Majanga: Waziri Muhongo Asusia Ndege, Kisa, Kakosa Daraja La Kwanza

Watanzania acheni wivu wa kike na mjadili hoja baada ya kupata upande wa pili.

MUHONGO alikata ndege baada ya kuambiwa inapita DUBAI na wanalala DUBAI.
KWA HALI YA DUNIA HII KWENDA ALGERIA MPKA ULALE NJIANI???
WATU TUNAENDA CHINA MAREKANI HATULALI NJIANI IJE KUA ALGERIA?\
MUHONGO ALISEMA HAWEZI LALA DUBAI KWA SAFARI YA ALGERA

AKABADILI NDEGE AKAPANDA KLM AKAFIKA ALGERIA SIKU HIYO HIYO NA ALIPANDA Economy Class
KWA WALE WALIOWAHI KUPITIA DUBAI WANAWEZA KUSEMA. HASA KIPINDI HUKI CHA SIKUU DUBAI NI SHIDA SANA SEHEMU YA KULALA NI SHIDA. SASA MLITAKA MUHONGO AWAFRAHISHE AKALALE DUBAI? ACHENI UJINGA


Lakini mkuu, wakati wanakata ticket zao si walijua hilo?? Na pia hii si inaonyeshwa kwenye ticket?? Au kulikuwa na mabadiliko, fafanua manake unaonyesha unaijua hii issue vizuri!!!
 
Alijisahau kidogo kwamba ndege ikianguka au kupata shida angani hakuna cha first class au economy class wote huwa wanakufa sawa,sasa angeshauriwa on those lines am sure angejitambua,au vipi akodishe hustler mbona ziko nyingi sana kama anaona atachafuka akikaa na wavuja jasho.
 
Kama hii ni kweli na ndivyo alivyo fanya na msifu kwa uamuzi wake huu. Nasema hivi kwasababu jamaa ni waziri yuko jikoni anajua siri za nchi hii kuwa ni tajiri ya kupindukia. Na pengine yeye kama kiongozi anajua alivyo na wenzake walivyo matajiri. Sasa hana sababu yeyote ya msingi kupanda kajamba nani ya ndege.

Kwa jeuri na dharau ya huyu prof lazima kichwani alikuwa anafikiri hivi, mie nimesoma kuliko rais, halafu yeye apande first class mimi msomi wanipandishe kajamba nani, kama ni huo uwaziri wao wauchukue bwana, si safiri labda wabadilishe hii tiketi.
 
Ben Saa 8. Huko Chadema, mimi CCM damu....Nakwambia, kama kuna mabadiliko kwenye baraza la mawaziri na huyu mtu akabaki kwenye hilo baraza, natupa kadi navaa gwanda. I swear to God !

Utaifa kwanza !

Huyu mtu kazidi matusi kwa watanzania. Kwani kabla ya uwaziri alikuwa anapanda nini, wakati akeidna Musoma alikuwa anapanda basi la kawaida?
Kama kinachosemwa kina ukweli basi Huyu ni Limbukeni na hana huruma na fedha ya umma na si huyu tu hata wabunge na viongozi wote nchi hii .natamani Muumba siku moja anijalie uongozi wa juu nchi hii watu kama hawa watanyooka na ubunge utakuwa ni kazi ya kujitolea na uwakilishi wa kweli na si kitega uchumi kama hivi leo inanyosadikika.Daktari Bingwa wa Binaadamu aliye na PHD ambaye amejituma kwa kukaa Darasani miaka kumi na saba ndani ya fani anaambiwa tunakuajiri kwa mshahara wa milioni moja na laki nne(1,400,000)kabla ya tax na makato mengine take home laki saba na kitu na kufanyakazi ktk mazingira magumu lakini wajinga kama hawa wanafuja pato la Taifa kila leo na bado kuwaona waliowapa dhamana ni wajinga kwasababu tu hawana uwezo wa kuwaadhibu kwa yale wanayowatendea.
 
Atakuja na kisingizio kuna nyaraka alikuwa anataka kuzisoma na asingeweza kufanya hivyo kwenye daraja lingine.
 
[h=3]Business class[/h]
Why fly business?


  • Lie-flat seats allow you to rest and hit the road running for your early morning meeting. (This is a good one to tell to your boss.)
  • You can move around and stretch easily, helping prevent DVT.
  • Fewer crying babies, strange body odors and hysterical first-time flyers.
  • Hate the queues and want to get off the plane quickly as you are pressed for time in your final destination
  • Extra miles to accrue

For a long time, business class was akin to today's premium economy class, that is economy with larger seats and more seat pitch (space for your legs), but the continuing drive to strip all frills out of economy and outcompete other airlines' business classes has seen some major changes in the past decade.

At the airport, business class flyers typically have a separate check-in area or at least their own row, and can access abusiness class lounge that offers drinks, snacks, newspapers and maybe Internet access. Some of the best lounges offer showers and even nap rooms. Note that you can typically only use a business class lounge at your departure airport and when waiting for a connection, although some airlines allow long-haul passengers to use them on arrival as well.
Once on board - and you're usually boarded first - seat pitch in business remains good by any measure: while 91cm (36") is considered unusually generous in economy, few business seats are under 100cm (40") and 130-153cm (50-60") is considered standard. However, for many travellers the most important consideration is recline, particularly the holy grail of the flat bed seat (180° recline, parallel to the floor), which pretty much guarantees a good night's sleep. True flat bed seats are rare and expensive, with British Airways's Club World and Virgin Atlantic's Upper Class pioneering the concept, but lie-flat seats, angled seats like those found in Air France's business class cabin, which recline to an angle of perhaps 170° and are vertically tilted to squeeze in better, are increasingly common. Carriers are also offering herringbone-layout business classcabins. Generally, flat bed service is more expensive and can be found only on premium carriers like Air Canada, Cathay Pacific or Singapore Airlines. Any type of sleeper seat is usually only found on long-haul aircraft - check carefully to see whether your plane is equipped. But a rule of thumb is that if the origin and destination are financial centres far from each other, then it is more likely to get flat-bed seats.
Food and drink in business class is much better than the slop usually encountered in economy class. You can expect to be given actual menus with several choices, with courses served one by one from actual porcelain plates and accompanied by free drinks. Some airlines allow you to preorder from an extensive menu before you fly, in which case the meal will be boarded specially for you.
Entertainment options in business class are also good, with audio and video on demand (AVOD) a standard amenity, either via a display built into your seat or portable DVD players passed out by request. Power sockets for laptops are often provided and Internet access may be available too.
The last perk comes as the end, as you'll be the first out of the plane and into the immigration and customs lines.
 
WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, amegoma kusafiri na Watanzania wenzake kwenda nchini Algeria kwa daraja la kawaida baada ya kukosa daraja la kwanza, hivyo kuahirisha safari yake kwa siku moja, Tanzania Daima limebaini.

Profesa Muhongo ambaye amekuwa akionyesha dharau kwa Watanzania mara kadhaa, aligoma kusafiri katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam Jumapili ya Novemba 24, 2013, saa 10.45 akiwa na wenzake tisa kwenda kwenye safari ya kikazi nchini Algeria alikoenda baadaye.Moja ya kauli ya dharau iliyotolewa hivi karibuni na Waziri Muhongo ni pale aliposema wafanyabiashara Watanzania wana uwezo wa kuwekeza kwenye soda na juisi badala ya gesi na pia aliwahi kuwashambulia viongozi wa dini kwa kuwaita waongo.

Uchunguzi wa Tanzania Daima uliofanyika kwa siku kadhaa sasa, umethibitisha kwamba Muhongo alikuwa aondoke na ndege ya shirika la ndege la Emirates namba EK 726 kutoka Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere kupitia Dubai kwenda Algeria akiwa na tiketi ya daraja la kawaida bila kujua kabla ya kufika uwanjani hapo na kisha kuanza kumfokea kila aliyekuwa anamsemesha.

“Tiketi yake na wenzake kumi ilikuwa ni Economy Class (Daraja la Kawaida), lakini akakataa akitaka asafiri kwa First Class (Daraja la Kwanza). Alibembelezwa na wenzake na wafanyakazi wa Emirates na wale wa Uwanja wa Ndege lakini akagoma huku akifoka na wenzake wakataka kuahirisha safari.

Ikawa tena ni sisi kuwaomba wasafiri ili Bwana Mkubwa (Muhongo) atafutiwe nafasi kwa daraja analotaka.
“Walimbembeleza wakamwambia kwa kutumia ‘millage’ ya safari zake watambadilishia akiwa ndani ya ndege na kumuweka daraja la kwanza lakini alionekana ameshakuwa mkali na hakuwa anamsikiliza yeyote.“Baadaye tulifanikiwa kuwashawishi wenzake kuendelea na safari na yeye sijui aliondoka na ndege gani tena maana wakubwa wetu wana mambo sana,” anasema ofisa mmoja uwanjani hapo.

Taarifa za awali kuhusu sakata hili, ziliripotiwa siku hiyo katika mtandao wa jamiiforums.com zikieleza kwamba kitendo cha Waziri Muhongo cha kususia safari hiyo, kiliwakera baadhi ya wasafiri wakiwamo raia wa kigeni ambao walishangazwa na hatua hiyo ya kiongozi wa nchi maskini inayotegemea misaada kulazimisha kusafiri kwa daraja la kwanza, daraja ambalo viongozi wa mataifa makubwa hawaruhusiwi kusafiri bila sababu maalumu.

Taarifa hiyo kwenye mtandao wa JamiiForums. Com iliripotiwa hivi: “Kweli viongozi wa nchi hii wanatia aibu, wakati mawaziri wa Uingereza wanakataa First Class, hapa kwetu kimetokea kioja. Waziri wenu wa Nishati na Madini (Muhongo) ambaye anazidi kutulaza na joto na giza leo amewaacha hoi Watanzania pale alipofika mpaka Airport na akiwa anaboard akakuta anawekwa sehemu ya abiria wa daraja la kati, baada ya kuambiwa hayuko First Class akagoma na kutoka nje ya mlango. Wakati hayo yakiendelea kumbe ana wenzake zaidi ya tisa wako economy na wawili Bussiness Class, ghafla nao wakaanza kushuka.

“Hapo ndipo hekima za mmoja wa wahusika wa Airline (Emirates) akawaomba hao waende ili yeye akabadilishe aje kesho yake.” “Jamani kweli First Class inakushushia aibu hivi Profesa na bado unasema maisha magumu Tanzania!? Inaonekana zile buti za bora ulizivalia ukiwa form V na haya ndio madhara yake, mnapewa vyeo wakati maisha yalishawapiga; mnatafuta muafaka na Yesu mkiwa madarakani,” anaeleza mtu aliyewasilisha mada husika akijulikana kwa jina la Basiasi.

Basiasi alihoji sababu ya abiria wenzake ambao nao walikuwa wakisafiri kikazi kutaka kushuka na kusababisha hasara kwa serikali au wafadhili waliokata tiketi hizo. Kwa utaratibu wa kawaida abiria anayeahirisha safari baada ya kuwa ameshaingia ndani ya eneo la kusafiria (boarding) anaweza kupoteza kabisa tiketi au kulipishwa fedha nyingi zinazoweza kuwa sawa na kununua tiketi mpya.

“Hebu kuweni wastaarabu, sasa wale watu tisa walitaka kuwashusha kwa nini na kama wamekwenda, mlishindwa kuwaambia wabaki mpaka mkaanza kuleta aibu uwanjani? Inaonekena ndege mmeanza kupanda uzeeni; najiuliza kivipi unaletewa tiketi hata kama na ‘travel agency’ halafu unashindwa kuuliza au kukagua mpaka unaenda uwanjani na unapewa ‘boarding pass’ bado unashindwa kukagua ipi ‘bussiness class’ na ipi ‘first class’!” anahoji Basiasi. Abiria mmoja aliyenukuliwa na Jamiiforums alisema kwa waziri wa nchi kama Uingereza anatakiwa kutoa maelezo ya sababu za kusafiri na daraja la kwanza (first class) ikiwa atalazimika kufanya hivyo, vingine viongozi husafiri kwa madaraja ya kawaida.

Wakati Waziri Muhongo akisusia ndege kwa kukosa nafasi ya kusafiri na daraja la kwanza, baadhi ya mawaziri wanaofanya ziara mikoani na kusafiri kwa ndege, hulazimika kuyaagiza mashangingi yao kutoka Dar es Salaam hadi katika mikoa wanayokwenda kufanya ziara hizo hata kama yatatumika kwa siku moja.

Umasikini ni kitu kibaya sana huyo profesor majalala amedhihilisha
 
Ben Saa 8. Huko Chadema, mimi CCM damu....Nakwambia, kama kuna mabadiliko kwenye baraza la mawaziri na huyu mtu akabaki kwenye hilo baraza, natupa kadi navaa gwanda. i swear to God !

Mgiro anaweza kuchukua nafasi yake.
 
Dk Slaa alisema pia kuwa Chadema kitatumia wabunge wake kuibana Serikali kuhusu Fedha za ruzuku ya kilimo zinazotolewa kwa ajiri ya maendeleo ya kilimo lakini zimekuwa zikatafunwa na wajanja wachache"source Mwananchi leo
Angalizo,sialalishi wizi,na sipendi wezi kuwaita wajanja,Je Slaa yupo tayali kuwajibika sababu utafanaji olela wa ruzuku ndani ya CDM
 
Kama booking na subsequent ticket ilikuwa ni first class then Prof Muhongo is right to be irate. Kama ni mbwembwe za kulazimisha first class then that is another debate on its own. Tanzania I think has some of the most wasteful spending sio tu kwa mawaziri bali pia wa watumishi wa umma kwa ngazi zote. Umasikini ni mzigo.
 
Mmm hii kali anyway mimi namsifu Wasira kwani siku ya Jpili natoka Mwanza baba wa watu alikaa kwenye zile siti za mbele pembeni wala hakutaka kumsumbua mtu pamoja na uwaziri wake .Big up Wasira mfundishe mwenzio ajishushe kidogo tu asinge kufa au kukonda wote tu binadam

Hiyo seat unayosema ndiyo daraja la kwanza kwa ndege zetu hapa.
 
Maskini akipata.........................





View attachment 125210

waziri wa nishati na madini, profesa sospeter muhongo, amegoma kusafiri na watanzania wenzake kwenda nchini algeria kwa daraja la kawaida baada ya kukosa daraja la kwanza, hivyo kuahirisha safari yake kwa siku moja, tanzania daima limebaini.

profesa muhongo ambaye amekuwa akionyesha dharau kwa watanzania mara kadhaa, aligoma kusafiri katika uwanja wa ndege wa julius nyerere, dar es salaam jumapili ya novemba 24, 2013, saa 10.45 akiwa na wenzake tisa kwenda kwenye safari ya kikazi nchini algeria alikoenda baadaye.


moja ya kauli ya dharau iliyotolewa hivi karibuni na waziri muhongo ni pale aliposema wafanyabiashara watanzania wana uwezo wa kuwekeza kwenye soda na juisi badala ya gesi na pia aliwahi kuwashambulia viongozi wa dini kwa kuwaita waongo.


uchunguzi wa tanzania daima uliofanyika kwa siku kadhaa sasa, umethibitisha kwamba muhongo alikuwa aondoke na ndege ya shirika la ndege la emirates namba ek 726 kutoka uwanja wa ndege wa mwalimu nyerere kupitia dubai kwenda algeria akiwa na tiketi ya daraja la kawaida bila kujua kabla ya kufika uwanjani hapo na kisha kuanza kumfokea kila aliyekuwa anamsemesha.


“tiketi yake na wenzake kumi ilikuwa ni economy class (daraja la kawaida), lakini akakataa akitaka asafiri kwa first class (daraja la kwanza). Alibembelezwa na wenzake na wafanyakazi wa emirates na wale wa uwanja wa ndege lakini akagoma huku akifoka na wenzake wakataka kuahirisha safari.

ikawa tena ni sisi kuwaomba wasafiri ili bwana mkubwa (muhongo) atafutiwe nafasi kwa daraja analotaka.

“walimbembeleza wakamwambia kwa kutumia ‘millage’ ya safari zake watambadilishia akiwa ndani ya ndege na kumuweka daraja la kwanza lakini alionekana ameshakuwa mkali na hakuwa anamsikiliza yeyote.


“baadaye tulifanikiwa kuwashawishi wenzake kuendelea na safari na yeye sijui aliondoka na ndege gani tena maana wakubwa wetu wana mambo sana,” anasema ofisa mmoja uwanjani hapo.

taarifa za awali kuhusu sakata hili, ziliripotiwa siku hiyo katika mtandao wa jamiiforums.com zikieleza kwamba kitendo cha waziri muhongo cha kususia safari hiyo, kiliwakera baadhi ya wasafiri wakiwamo raia wa kigeni ambao walishangazwa na hatua hiyo ya kiongozi wa nchi maskini inayotegemea misaada kulazimisha kusafiri kwa daraja la kwanza, daraja ambalo viongozi wa mataifa makubwa hawaruhusiwi kusafiri bila sababu maalumu.

taarifa hiyo kwenye mtandao wa jamiiforums. Com iliripotiwa hivi: “kweli viongozi wa nchi hii wanatia aibu, wakati mawaziri wa uingereza wanakataa first class, hapa kwetu kimetokea kioja. Waziri wenu wa nishati na madini (muhongo) ambaye anazidi kutulaza na joto na giza leo amewaacha hoi watanzania pale alipofika mpaka airport na akiwa anaboard akakuta anawekwa sehemu ya abiria wa daraja la kati, baada ya kuambiwa hayuko first class akagoma na kutoka nje ya mlango. Wakati hayo yakiendelea kumbe ana wenzake zaidi ya tisa wako economy na wawili bussiness class, ghafla nao wakaanza kushuka.


“hapo ndipo hekima za mmoja wa wahusika wa airline (emirates) akawaomba hao waende ili yeye akabadilishe aje kesho yake.”

“jamani kweli first class inakushushia aibu hivi profesa na bado unasema maisha magumu tanzania!? Inaonekana zile buti za bora ulizivalia ukiwa form v na haya ndio madhara yake, mnapewa vyeo wakati maisha yalishawapiga; mnatafuta muafaka na yesu mkiwa madarakani,” anaeleza mtu aliyewasilisha mada husika akijulikana kwa jina la basiasi.

basiasi alihoji sababu ya abiria wenzake ambao nao walikuwa wakisafiri kikazi kutaka kushuka na kusababisha hasara kwa serikali au wafadhili waliokata tiketi hizo.

kwa utaratibu wa kawaida abiria anayeahirisha safari baada ya kuwa ameshaingia ndani ya eneo la kusafiria (boarding) anaweza kupoteza kabisa tiketi au kulipishwa fedha nyingi zinazoweza kuwa sawa na kununua tiketi mpya.

“hebu kuweni wastaarabu, sasa wale watu tisa walitaka kuwashusha kwa nini na kama wamekwenda, mlishindwa kuwaambia wabaki mpaka mkaanza kuleta aibu uwanjani? Inaonekena ndege mmeanza kupanda uzeeni; najiuliza kivipi unaletewa tiketi hata kama na ‘travel agency’ halafu unashindwa kuuliza au kukagua mpaka unaenda uwanjani na unapewa ‘boarding pass’ bado unashindwa kukagua ipi ‘bussiness class’ na ipi ‘first class’!” anahoji basiasi.


abiria mmoja aliyenukuliwa na jamiiforums alisema kwa waziri wa nchi kama uingereza anatakiwa kutoa maelezo ya sababu za kusafiri na daraja la kwanza (first class) ikiwa atalazimika kufanya hivyo, vingine viongozi husafiri kwa madaraja ya kawaida.


wakati waziri muhongo akisusia ndege kwa kukosa nafasi ya kusafiri na daraja la kwanza, baadhi ya mawaziri wanaofanya ziara mikoani na kusafiri kwa ndege, hulazimika kuyaagiza mashangingi yao kutoka dar es salaam hadi katika mikoa wanayokwenda kufanya ziara hizo hata kama yatatumika kwa siku moja.
 
Ebu acha ushamba wewe, una ushahidi wa kilichowekwa hapa jukwaani?? Na kama ni kweli jee umejua sababu ya mhongo kukataa kupanda bisnes clas? Na una uhakika kakataa kupanda au kaahirisha ziara?

Mimi naona ni umbea tuu huu. Nina mengi ya kujadili.

Kweli nimeamini ukiwa maccm unakuwa na akili kama maiti. Umehamia juzi tu nawe umekuwa wale waleeeeeee.
 
Kama hii ni kweli na ndivyo alivyo fanya na msifu kwa uamuzi wake huu. Nasema hivi kwasababu jamaa ni waziri yuko jikoni anajua siri za nchi hii kuwa ni tajiri ya kupindukia. Na pengine yeye kama kiongozi anajua alivyo na wenzake walivyo matajiri. Sasa hana sababu yeyote ya msingi kupanda kajamba nani ya ndege.

