Majibu; je, ni sahihi kufanya mapenzi wakati mkeo akiwa na mimba?

CompaQ

JF-Expert Member
Dec 31, 2012
281
133
Ni kawaida kwa mwanaadamu aliye mzima kupenda kuwa na mtoto, na kwa namna ya upekee katika kuumbwa kwa mwanaadamu, hakuna njia nyingine yoyote ile ambako mtoto anaweza kupatikana bila ya maingiliano ya kimwili baina ya watu wa jinsia mbili tofauti (ukiachilia mbali instances chache ambapo mambo ya test tube na artificial insemination hutumika).

Kifupi ni kwamba, kama mwanamke atataka kubeba ujauzito ni lazima akubali kuingiliwa, Vivyo hivyo kama mwanaume anataka kumbebesha mwenza wake ujauzito ni lazima ahakikishe kuwa amemwiligilia mke

Hata hivyo, licha ya ukweli wa kuwa ili ujauzito upatikane ni lazima kuwe na kufanya mapenzi, kumekuwa na mkanganyiko sana juu ya tendo hili la kufanya mapenzi pindi inapotokea mwanamke ameshashika ujauzito.

Je, ni sahihi kufanya mapenzi wakati mwanamke wako ni mjamzito?
Je, ni hadi muda gani kabla ya kujifungua, ambapo mwanamke mjamzito anaweza kuwa anaingiliwa kimwili na mwenza wake?

Kwa maswali haya na mengine kadhaa, hebu twende pamoja mdogo mdogo kama ifuatavyo:-

1. JE, NI SAHIHI KUFANYA MAPENZI IKIWA MWANAMKE WAKO NI MJAMZITO?

Ndio, hakuna tatizo lolote kwa mwanamke kuendelea kufurahia mapenzi na mumewe au mpenzi wake wakati anapokuwa mjamzito.

Wataalamu wanaeleza kuwa, ikiwa ujauzito ulioubeba haukupi shida yoyote ile na unajisikia uko poa, basi hakuna hatari yoyote ile ikiwa utataka kufanya.

Tatizo pekee ambalo huwa linawakumba wengi wa wanawake wakiwa wajawazito ni kuwa, huwa wanapoteza hamu ya tendo lenyewe wanapokuwa katika hali hii, au kushindwa kumudu kutokana na kujisikia uchovu muda mwingi.

Ingawa pia wapo wanawake ambao wakiwa katika hali hii ndio kwanza, wanakuwa wanajisikia kukereketwa huko kwenye ki**i kupita maelezo, na wanatamani muda wote wafanye mapenzi.

Wapo baadhi ya wanawake ambao wanakuwa wako normal kimwili, lakini kisaikolojia wanakuwa na ile hofu ya kuwa kufanya kunaweza kuwaharibia mimba zao, fikra ambazo huwatoa kabisa katika mstari wa kufurahia tendo hili.


Kwa hiyo, ikiwa mwili wako uko poa, na madaktari wamekwambia kiumbe kinakua bila shaka, na unaweza kwenda kazini, huna haja ya kujibania utamu wa mumeo au kumbania mumeo.

(2). JE, KUFANYA WAKATI WA UJAUZITO KUNAWEZA KUSABABISHA UJAUZITO KUHARIBIKA?

Hili pia ni miongoni mwa maswali na hali ambazo zimekuwa zikiwachanganya watu wengi, waume kwa wanawake.
Ila ukweli ni kwamba, kufanya hakuhusiani na kuharibika kwa mimba au kujifungua kabla ya wakati muafaka.

Kwa kawaida, kuharibika kwa mimba hutokana na sababu zingine tofauti kabisa, ikiwa ni pamoja na kizazi cha mwanamke kuwa na matatizo hasa katika kuhimili ukuaji wa kiumbe tumboni na sababu zingine za kimazingira.

Wala sio kwa sababu ya kitu ambacho unakifanya au hukifanyi.


(3). JE, KUFANYA WAKATI WA UJAUZITO KUNAHARIBU AU KUMDHURU MTOTO?

Kiumbe kilicho tumboni wakati wa ujauzito huwa kinakingwa na ute maalum unaojulikana kitaalamu kwa jina la "amniotic fluid" ndani ya mji wa uzazi, pamoja na kuta za mji wenyewe wa uzazi.

Hakuna namna ambavyo muhogo unaweza kupita na kufika mahali mtoto anapokuwa anakua huko ndani, au zile mbegu kuwa zitapita moja kwa moja na kwenda kumdhuru mtoto.

Kumekuwa na ule msemo wa kuwa kufanya wakati wa ujauzito ni kulea mimba, watu wakiamini kuwa mbegu huwa zinakwenda moja kwa moja kwenye kiumbe.

Dhana hii ni potofu. Kama kilivyo chakula cha kawaida mtu anapokula, ndivyo ambavyo mbegu nazo huwa hivyo.

Kila kitu kwanza lazima kiingie katika mfumo wa kawaida wa usafirishaji wa virutubisho vilivyo sahihi kuelekea kwenye kiumbe husika.

Hii ikimaanisha kuwa mbegu nazo huingia katika mfumo huo huo, huchujwa na kile kinachoonekana kuwa ni kirutubisho kitasafirishwa kwenda kulea kiumbe, ilhali yale makapi lazima yatatoka.

Tofauti pekee hapa ni kuwa, "mbegu za kiume zina protini nyingi", hii ikimaanisha kuwa sehemu kubwa ya kile kinachomwagwa kwenye uke wa mjamzito, kina nafasi ya kutumika kwa ajili ya kuongeza rutuba kwa kiumbe kinachokuaa ndani ya tumbo.

Na nyingine zinaweza kutoka tu zenyewe bila matatizo yo yote.


(4). NI MIKAO IPI (STAILI) AMBAYO NI MIZURI ZAIDI KUITUMIA KUFANYA WAKATI WA UJAUZITO?

Hakuna mkao maalum. Ujauzito sio ulemavu kwamba mnalazimika kujipanga upya namna ya kuridhishana, wala sio ugonjwa pia.

Ikiwa mwanamke unajihisi uko fresh kuendelea kutumia staili ya mwanzo ambayo mlikuwa mnaitumia na unafikishwa na mwenzio, huku huyo mwenzio naye akiwa yuko ok kuitumia staili hiyo na anaimudu hata unapokuwa na tumbo lako, hakuna shida

Jichumishe mboga, jifanye mbuzi ulogoma kwenda, jifanye namna yoyote ile unayoona uko poa, na mambo yatakuwa vizuri.

(5). VIPI KUHUSU KITU ULE MTANDAO WETU NA OR*L S*X? (CHUMVI)

Or*l s*x ni salama kabisa wakati wa ujauzito. Hata hivyo, ni muhimu kuepuka hewa kuingia ndani ya uke wako wakati ukiwa katika hali hii.
Wapo wale watu watundu ambao hugeuza uke kama pulizo na kujitia umahiri wa kutaka kulijaza hewa wakati wa kupeana raha.

Katika mazingira ya kawaida, ikiwa mnafurahia hili, hakuna tatizo, ila wakati wa ujauzito, hii ni hatari kwani inaweza kuleta madhara katika mishipa fulani ndani ya uke, ambayo iko na uhusiano na mishipa ya kuelekea kwenye mji wa uzazi.

Kuhusu ule mtandao wa vijana (Tigo), ambao kwa kawaida hauruhusiwi kutumika, hakuna wakati unaokuwa mbaya zaidi kuutumia kama wakati huu wa ujauzito.
Katika wakati huu, uke wa mwanamke mara nyingi unakuwa sensitive zaidi ya wakati akiwa hana ujauzito, na kuendekeza kuf**ana, kunaongeza hatari ya bakteria kuhamia kwenye uke na kusababisha magonjwa ambayo yatadhuru kiumbe kilichobebwa ndani.

(6). KUNA UMUHIMU WA KUTUMIA KONDOMU?
Kama nilivyodokeza hapo awali, wakati wa ujauzito uchi wa mwanamke unakuwa sensitive zaidi kwa magonjwa.
Unaweza tu kuguswa na mwenzako ambaye hakuwa amenawa mikono uzuri na ikakusababishia tatizo fulani, hivyo basi, inashauriwa kutumia kondomu ikiwa:

mwenza wako aliwahi au ana maradhi ya maambukizi
uko kwenye mahusiano na zaidi ya mtu mmoja
umeamua kungonoka na king'asti kipya wakati wa ujauzito


(7). JE, KUKOJOA AU KU-SQUI*T MARA KWA MARA KUNAWEZA HARIBU MIMBA?
Hapana. Licha ya ukweli kuwa wakati wa ujauzito uke huzalisha kemikali ambazo ni mahususi kwa ajili ya kumkinga mjamzito na uvamizi wa bakteria wowote wanaoweza kuwa tishio kwa ujauzito wake, na kwamba kemikali hizi wakati mwingine huweza kuhitilafiana na lile bao analopiga mwanamke na hivyo kumletea hali fulani ya kukwaza, kwa ujumla wake hakuna baya linaloweza kusababishwa na kukojoa au kufika kileleni .

Na wala kufanyana hakuwezi kuathiri kwa namna yoyote ile muda wako wa kujifungua (kuuchelewesha au kuuwahisha)


(8). JE, NI WAKATI GANI MWANAMKE MJAMZITO ANATAKIWA KUACHA KUFANYA MAPENZI?
Ijapokuwa wapo wanawake wengi ambao wanaweza kabisa kuendelea kufurahia kufanywa hadi siku wanakwenda kujifungua , kuna baadhi ya nyakati mshauri wako wa afya anaweza kukushauri kuacha ngono kutokana na moja au yote kati ya yafuatayo:

umekuwa na tatizo la kujifungua kabla ya muda muafaka kabla ya ujauzito ulio nao
umetokewa na tatizo la kutokwa na damu kwenye uke
umekuwa ukitokwa na ute fulani ambao wataalamu wanauita kwa jina la "amniotic fluid"
umekuwa na tatizo la kwenye mlango wa uzazi, ambalo kitaalamu linajulikana kama cervical incompetence
kondo la nyuma limesambaa na kuziba kabisa mlango wa uzazi na kuanza kujitokeza kwa nje (placenta previa)

(9). JE, KUNA TATIZO LOLOTE IKIWA HUHITAJI KUFANYA?
Hapana, na hii ni hali ya kawaida sana kwa baadhi ya wanawake wanapokuwa wajawazito, ama kutokana na hofu inayokuwa vichwani mwao kuwa atapata madhara kwa kufanya hivyo, au kutokana tu na aina ya homoni zinazozalishwa mwilini wakati huo.

Kuna mengi mnaweza kufanya bila kuhusisha maingiliano ya kimwili na ambayo yanaweza kumfanya mwanamke kuridhika anapokuwa katika hali hiyo.

10. NI BAADA YA MUDA GANI TOKA KUJIFUNGUA MWANAMKE ANAWEZA KUENDELEA KUFANYA MAPENZI?
Iwe kwa njia ya upasuaji au kwa njia ya kawaida, inaeleweka wazi kuwa baada ya kujifungua, mwanamke anakuwa na hali fulani ya mwili kuchoka, hali ambayo ni ya kawaida.

Ingawa wapo ambao wanaweza kujihisi wanamudu kushiriki tendo la ndoa kabla, lakini wataalamu wanashauri kuwa wakati mzuri wa kurejea kufanyana na mwenzio baada ya kujifungua, inakuwa ni baada ya kupita wiki sita.

CHANZO; JE, NI SAHIHI KUFANYA MAPENZI WAKATI MKEO AKIWA NA MIMBA? « ManyandaHealthy&[HASHTAG]#8482[/HASHTAG];
 
Back
Top Bottom