanayounda serikali, yaani Bunge, Mahakama na Utawala.

Kwa mfumo huo matawi mawil ya Bunge na Utawala huongozwa na wanasiasa wakati tawi la Mahakama huongozwa na Majaji wanaoteuliwa pia na wanasiasa. Kinadharia matawi haya matatu hutakiwa kuwa huru na kila tawi kuwa na uwezo fulani wa kusimamia msawaziko wa tawi Jingine.

Kwa Tanzania inaonekana kuwa Mahakama yetu inaendeshwa zaidi kwa kufuata matakwa ya tawi la Utawala na hata wanasiasa waliomo kwenye tawi la utawala wakati fulani hugoma kutekeleza maamuzi ya Mahakama na mahakama huwa inakaa kimya.

Wengi wetu tuna uzowefu kwamba jambo la kisiasa likipelekwa kwenye mahakama zetu kama liko kinyume na maslahi makubwa na tawi la Utawala ama chama kilichoko madarakani, basi mahakama hushindwa kufanya maamuzi kwa wakati ama ikifanya maamuzi ni lazima yaegemee upande wa Watawala au chama kilichoko madarakani yaani CCM.

Kuanzia uamuzi wa Mgombea binafsi mpaka Ubunge wa Lissu kule Singida Mashariki na sasa kesi ya Wabunge 19 wa CHADEMA, bado mtu wa kawaida kabisa mtaani anashangaa ni kwa nini jambo la wazi kama la hao wabunge linaweza kuchukua zaidi ya miaka 3 kuamuliwa.

Nimeandika makala haya baada ya kusisimuliwa na Uamuzi wa Mahakama Kuu ya Pakistan kutangaza kwamba kukamatwa kwa kiongozi wa chama cha siasa cha Pakistan Tehreek-e-Insaf (PTI) Imran Khan, kuwa kulikuwa batili.

Yaani Khan kakamatwa Jumanne na leo Mahakama Kuu inatoa uamuzi kwamba kukamatwa kwake ni batili, kwa Tanzania inawezekana kweli? Mahakama zetu linapokuja suala dhidi ya watawala ama CCM huwa haina uwezo wa kufanya maamuzi kwa wakati.
Waliopeleka kesi hiyo ya Pakistan walienda kuomba nini? Maana mawakili wa Tanzania ambao wamesoma pamoja na hao majaji wanafanana kwa kila kitu na hata wewe na mimi hakuna tofauti. Kule Kenya pia wakili alienda kuomba matokeo yafutwe kumbe alitaka matokeo yafutwe na yeye atangazwe kuwa mshindi, mahakama ikampa alichoomba akaishia kulalamika. Niruhusu nikukumbushe pia kuwa Pakistan nayo ilitawaliwa na Uingereza hivyo kila kitu tunafanana
 
.Weledi wa Jaji sio kujua kuandika kizungu bali ni kujua Sheria, ndio maana sisi wananchi wa Tanzania tunazitaka mahakama zetu zitoa haki za wananchi kwa lugha ya kiswahili sio kiingereza.
Kwenye sheria kinachozingatiwa kwenye kutoa haki ni mantiki na athari ya hukumu inapoptolewa.

Sasa Jaji kwa mfano anapoendelea kuitaja kesi kwa zaidi ya miaka mitatu na kuendelea kuipangia siku kwa kuwa upande wa mashitaka umesema "Ushahidi haujakamilika". Jaji wa aina hiyo anatumia mantiki gani kuendelea kusubiria ushahidi ambao kwa zaidi ya miaka 3 haujakamilika??
 
Kwenye sheria kinachozingatiwa kwenye kutoa haki ni mantiki na athari ya hukumu inapoptolewa.

