Majambo mbaya kitandani

BIN BOR

JF-Expert Member
Nov 23, 2010
1,013
407
Harry alipochoka kufanya kazi zake akazima taa, akambusu mkewe, akalala na usingizi mzito ukampitia. Mara akamwona mwanamme amesimama kitandani.

"Toka hapa nani wewe unakuja kitandani kwangu?"
"mimi ni mtakatifu Petro na hapa si kitandani kwako bali ni mbinguni"
"Ina maana nimekufa? Mbona mimi bado kijana? Naomba unirudishe duniani."
"Inawezekana, lakini siwezi kukurudisha kama mtu, labda nikurudishe kama mbwa au kuku"

Harry akakumbuka mbwa anavyopata taabu ya kulinda, " Bora nirudi kama kuku"

Mara akajikuta yuko kwenye banda, akiwa kuku jike na matakoni kunawaka moto. Akamwona jogoo pembeni, akamwambia shida yake.

"Kaka ninasikia moto matakoni, inakuwaje?"
"Kwani hujawahi kutaga weye?" Jogoo akamjibu kwa maringo.
"Sijawahi"
"Chuchumaa, kamua kwa nguvu yai litoke."

Basi akakamua, yai la kwanza likatoka, akakamua tena yai la pili hilo! Akiwa anataka kukamua yai la tatu akasikia sauti ya mke wake.

"Harry, pumbavu wewe, unakunya kitandani!"
 
kwi kwi kwi tehe tehe tehe teeeheee.................nimecheka sanaaaaaaaaaaaaa
 
Hhahahahahahahahahahaaah nimecheka mpaka nami majambo mbaya yamenitoka.
 
HAHAHAHAHAHAHAHAHAHAHAHAHAHAHAHAHAHAHAH.......nadhani kwa leo siku yangu ndio imeisha.


 
Duh wewe ni noma tena zaidi ya noma nimecheka sanaaaaaaaaaaaaaa
 
Huu utani unanikumbusha enzi zileee nilipokuwa kikojozi....naota niko nje natoa nanihii nakojoa....naanza tu nashtuka usingizini naamka mbio wakati mkojo unatoka nawaloesha wenzangu wawili niliolala nao.....kurudi wanakuwa mbogo naishia kulala "umwango" I mean sebuleni.
 
Nakusalutia mkuu umenifanya simanzi yote ya kuitafakali nchi hii na wanadishaji wake inatoke kwa muda .
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…