Kwa jeuri na dharau ya huyu prof lazima kichwani alikuwa anafikiri hivi, mie nimesoma kuliko rais, halafu yeye apande first class mimi msomi wanipandishe kajamba nani, kama ni huo uwaziri wao wauchukue bwana, si safiri labda wabadilishe hii tiketi.

Masikini akipata makalio hulia mbwaaaa!!!!!! hii ni dalili tosha ya Darfur a.k.a njaa,dhiki utotoni.
 
Lakini mkuu, wakati wanakata ticket zao si walijua hilo?? Na pia hii si inaonyeshwa kwenye ticket?? Au kulikuwa na mabadiliko, fafanua manake unaonyesha unaijua hii issue vizuri!!!

ndio kulikua na mabadiliko ya tiket na ndio maana waziri akawa na uwezo wa kubadili ndege maana hakutaarifiwa kama ndege itapita dubai na watalala dubai

na yeye hakutaka kulala dubai maana matatizo ya dubai hasa kippindi hiki yanajulikana sehemu ya kulala ni shida sana

tatizo wengi wenu mnacoment hapa hata ndege hamjawahi kupanda ndio maana mnatoa mishipa

ivi nyie TANZANIA DAIMA kabla ya kuandika hii habari mlimuuliza Mh waziri ilikuaje? au ni ule mwendelzo wenu wa kmchafua?
mliandika amewatuka Maaskofu ila baadae Askofu ndege na Askofu Kilaini wakakanusha lakn mkashindwa kuandika.
acheni ujinga jengeni Nchi yenu siasa za kuchafua mawaziri wanaofanya kazi muache wafanye kazi
 
Watanzania acheni wivu wa kike na mjadili hoja baada ya kupata upande wa pili. MUHONGO alikata ndege baada ya kuambiwa inapita DUBAI na wanalala DUBAI. KWA HALI YA DUNIA HII KWENDA ALGERIA MPKA ULALE NJIANI??? WATU TUNAENDA CHINA MAREKANI HATULALI NJIANI IJE KUA ALGERIA?\ MUHONGO ALISEMA HAWEZI LALA DUBAI KWA SAFARI YA ALGERA AKABADILI NDEGE AKAPANDA KLM AKAFIKA ALGERIA SIKU HIYO HIYO NA ALIPANDA Economy Class KWA WALE WALIOWAHI KUPITIA DUBAI WANAWEZA KUSEMA. HASA KIPINDI HUKI CHA SIKUU DUBAI NI SHIDA SANA SEHEMU YA KULALA NI SHIDA. SASA MLITAKA MUHONGO AWAFRAHISHE AKALALE DUBAI? ACHENI UJINGA
Mkuu kila mtu mwenye akili timamu anajua Prof. hawezi kufanya mambo ya kijinga, kwa bahati mbaya kuna Watanzania wenzetu wamejipanga kumzulia Mh.Muhongo kashifa za kila sampuri, kila anacho sema kinakuwa grossly misinterpreted kimakusudi, kila alifanyalo mahasimu wake wanaliona lina WALAKINI!! Mimi namshauri Prof. Muhogo achape kazi na kuinua Uchumi wa Taifa letu, uwezo huo anao sana aogopi kusema ukweli na nana interest za Taifa letu ndani ya moyo wake - asiwasikilize watu waigizaji wanao jifanya wana majibu ya kila tatizo linalo kabiri Taifa letu specifically nyanja za "GESI NA MAFUTA".
 
Alijisahau kidogo kwamba ndege ikianguka au kupata shida angani hakuna cha first class au economy class wote huwa wanakufa sawa,sasa angeshauriwa on those lines am sure angejitambua,au vipi akodishe hustler mbona ziko nyingi sana kama anaona atachafuka akikaa na wavuja jasho.

acheni ujinga waziri hajakataa ndege kwa sababu hakupata 1CLASS si kweli ni umbea mtupu
waziri alikataa kupitia na kulala DUBAI, Na hata alipopanda KLM Economy Class

ivi kwa dunia ya sasa kwenda ALGERIA lazima ulale njiani? watu tunaenda china na Marekani hatulali njiani ije kua hapa jiran ALGERIA?
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom