Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,634
- 697,904
Usiku wa deni ni mfupi sana! Kesho ndio kesho ndio kesho siku tuliyoahidiwa umeme wa uhakika na mheshimiwa rais wa jamhuri ya muungano! SIMLAUMU kwa asilimia kadhaa maana naye alihakikishiwa na wateule wake! Akaridhika na hakikisho akasahau kukumbushana! Mambo ni mengi ni vigumu kukumbuka yote
Tanesco ni fupa gumu lililomshinda hata fisi. Kuna fupa lingine la SGR..! halitafuniki, halimezeki, halitemeki kufa halifi, kuishi haliishi.. Lipo tu hapo lilipo kama zezeta..! Mama hajui alifanyeje..!
Nusu ya pili ya mwaka jana 2023 kulitokea tatizo kubwa la maji jijini Dsm! Kelele zikawa nyingi mno.. Mama kuhoji wakamyingiza kingi cha maana! Haraka haraka likatengenezwa tukio la kuzindua kisima kikubwa cha maji kilichopo Kibada Kigamboni.. Na ahadi ya kwamba maji yake yatafika jijini ndani ya wiki mbili na tatizo la maji kuwa historia..!
Wananchi wakaamini kwa asilimia 100 na kwa shangwe kubwa.. Lakini huo ulikuwa uongo mkubwa maana mpaka January hii 2024 yale maji yalikuwa hayajavuka hata bahari!
Marehemu Edward Lowassa kwenye sekeseke la umeme wa Richmond aliwahi kusema.... tukileta siasa kwenye umeme, tatizo la umeme halitaa liishe
Edward Lowassa aliponzwa na kupush mambo yaende haraka! Serikali ya CCM haijazoea kupush mambo mpaka kuwe na maslahi binafsi hasa ya rushwa na 10%
Hakuna watendaji wabovu, wavivu, wasiofuatilia na goigoi kama watendaji wa serikali ya CCM... Sehemu pekee ambayo wako makini nayo sana ni sehemu ya shekeli hasa kama kuna maslahi binafsi
Tofauti na hapo ni business as usual
Kufuatwa na gari nyumbani
Kupelekwa kazini
Kujifungia ofisini
Kusoma magazeti
Kupata chai
Kupitia ripoti juujuu na kuzisaini
Kupokea wageni
Kupata lunch
Kuchat
Kumaliza siku
Kuondoka ofisini
Ufuatiliaji zero.. Wanategemea ripoti za wasaidizi
Wasaidizi nao wanategemea ripoti za mainjinia
Mainjinia nao wanategemea ripoti za wakandarasi
Mkandarasi yeye naye hutoa ripoti kulingana na joto lililopo.. Kwa sehemu kubwa HUDANGANYA!
WAtendaji na wataalam waendao site kwa sehemu kubwa hudanganywa na wakandarasi na hawafuatilii sana kwakuwa nguvu ya kufuatilia humalizwa na bahasha walizoandaliwa!
Tushishangae sana ya umeme kuna ya SGR na kuna ya maji ya Kigamboni na mengine mengi!
Mvua zilizinyesha mfululizo December na January
Zimeokoa mengi
Zimeficha mengi
Zimesingiziwa mengi
Je mama anakumbuka maji ya Kigamboni hayajafika huku mjini!?
Watendaji wa serikali ya CCM ni tatizo donda ndugu! Halina tiba..!
Sent using Jamii Forums mobile app
Tanesco ni fupa gumu lililomshinda hata fisi. Kuna fupa lingine la SGR..! halitafuniki, halimezeki, halitemeki kufa halifi, kuishi haliishi.. Lipo tu hapo lilipo kama zezeta..! Mama hajui alifanyeje..!
Nusu ya pili ya mwaka jana 2023 kulitokea tatizo kubwa la maji jijini Dsm! Kelele zikawa nyingi mno.. Mama kuhoji wakamyingiza kingi cha maana! Haraka haraka likatengenezwa tukio la kuzindua kisima kikubwa cha maji kilichopo Kibada Kigamboni.. Na ahadi ya kwamba maji yake yatafika jijini ndani ya wiki mbili na tatizo la maji kuwa historia..!
Wananchi wakaamini kwa asilimia 100 na kwa shangwe kubwa.. Lakini huo ulikuwa uongo mkubwa maana mpaka January hii 2024 yale maji yalikuwa hayajavuka hata bahari!
Marehemu Edward Lowassa kwenye sekeseke la umeme wa Richmond aliwahi kusema.... tukileta siasa kwenye umeme, tatizo la umeme halitaa liishe
Edward Lowassa aliponzwa na kupush mambo yaende haraka! Serikali ya CCM haijazoea kupush mambo mpaka kuwe na maslahi binafsi hasa ya rushwa na 10%
Hakuna watendaji wabovu, wavivu, wasiofuatilia na goigoi kama watendaji wa serikali ya CCM... Sehemu pekee ambayo wako makini nayo sana ni sehemu ya shekeli hasa kama kuna maslahi binafsi
Tofauti na hapo ni business as usual
Kufuatwa na gari nyumbani
Kupelekwa kazini
Kujifungia ofisini
Kusoma magazeti
Kupata chai
Kupitia ripoti juujuu na kuzisaini
Kupokea wageni
Kupata lunch
Kuchat
Kumaliza siku
Kuondoka ofisini
Ufuatiliaji zero.. Wanategemea ripoti za wasaidizi
Wasaidizi nao wanategemea ripoti za mainjinia
Mainjinia nao wanategemea ripoti za wakandarasi
Mkandarasi yeye naye hutoa ripoti kulingana na joto lililopo.. Kwa sehemu kubwa HUDANGANYA!
WAtendaji na wataalam waendao site kwa sehemu kubwa hudanganywa na wakandarasi na hawafuatilii sana kwakuwa nguvu ya kufuatilia humalizwa na bahasha walizoandaliwa!
Tushishangae sana ya umeme kuna ya SGR na kuna ya maji ya Kigamboni na mengine mengi!
Mvua zilizinyesha mfululizo December na January
Zimeokoa mengi
Zimeficha mengi
Zimesingiziwa mengi
Je mama anakumbuka maji ya Kigamboni hayajafika huku mjini!?
Watendaji wa serikali ya CCM ni tatizo donda ndugu! Halina tiba..!
Sent using Jamii Forums mobile app