Sasa Jaji kwa mfano anapoendelea kuitaja kesi kwa zaidi ya miaka mitatu na kuendelea kuipangia siku kwa kuwa upande wa mashitaka umesema "Ushahidi haujakamilika". Jaji wa aina hiyo anatumia mantiki gani kuendelea kusubiria ushahidi ambao kwa zaidi ya miaka 3 haujakamilika??
Ndio maana Mhe. Rais Dr.Samia ameunda tume ya Haki jinai ambayo itakusanya maoni na kuboresha na kurwlebisha dosari na kasoro zote zilizopo kwenye mfumo wa haki jinai.

Tusubirie mapendekezo ya Haki jinai.
 
Ndio maana Mhe. Rais Dr.Samia ameunda tume ya Haki jinai ambayo itakusanya maoni na kuboresha na kurwlebisha dosari na kasoro zote zilizopo kwenye mfumo wa haki jinai.

Tusubirie mapendekezo ya Haki jinai.
Tume kadhaa kuhusu marekebisho ya utendaji wa mahakama zimeshatoa maoni yake. RUSHWA na ukosefu wa weledi ndiyo chanzo cha kuwa na mahakama goi goi.

Haiwezekani zaidi ya asilimia 70 ya waliomo kwenye magereza yetu wawe siyo wafungwa bali mahabusu. Yote hiyo ni kwa sababu ya mahakama kutokushughulia kesi kwa weledi.
 
....Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar aliamua kugombea Urais wa Zanzibar kwa kutumia tiketi ya chama cha ccm !,Judge Bomani aligombea Urais wa Tanzania kwa kutumia tiketi ya chama cha ccm!,siku utakayoshuhudia hawa majaji wanaomba hizi nafasi za ujaji, na wanafanyiwa interview ya nafasi hiyo, ndio siku ambayo JUDICIARY nchi hii itakua huru, kwa sasa ni upuuzi mtupu na binafsi always Nina respects kubwa kwa CJ Nyalali (MHSRIP),alifanya kazi kipindi cha Chama kimoja na mahakama zili earn respects
 
siku utakayoshuhudia hawa majaji wanaomba hizi nafasi za ujaji, na wanafanyiwa interview ya nafasi hiyo, ndio siku ambayo JUDICIARY nchi hii itakua huru,
Hivi karibuni Jaji Mmoja mstaafu anasema eti aliwahi kufanya maamuzi lakini maamuzi hayo yalipofika mikononi mwa aliyekuwa Waziri Mkuu kwa wakati huo, aliichana nakala ya Hukumu hiyo.

Swali la kujiuliza, baada ya nakala ya Hukumu hiyo kuchanwa na huyo aliyekuwa Waziri Mkuu, Jaji alifanya nini kuhakikisha hukumu yake inasimama!??
 
Kwa ivo unataka kusema mawakili wetu ndiyo huwa wanaomba vitu visivyoeleweka kwa majaji na kila hukumu hutoa kile kilichoombwa!!??
Hakika na sahihi kabisa. Kwa mfano majuzi Wakili Magoti aliiomba mahakama itoe uhuru wa watu wote wakiwemo wafungwa wapewe haki ya kupigiwa kura; mahakama ikampa. Lakini huwezi kutenganisha haki ya kupigiwa na kupiga kura, hizi zinaenda pamoja kama misuli na damu-sasa sijui alifanya makusudi, hajui, au alipitiwa.
 
Hakika na sahihi kabisa. Kwa mfano majuzi Wakili Magoti aliiomba mahakama itoe uhuru wa watu wote wakiwemo wafungwa wapewe haki ya kupigiwa kura; mahakama ikampa. Lakini huwezi kutenganisha haki ya kupigiwa na kupiga kura, hizi zinaenda pamoja kama misuli na damu-sasa sijui alifanya makusudi, hajui, au alipitiwa.
Inawezekana labda...

Maana Jaji Mkuu Profesa Juma alishawahi kusema mawakili wengi wana upungufu wa weledi.

Inashangaza wakili anapomwambia mteja wake ampe hela akampe Jaji ili ahukumu kwa "Haki".
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom