Majeraha ya Siasa yanawasumbua watu CCM Mkoa wa Songwe.

Ushindi Daima

Member
May 4, 2013
92
27
Mapema leo humu ndani nimeona thread inayosema kuwa (Mkakati wa Zambi na Mulugo kupinga mabadiliko ya Katiba ya CCM [mtu mmoja,cheo kimoja] wafichuka
Wadau, amani iwe kwenu.)

Ndani ya huo uzi kuna watu wametajwa kwa majina na nafasi zao pamoja na nia ya mwandishi aliyowabebesha hao viongozi bila ya wao kusema.
Mfano mzuri tu kuwa Mheshimiwa Zambi kupitia kwa Wajumbe wa Mkutano Mkuu Taifa Julai 2016 muda wa saa 2 usiku VETA HOTEL katika chakula cha pamoja na wajumbe wa Mkutano huo toka Mbeya na Songwe aliwaaga na kuwathibitishia kuwa hatogombea tena nafasi ya Uenyekiti wa CCM Mkoa iwe Mbeya au Songwe.
Pia wakati wa ziara zake za kukutana na Halmashauri Kuu za CCM kwenye wilaya zote aliwaambia wajumbe kuwa hatogombea tena na atampisha mwana CCM mwingine kwani anataka kutumia muda mwingi wa kumsaidia Mheshimiwa Rais Magufuli kama Mkuu wa Mkoa wa Lindi.
Lakini pia alisema kwa sasa hawazi na kufikiri kugombea ubunge Jimbo la Mbozi 2020.
HIVYO MHESHIMIWA GODFREY ZAMBI HAGOMBEI TENA UENYEKITI WA CCM MKOA MBEYA AU SONGWE.

Kuhusiana na Mheshimiwa Philipo Mulugo ambaye ni Mbunge wa Songwe naye hakuna sehemu ambayo amewahi kutangaza kugombea nafasi ya uongozi katika Mkoa Mpya wa Songwe hasa katika nafasi hiyo ya mtoa uzi aliyoandika ya Uenyekiti wa Mkoa.
Mulugo ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM(Mnec) na alikuwepo kwenye kikao kilichopita cha NEC kule Ikulu na walikubaliana kwa pamoja kukubali mapendekezo hayo.
Leo hii hawezi kuwa sehemu ya usaliti maana anakifahamu chama na kujua utaratibu wake.
Yeye kwa sasa yupo busy na wapiga kura wake ambao ndio waajiri wake.
NA HANA MPANGO WA KUGOMBEA UENYEKITI WA CCM MKOA WA SONGWE.

Ndugu wana JF kwenye andiko la huyo ndugu ambaye ni majeruhi wa Siasa za uchaguzi 2015, amemzungumzia pia Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ileje ndugu Kibona, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mbozi ndugu Aloyce Mdalavuma na Katibu wa CCM Wilaya ya Mbozi ndugu Doris Kimambo kuwa nao ni sehemu ya mkakati huo kwa kutumia group la Whatsapp.
Mfano mdogo ni huyo Mwenyekiti wa CCM Ileje yeye hanaga makuu zaidi ya ujenzi na uimarishaji wa Chama wilayani kwake na hata masuala ya Whatsapp sio muumini sana wa magroup na kuchagia.
Kuhusiana na Mdalavuma na Doris Kimambo hawa wamekuwa sehemu ya hasira za majeruhi wa siasa za 2015 huko Mbozi na amewaandika kwa hila zake zilizo na chuki binafsi.

Miaka yote Mkutano Mkuu wa CCM unaenda kupokea na kubariki mapendekezo ya vikao vya NEC ambavyo navyo vinatangukiwa na CCM.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu eana kazi moja tu ya kupitisha.
Alafu majeruhi huyo anakwambia Wajumbe wa Mbozi ambao ni 10 pekee wasafiri kwa gari ya Chama Wilaya ambayo ameitaja kwa aina na namba ya usajili, kitu cha kuchekesha ni kuwa watu 10 wa Mbozi wawe sehemu ya kuhamasisha Wilaya nyingine Tanzania sembuse Mbeya na Songwe tu?
HAPA INAHITAJI AKILI NYEPESI KUELEWA KAMA HUU NI UZUSHI.

Mwisho, ndugu wana JF tambueni kuwa CCM Mpya yenye kuanikisha TANZANIA Mpya inakuja kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu CCM Taifa kupitisha mapendekezo ya Katiba ya CCM Toleo la 2012, Kanuni za Uchaguzi pamoja na Kanuni za Jumuiya zake ambazo tayari mabaraza ya kupitisha yamekaa huko Dodoma.

Nawaonya tu majeruhi hao wa Siasa za Mkoa wa Songwe kwenye uchaguzi wa 2015 kule Mbozi na Songwe kwa majina yao George Mwenisongole na Noel Nkana acheni upuuzi na uzushi wa kuandika uongo huu kwenye mitandao ya kijamii.
TUMESHAWAFAHAMU!
 
Back
Top Bottom