fab280391
Senior Member
- Jul 29, 2015
- 122
- 31
Leo eneo La Chanika, Dar es salaam mida ya saa 9 jioni majambazi wapatao zaidi ya 8 wavamia na kuziteka Bank mbili zilizo eneo moja kwa muda wa dakika 45. CRDB ambayo hata haijaanza kufanya kazi rasmi na DCB Bank..
Majambazi walikuwa na Pikipiki 4 aina ya boxer, gari tinted na Silaha za kivita wamefanikiwa kuchukua pesa nyingi, kuua walinzi 2 wa Suma JKT na kujeruhi wafanyakazi wengine..
Polisi wamefika dakika 15 baada ya majambazi kuondoka ijapokuwa kituo kidogo cha Polisi kipo karibu ni kama umbali wa dakika 10 kwa miguu kutoka Bank.
=================
Majambazi walikuwa na Pikipiki 4 aina ya boxer, gari tinted na Silaha za kivita wamefanikiwa kuchukua pesa nyingi, kuua walinzi 2 wa Suma JKT na kujeruhi wafanyakazi wengine..
Polisi wamefika dakika 15 baada ya majambazi kuondoka ijapokuwa kituo kidogo cha Polisi kipo karibu ni kama umbali wa dakika 10 kwa miguu kutoka Bank.
=================
Kamanda wa Polisi mkoa wa Ilala, Ulrich Matei, ameithibitishia JamiiForums kutokea kwa tukio hilo na kwamba majambazi hao wanasadikiwa kuwa walikuwa kati ya 6 hadi 8.
Amesema wahalifu hao walianza kuingia kwenye Benki ya DCB na kupora fedha zilizokuwa kaunta na muda mchache baada ya hapo walivamia Benki ya CRDB na kupora fedha ambazo hadi sasa haijajulikana thamani yake.
Aidha, amesema majambazi hao waliwaua askari wawili wa Suma JKT, waliotambuliwa kwa majina ya Ramadhani Halidi na Shane Rajabu.
"Tumeanza upelelezi ikiwemo kuelekea katika maeneo ya Mkuranga ambapo ndiko tunakoamini kwamba hawa wahalifu wameelekea, tutakapowakamata tutawapa taarifa kamili" alikaririwa na JamiiForums.