Watanzania acheni wivu wa kike na mjadili hoja baada ya kupata upande wa pili.
MUHONGO alikata ndege baada ya kuambiwa inapita DUBAI na wanalala DUBAI.
KWA HALI YA DUNIA HII KWENDA ALGERIA MPKA ULALE NJIANI???
WATU TUNAENDA CHINA MAREKANI HATULALI NJIANI IJE KUA ALGERIA?\
MUHONGO ALISEMA HAWEZI LALA DUBAI KWA SAFARI YA ALGERA
AKABADILI NDEGE AKAPANDA KLM AKAFIKA ALGERIA SIKU HIYO HIYO NA ALIPANDA Economy Class
KWA WALE WALIOWAHI KUPITIA DUBAI WANAWEZA KUSEMA. HASA KIPINDI HUKI CHA SIKUU DUBAI NI SHIDA SANA SEHEMU YA KULALA NI SHIDA. SASA MLITAKA MUHONGO AWAFRAHISHE AKALALE DUBAI? ACHENI UJINGA
Kama kinachosemwa kina ukweli basi Huyu ni Limbukeni na hana huruma na fedha ya umma na si huyu tu hata wabunge na viongozi wote nchi hii .natamani Muumba siku moja anijalie uongozi wa juu nchi hii watu kama hawa watanyooka na ubunge utakuwa ni kazi ya kujitolea na uwakilishi wa kweli na si kitega uchumi kama hivi leo inanyosadikika.Daktari Bingwa wa Binaadamu aliye na PHD ambaye amejituma kwa kukaa Darasani miaka kumi na saba ndani ya fani anaambiwa tunakuajiri kwa mshahara wa milioni moja na laki nne(1,400,000)kabla ya tax na makato mengine take home laki saba na kitu na kufanyakazi ktk mazingira magumu lakini wajinga kama hawa wanafuja pato la Taifa kila leo na bado kuwaona waliowapa dhamana ni wajinga kwasababu tu hawana uwezo wa kuwaadhibu kwa yale wanayowatendea.Ben Saa 8. Huko Chadema, mimi CCM damu....Nakwambia, kama kuna mabadiliko kwenye baraza la mawaziri na huyu mtu akabaki kwenye hilo baraza, natupa kadi navaa gwanda. I swear to God !
Utaifa kwanza !
Huyu mtu kazidi matusi kwa watanzania. Kwani kabla ya uwaziri alikuwa anapanda nini, wakati akeidna Musoma alikuwa anapanda basi la kawaida?
Why fly business?
|
WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, amegoma kusafiri na Watanzania wenzake kwenda nchini Algeria kwa daraja la kawaida baada ya kukosa daraja la kwanza, hivyo kuahirisha safari yake kwa siku moja, Tanzania Daima limebaini.
Profesa Muhongo ambaye amekuwa akionyesha dharau kwa Watanzania mara kadhaa, aligoma kusafiri katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam Jumapili ya Novemba 24, 2013, saa 10.45 akiwa na wenzake tisa kwenda kwenye safari ya kikazi nchini Algeria alikoenda baadaye.Moja ya kauli ya dharau iliyotolewa hivi karibuni na Waziri Muhongo ni pale aliposema wafanyabiashara Watanzania wana uwezo wa kuwekeza kwenye soda na juisi badala ya gesi na pia aliwahi kuwashambulia viongozi wa dini kwa kuwaita waongo.
Uchunguzi wa Tanzania Daima uliofanyika kwa siku kadhaa sasa, umethibitisha kwamba Muhongo alikuwa aondoke na ndege ya shirika la ndege la Emirates namba EK 726 kutoka Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere kupitia Dubai kwenda Algeria akiwa na tiketi ya daraja la kawaida bila kujua kabla ya kufika uwanjani hapo na kisha kuanza kumfokea kila aliyekuwa anamsemesha.
Tiketi yake na wenzake kumi ilikuwa ni Economy Class (Daraja la Kawaida), lakini akakataa akitaka asafiri kwa First Class (Daraja la Kwanza). Alibembelezwa na wenzake na wafanyakazi wa Emirates na wale wa Uwanja wa Ndege lakini akagoma huku akifoka na wenzake wakataka kuahirisha safari.
Ikawa tena ni sisi kuwaomba wasafiri ili Bwana Mkubwa (Muhongo) atafutiwe nafasi kwa daraja analotaka.
Walimbembeleza wakamwambia kwa kutumia millage ya safari zake watambadilishia akiwa ndani ya ndege na kumuweka daraja la kwanza lakini alionekana ameshakuwa mkali na hakuwa anamsikiliza yeyote.Baadaye tulifanikiwa kuwashawishi wenzake kuendelea na safari na yeye sijui aliondoka na ndege gani tena maana wakubwa wetu wana mambo sana, anasema ofisa mmoja uwanjani hapo.
Taarifa za awali kuhusu sakata hili, ziliripotiwa siku hiyo katika mtandao wa jamiiforums.com zikieleza kwamba kitendo cha Waziri Muhongo cha kususia safari hiyo, kiliwakera baadhi ya wasafiri wakiwamo raia wa kigeni ambao walishangazwa na hatua hiyo ya kiongozi wa nchi maskini inayotegemea misaada kulazimisha kusafiri kwa daraja la kwanza, daraja ambalo viongozi wa mataifa makubwa hawaruhusiwi kusafiri bila sababu maalumu.
Taarifa hiyo kwenye mtandao wa JamiiForums. Com iliripotiwa hivi: Kweli viongozi wa nchi hii wanatia aibu, wakati mawaziri wa Uingereza wanakataa First Class, hapa kwetu kimetokea kioja. Waziri wenu wa Nishati na Madini (Muhongo) ambaye anazidi kutulaza na joto na giza leo amewaacha hoi Watanzania pale alipofika mpaka Airport na akiwa anaboard akakuta anawekwa sehemu ya abiria wa daraja la kati, baada ya kuambiwa hayuko First Class akagoma na kutoka nje ya mlango. Wakati hayo yakiendelea kumbe ana wenzake zaidi ya tisa wako economy na wawili Bussiness Class, ghafla nao wakaanza kushuka.
Hapo ndipo hekima za mmoja wa wahusika wa Airline (Emirates) akawaomba hao waende ili yeye akabadilishe aje kesho yake. Jamani kweli First Class inakushushia aibu hivi Profesa na bado unasema maisha magumu Tanzania!? Inaonekana zile buti za bora ulizivalia ukiwa form V na haya ndio madhara yake, mnapewa vyeo wakati maisha yalishawapiga; mnatafuta muafaka na Yesu mkiwa madarakani, anaeleza mtu aliyewasilisha mada husika akijulikana kwa jina la Basiasi.
Basiasi alihoji sababu ya abiria wenzake ambao nao walikuwa wakisafiri kikazi kutaka kushuka na kusababisha hasara kwa serikali au wafadhili waliokata tiketi hizo. Kwa utaratibu wa kawaida abiria anayeahirisha safari baada ya kuwa ameshaingia ndani ya eneo la kusafiria (boarding) anaweza kupoteza kabisa tiketi au kulipishwa fedha nyingi zinazoweza kuwa sawa na kununua tiketi mpya.
Hebu kuweni wastaarabu, sasa wale watu tisa walitaka kuwashusha kwa nini na kama wamekwenda, mlishindwa kuwaambia wabaki mpaka mkaanza kuleta aibu uwanjani? Inaonekena ndege mmeanza kupanda uzeeni; najiuliza kivipi unaletewa tiketi hata kama na travel agency halafu unashindwa kuuliza au kukagua mpaka unaenda uwanjani na unapewa boarding pass bado unashindwa kukagua ipi bussiness class na ipi first class! anahoji Basiasi. Abiria mmoja aliyenukuliwa na Jamiiforums alisema kwa waziri wa nchi kama Uingereza anatakiwa kutoa maelezo ya sababu za kusafiri na daraja la kwanza (first class) ikiwa atalazimika kufanya hivyo, vingine viongozi husafiri kwa madaraja ya kawaida.
Wakati Waziri Muhongo akisusia ndege kwa kukosa nafasi ya kusafiri na daraja la kwanza, baadhi ya mawaziri wanaofanya ziara mikoani na kusafiri kwa ndege, hulazimika kuyaagiza mashangingi yao kutoka Dar es Salaam hadi katika mikoa wanayokwenda kufanya ziara hizo hata kama yatatumika kwa siku moja.
Ben Saa 8. Huko Chadema, mimi CCM damu....Nakwambia, kama kuna mabadiliko kwenye baraza la mawaziri na huyu mtu akabaki kwenye hilo baraza, natupa kadi navaa gwanda. i swear to God !
Umbea huu, watz fanyeni kazi
Mmm hii kali anyway mimi namsifu Wasira kwani siku ya Jpili natoka Mwanza baba wa watu alikaa kwenye zile siti za mbele pembeni wala hakutaka kumsumbua mtu pamoja na uwaziri wake .Big up Wasira mfundishe mwenzio ajishushe kidogo tu asinge kufa au kukonda wote tu binadam
View attachment 125210
waziri wa nishati na madini, profesa sospeter muhongo, amegoma kusafiri na watanzania wenzake kwenda nchini algeria kwa daraja la kawaida baada ya kukosa daraja la kwanza, hivyo kuahirisha safari yake kwa siku moja, tanzania daima limebaini.
profesa muhongo ambaye amekuwa akionyesha dharau kwa watanzania mara kadhaa, aligoma kusafiri katika uwanja wa ndege wa julius nyerere, dar es salaam jumapili ya novemba 24, 2013, saa 10.45 akiwa na wenzake tisa kwenda kwenye safari ya kikazi nchini algeria alikoenda baadaye.
moja ya kauli ya dharau iliyotolewa hivi karibuni na waziri muhongo ni pale aliposema wafanyabiashara watanzania wana uwezo wa kuwekeza kwenye soda na juisi badala ya gesi na pia aliwahi kuwashambulia viongozi wa dini kwa kuwaita waongo.
uchunguzi wa tanzania daima uliofanyika kwa siku kadhaa sasa, umethibitisha kwamba muhongo alikuwa aondoke na ndege ya shirika la ndege la emirates namba ek 726 kutoka uwanja wa ndege wa mwalimu nyerere kupitia dubai kwenda algeria akiwa na tiketi ya daraja la kawaida bila kujua kabla ya kufika uwanjani hapo na kisha kuanza kumfokea kila aliyekuwa anamsemesha.
tiketi yake na wenzake kumi ilikuwa ni economy class (daraja la kawaida), lakini akakataa akitaka asafiri kwa first class (daraja la kwanza). Alibembelezwa na wenzake na wafanyakazi wa emirates na wale wa uwanja wa ndege lakini akagoma huku akifoka na wenzake wakataka kuahirisha safari.
ikawa tena ni sisi kuwaomba wasafiri ili bwana mkubwa (muhongo) atafutiwe nafasi kwa daraja analotaka.
walimbembeleza wakamwambia kwa kutumia millage ya safari zake watambadilishia akiwa ndani ya ndege na kumuweka daraja la kwanza lakini alionekana ameshakuwa mkali na hakuwa anamsikiliza yeyote.
baadaye tulifanikiwa kuwashawishi wenzake kuendelea na safari na yeye sijui aliondoka na ndege gani tena maana wakubwa wetu wana mambo sana, anasema ofisa mmoja uwanjani hapo.
taarifa za awali kuhusu sakata hili, ziliripotiwa siku hiyo katika mtandao wa jamiiforums.com zikieleza kwamba kitendo cha waziri muhongo cha kususia safari hiyo, kiliwakera baadhi ya wasafiri wakiwamo raia wa kigeni ambao walishangazwa na hatua hiyo ya kiongozi wa nchi maskini inayotegemea misaada kulazimisha kusafiri kwa daraja la kwanza, daraja ambalo viongozi wa mataifa makubwa hawaruhusiwi kusafiri bila sababu maalumu.
taarifa hiyo kwenye mtandao wa jamiiforums. Com iliripotiwa hivi: kweli viongozi wa nchi hii wanatia aibu, wakati mawaziri wa uingereza wanakataa first class, hapa kwetu kimetokea kioja. Waziri wenu wa nishati na madini (muhongo) ambaye anazidi kutulaza na joto na giza leo amewaacha hoi watanzania pale alipofika mpaka airport na akiwa anaboard akakuta anawekwa sehemu ya abiria wa daraja la kati, baada ya kuambiwa hayuko first class akagoma na kutoka nje ya mlango. Wakati hayo yakiendelea kumbe ana wenzake zaidi ya tisa wako economy na wawili bussiness class, ghafla nao wakaanza kushuka.
hapo ndipo hekima za mmoja wa wahusika wa airline (emirates) akawaomba hao waende ili yeye akabadilishe aje kesho yake.
jamani kweli first class inakushushia aibu hivi profesa na bado unasema maisha magumu tanzania!? Inaonekana zile buti za bora ulizivalia ukiwa form v na haya ndio madhara yake, mnapewa vyeo wakati maisha yalishawapiga; mnatafuta muafaka na yesu mkiwa madarakani, anaeleza mtu aliyewasilisha mada husika akijulikana kwa jina la basiasi.
basiasi alihoji sababu ya abiria wenzake ambao nao walikuwa wakisafiri kikazi kutaka kushuka na kusababisha hasara kwa serikali au wafadhili waliokata tiketi hizo.
kwa utaratibu wa kawaida abiria anayeahirisha safari baada ya kuwa ameshaingia ndani ya eneo la kusafiria (boarding) anaweza kupoteza kabisa tiketi au kulipishwa fedha nyingi zinazoweza kuwa sawa na kununua tiketi mpya.
hebu kuweni wastaarabu, sasa wale watu tisa walitaka kuwashusha kwa nini na kama wamekwenda, mlishindwa kuwaambia wabaki mpaka mkaanza kuleta aibu uwanjani? Inaonekena ndege mmeanza kupanda uzeeni; najiuliza kivipi unaletewa tiketi hata kama na travel agency halafu unashindwa kuuliza au kukagua mpaka unaenda uwanjani na unapewa boarding pass bado unashindwa kukagua ipi bussiness class na ipi first class! anahoji basiasi.
abiria mmoja aliyenukuliwa na jamiiforums alisema kwa waziri wa nchi kama uingereza anatakiwa kutoa maelezo ya sababu za kusafiri na daraja la kwanza (first class) ikiwa atalazimika kufanya hivyo, vingine viongozi husafiri kwa madaraja ya kawaida.
wakati waziri muhongo akisusia ndege kwa kukosa nafasi ya kusafiri na daraja la kwanza, baadhi ya mawaziri wanaofanya ziara mikoani na kusafiri kwa ndege, hulazimika kuyaagiza mashangingi yao kutoka dar es salaam hadi katika mikoa wanayokwenda kufanya ziara hizo hata kama yatatumika kwa siku moja.
Ebu acha ushamba wewe, una ushahidi wa kilichowekwa hapa jukwaani?? Na kama ni kweli jee umejua sababu ya mhongo kukataa kupanda bisnes clas? Na una uhakika kakataa kupanda au kaahirisha ziara?
Mimi naona ni umbea tuu huu. Nina mengi ya kujadili.
Kama hii ni kweli na ndivyo alivyo fanya na msifu kwa uamuzi wake huu. Nasema hivi kwasababu jamaa ni waziri yuko jikoni anajua siri za nchi hii kuwa ni tajiri ya kupindukia. Na pengine yeye kama kiongozi anajua alivyo na wenzake walivyo matajiri. Sasa hana sababu yeyote ya msingi kupanda kajamba nani ya ndege.
Kwa jeuri na dharau ya huyu prof lazima kichwani alikuwa anafikiri hivi, mie nimesoma kuliko rais, halafu yeye apande first class mimi msomi wanipandishe kajamba nani, kama ni huo uwaziri wao wauchukue bwana, si safiri labda wabadilishe hii tiketi.
Lakini mkuu, wakati wanakata ticket zao si walijua hilo?? Na pia hii si inaonyeshwa kwenye ticket?? Au kulikuwa na mabadiliko, fafanua manake unaonyesha unaijua hii issue vizuri!!!
Mkuu kila mtu mwenye akili timamu anajua Prof. hawezi kufanya mambo ya kijinga, kwa bahati mbaya kuna Watanzania wenzetu wamejipanga kumzulia Mh.Muhongo kashifa za kila sampuri, kila anacho sema kinakuwa grossly misinterpreted kimakusudi, kila alifanyalo mahasimu wake wanaliona lina WALAKINI!! Mimi namshauri Prof. Muhogo achape kazi na kuinua Uchumi wa Taifa letu, uwezo huo anao sana aogopi kusema ukweli na nana interest za Taifa letu ndani ya moyo wake - asiwasikilize watu waigizaji wanao jifanya wana majibu ya kila tatizo linalo kabiri Taifa letu specifically nyanja za "GESI NA MAFUTA".Watanzania acheni wivu wa kike na mjadili hoja baada ya kupata upande wa pili. MUHONGO alikata ndege baada ya kuambiwa inapita DUBAI na wanalala DUBAI. KWA HALI YA DUNIA HII KWENDA ALGERIA MPKA ULALE NJIANI??? WATU TUNAENDA CHINA MAREKANI HATULALI NJIANI IJE KUA ALGERIA?\ MUHONGO ALISEMA HAWEZI LALA DUBAI KWA SAFARI YA ALGERA AKABADILI NDEGE AKAPANDA KLM AKAFIKA ALGERIA SIKU HIYO HIYO NA ALIPANDA Economy Class KWA WALE WALIOWAHI KUPITIA DUBAI WANAWEZA KUSEMA. HASA KIPINDI HUKI CHA SIKUU DUBAI NI SHIDA SANA SEHEMU YA KULALA NI SHIDA. SASA MLITAKA MUHONGO AWAFRAHISHE AKALALE DUBAI? ACHENI UJINGA
Alijisahau kidogo kwamba ndege ikianguka au kupata shida angani hakuna cha first class au economy class wote huwa wanakufa sawa,sasa angeshauriwa on those lines am sure angejitambua,au vipi akodishe hustler mbona ziko nyingi sana kama anaona atachafuka akikaa na wavuja jasho.