Slim5
JF-Expert Member
- Jan 7, 2014
- 28,108
- 37,644
View attachment 1313820
Mbabe na mwamba katika medani za kivita katika eneo lote la Mashariki ya kati General Qassem Soleiman ameshamaliza majukumu yake na sasa amepumzika katika ufalme wa Mungu huku harakati zake zikiwa zimeshaonekana Dunia nzima.
Je, huyu mwamba Qassem Soleiman ni nani hadi Dunia itikisike baada ya kifo chake!!?
Hapo mwanzo wale wasiomjua walikuwa wakimbeza sana kuwa si lolote si chochote lakini leo hii wao wenyewe wanakiri kuwa alikuwa ni mwamba kweli, wanakiri kuwa alikuwa ni chuma cha pua. Wanakiri kuwa kwa hakika alikuwa ni KINGPIN.
Yaani athari za kifo chake zimetikisa mpaka mifuko yetu sisi wananchi wa kawaida kwenye mataifa mengine kwa kusababisha ongezeko la bei ya mafuta.
Huyo ndiye General Qassem Soleiman, kiongozi wa IRGC ( The Islamic Revolutionary Guard Corps ) ambalo ni mojawapo katika matawi ya jeshi la Iran linalohusika na ulinzi wa mapinduzi na operation za kijeshi zinazofanyika nje ya Iran ambaye ameuawa jana Januari 02, 2019 karibu na uwanja wa ndege wa kimataifa wa Baghada nchini Iraq alipokuwa akijiandaa kwa ajili ya kuondoka Iraq baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi. Gari alilopanda lilishambuliwa na ndege isiyokuwa na rubani (UAV) ya jeshi la Marekani kwa amri ya rais Donald Trump.
Watu wengi wanachanganya baina ya Jeshi la Iran (Artesh) na jeshi la ulinzi wa mapindunzi (SEPAH au IRGC). Ni kwamba IRGC ni tawi tu lililokuwa likiongozwa na huyu mwamba Qassem Soleiman ambaye ni miongoni mwa maofisa wa ngazi za juu katika jeshi la Iran.
Mkuu wa majeshi ya Iran ni Major General Mohammad Bagheri. Ingawa Major General Qassem Soleiman alikuwa akiripoti moja kwa moja kwa Ayatollah Khamenei lakini mkuu wake wa kazi ni huyo Mohammad Bagheri.
Huyu mwamba katika medani ya vita alizaliwa mwaka 1957 na kujiunga na jeshi la Iran mnamo mwaka 1979. Katika kipindi chote cha utumishi wake jeshini ameshiriki kwenye operation kubwa na ndogo 59 za kijeshi ndani na nje ya Iran.
Miongoni mwa operation kubwa alizoshiriki ni pamoja na vita kati ya Israel na Lebanon ya mwaka 1985-2000 ( South Lebanon conflict (1985–2000) ambapo Israel ilishindwa vita na kuondoa majeshi yake kusini mwa Lebanon, vita kati ya Israel na Lebanon ya mwaka 2006 ( 2006 Israel–Hezbollah War )ambapo kila upande ulijitangazia ushindi, na Vita dhidi ya kundi la kigaidi la Islamic state huko nchini Iraq na Syria. Pia amekuwa akiratibu na kubuni mipango katika vita vya kiwakala (Proxy war) baina ya Iran na Israel kupitia makundi ya Hamas na Hizbullah.
Mafunzo ya kijeshi na mbinu zake za kivita huko Yemen zimefanikiwa kuisambaratisha Saudi Arabia kwenye uwanja wa vita na kuwafanya Wapiganaji wa Hauthi kuendelea kuiongoza Yemen.
Ndiye aliyefanikisha kumbakiza madarakani Rais Bashar al Assad kwa kupeleka maelfu ya Wapiganaji wa kishia kutoka Iran, Iraq na Afghanistan ili kuliongezea nguvu jeshi la Syria lililokuwa tayari limeshapoteza udhibiti wa ardhi ya Syria ambayo iliangukia mikononi mwa makundi ya waasi yaliyokuwa yakiungwa mkono na Marekani, Uingereza, Ufaransa, Uturuki na Saudi Arabia.
Bila huyu Qassem Soleiman leo hii Israel isingekuwa na Iron dome maana mafunzo yake kwa hamas ndio chanzo cha yale maroketi yanayoichapa Israel kila kukicha.
Generali Qassem Soleiman amekufa kishujaa huku akiiacha Iran likiwa ni taifa lenye nguvu kubwa kijeshi kuliko mataifa yote ya Mashariki ya kati. Ikumbukwe kuwa mashariki ya kati kuna nchi inaitwa Israel ambayo inasifiwa kuwa ina nguvu kubwa kijeshi lakini nguvu yao inatokana na kubebwa na mataifa makubwa ya Marekani na Ulaya magharibi ikiwa ni pamoja na kusaidiwa hadi bajeti ya ulinzi ya kila mwaka ya ulinzi. Yaani siku hayo mataifa yanayoibeba hiyo nchi yatakaposema hapana, basi hiyo nchi itakosa mahala wa kushika na kuanguka puuu.
General Soleiman amekufa shujaa baada ya kufanikisha malengo ya Iran. Waliomuua wamechelewa kwani wamemuua baada ya kuwa amekwisha kamilisha malengo ya Iran. Nafasi yake katika jeshi la Ulinzi wa mapinduzi ya kiislam (IRGC) imechukuliwa na msaidizi sake Brigedier General Ismail Ghaan. Rest in peace Mwamba, Mbabe na Chuma general Qassem Suleiman.
View attachment 1313823
NB: Usiibe makala za Infantry Soldier kwenye groups za WhatsApp na Facebook bila idhini yake
HahahaaaaaWabongo wajinga sana, eti kwa sifa zote hizo kwanini amekufa kizembe? Wewe na ujanja wote unashindwa kununua hata mosquito net unaliwa na mbu unakufa, unashindwa kununua hata condom unapata VVU unakufa, jinga sana.
Ametangulizwa mbele ya haki. Sad indeedthe general
Yes brother. No human is immune to a projectileKombora likikukaribia halina ukamanda. R. I. P Kassim
Wewe ndio "she" au general?She is no more.
Huyu mtu hajapambwa hata tone, katika Uzi huu. Mwaandishi ameacha sifa nyingi Sana za huyu mwamba. Kwanza kabisa ni yeye aliyesafiri mpaka Moscow kumwomba Putin atume jeshi la anga nchini Syria. Huyu mtu pia alikuwa moja ya watu wa mwanzo kushirikiana na marekani kutoa taarifa za intelligence kuhusu kambi za Taliban katika Afghanistan..
walimuonea huruma sema alipogusa read line wakala kichwa. Marekan waliona nivyema wale kichwa kulipizia dam ya contractor ambaye inasemekana alikuwa mtu muhim sana ktk jeshi la marekan. Upendo wa marekan kwa huyu contractor ambaye inasemekana alkuwa brain behind USA waliona bora wammalize ajuwe hata yeye walimstai kwa muda wakiheshm sheria zaka mataifa. Niyeye alie toa amri yakumaliza yule contractor na kuvmia ubaloz wa USA.View attachment 1313820
Mbabe na mwamba katika medani za kivita katika eneo lote la Mashariki ya kati General Qassem Soleiman ameshamaliza majukumu yake na sasa amepumzika katika ufalme wa Mungu huku harakati zake zikiwa zimeshaonekana Dunia nzima.
Je, huyu mwamba Qassem Soleiman ni nani hadi Dunia itikisike baada ya kifo chake!!?
Hapo mwanzo wale wasiomjua walikuwa wakimbeza sana kuwa si lolote si chochote lakini leo hii wao wenyewe wanakiri kuwa alikuwa ni mwamba kweli, wanakiri kuwa alikuwa ni chuma cha pua. Wanakiri kuwa kwa hakika alikuwa ni KINGPIN.
Yaani athari za kifo chake zimetikisa mpaka mifuko yetu sisi wananchi wa kawaida kwenye mataifa mengine kwa kusababisha ongezeko la bei ya mafuta.
Huyo ndiye General Qassem Soleiman, kiongozi wa IRGC ( The Islamic Revolutionary Guard Corps ) ambalo ni mojawapo katika matawi ya jeshi la Iran linalohusika na ulinzi wa mapinduzi na operation za kijeshi zinazofanyika nje ya Iran ambaye ameuawa jana Januari 02, 2019 karibu na uwanja wa ndege wa kimataifa wa Baghada nchini Iraq alipokuwa akijiandaa kwa ajili ya kuondoka Iraq baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi. Gari alilopanda lilishambuliwa na ndege isiyokuwa na rubani (UAV) ya jeshi la Marekani kwa amri ya rais Donald Trump.
Watu wengi wanachanganya baina ya Jeshi la Iran (Artesh) na jeshi la ulinzi wa mapindunzi (SEPAH au IRGC). Ni kwamba IRGC ni tawi tu lililokuwa likiongozwa na huyu mwamba Qassem Soleiman ambaye ni miongoni mwa maofisa wa ngazi za juu katika jeshi la Iran.
Mkuu wa majeshi ya Iran ni Major General Mohammad Bagheri. Ingawa Major General Qassem Soleiman alikuwa akiripoti moja kwa moja kwa Ayatollah Khamenei lakini mkuu wake wa kazi ni huyo Mohammad Bagheri.
Huyu mwamba katika medani ya vita alizaliwa mwaka 1957 na kujiunga na jeshi la Iran mnamo mwaka 1979. Katika kipindi chote cha utumishi wake jeshini ameshiriki kwenye operation kubwa na ndogo 59 za kijeshi ndani na nje ya Iran.
Miongoni mwa operation kubwa alizoshiriki ni pamoja na vita kati ya Israel na Lebanon ya mwaka 1985-2000 ( South Lebanon conflict (1985–2000) ambapo Israel ilishindwa vita na kuondoa majeshi yake kusini mwa Lebanon, vita kati ya Israel na Lebanon ya mwaka 2006 ( 2006 Israel–Hezbollah War )ambapo kila upande ulijitangazia ushindi, na Vita dhidi ya kundi la kigaidi la Islamic state huko nchini Iraq na Syria. Pia amekuwa akiratibu na kubuni mipango katika vita vya kiwakala (Proxy war) baina ya Iran na Israel kupitia makundi ya Hamas na Hizbullah.
Mafunzo ya kijeshi na mbinu zake za kivita huko Yemen zimefanikiwa kuisambaratisha Saudi Arabia kwenye uwanja wa vita na kuwafanya Wapiganaji wa Hauthi kuendelea kuiongoza Yemen.
Ndiye aliyefanikisha kumbakiza madarakani Rais Bashar al Assad kwa kupeleka maelfu ya Wapiganaji wa kishia kutoka Iran, Iraq na Afghanistan ili kuliongezea nguvu jeshi la Syria lililokuwa tayari limeshapoteza udhibiti wa ardhi ya Syria ambayo iliangukia mikononi mwa makundi ya waasi yaliyokuwa yakiungwa mkono na Marekani, Uingereza, Ufaransa, Uturuki na Saudi Arabia.
Bila huyu Qassem Soleiman leo hii Israel isingekuwa na Iron dome maana mafunzo yake kwa hamas ndio chanzo cha yale maroketi yanayoichapa Israel kila kukicha.
Generali Qassem Soleiman amekufa kishujaa huku akiiacha Iran likiwa ni taifa lenye nguvu kubwa kijeshi kuliko mataifa yote ya Mashariki ya kati. Ikumbukwe kuwa mashariki ya kati kuna nchi inaitwa Israel ambayo inasifiwa kuwa ina nguvu kubwa kijeshi lakini nguvu yao inatokana na kubebwa na mataifa makubwa ya Marekani na Ulaya magharibi ikiwa ni pamoja na kusaidiwa hadi bajeti ya ulinzi ya kila mwaka ya ulinzi. Yaani siku hayo mataifa yanayoibeba hiyo nchi yatakaposema hapana, basi hiyo nchi itakosa mahala wa kushika na kuanguka puuu.
General Soleiman amekufa shujaa baada ya kufanikisha malengo ya Iran. Waliomuua wamechelewa kwani wamemuua baada ya kuwa amekwisha kamilisha malengo ya Iran. Nafasi yake katika jeshi la Ulinzi wa mapinduzi ya kiislam (IRGC) imechukuliwa na msaidizi sake Brigedier General Ismail Ghaan. Rest in peace Mwamba, Mbabe na Chuma general Qassem Suleiman.
View attachment 1313823
NB: Usiibe makala za Infantry Soldier kwenye groups za WhatsApp na Facebook bila idhini yake
Hizo sifa angekuwa nazo angelivimbia kombora likadunda!
She is no more.