Majina ya vituo vya daladala sehemu mbalimbali

Huwa napata mtihani sana kwani kituo changu cha daladala kinaitwa SAMAKI kiko hapa Mbezi Beach

Mara nyingi tukikaribia kufika utasikia konda anauliza Samaki wapo?

Dah, napata mtihani sana kusema TUPO...... (maana infwakiti mimi sio samaki ni mtu)

Je unajua kituo gani kingine ambacho ni "mtihani"?

Mkuu nimecheka sana
 
Kuna kituo kimoja pale Kigogo kinaitwa First Inn actually ni jina maarufu la Baa, lakini sikia makonda wanavyokiita ........Vestini.............. vestini............. vestini..........afadhali hata wengine wanaosema festini
 
Wengi hawajui kabisa kwamba kituo cha Afrika Sana pale kwenye mambo yetu ukwlei kabisa kinatakiwa kiitwe Afrika Sanaa, uwkeli ni kwamba zamani kulikua na kituo cha Utamaduni cha Sanaa ambacho bado jengo na ofisi ipo kama unaelekea kanisa Katoliki Mwenge lakini kuna mtu aliharibu akaita sana na wengi wameshika hivyo (HATA KUNA rASTA ANA DUKA LAKE ANAITA AFRIKA SANA).....Ukwli ni afrika Sanaa na sio Afrika sana.waambie na wengine ukiona post hii
 
Tandale uzuri barabara inayotoka Sinza hadi Magomeni Moroco kuna kituo kinaitwa Popobawa..., utamsikia konda 'Popobawa mpo??' ukiitikia utaskia 'oya suka muache Popobawa'
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom