voicer
JF-Expert Member
- Jul 13, 2020
- 5,545
- 11,943
Naipongeza serikali kwa kumpatia ajira Majaliwa. Lakini ninakosoa aina na mahali walikompeleka.
Majaliwa ni shujaa mzamiaji wa Majini
(Deep Water Diver), kwenye vina virefu vya Maji na siyo majumbani kwenye Swiming Pool au Kwenye Matundu ya vyoo ambako ndio hasa zimamoto wanawajibika.
Lakini pia nimeshangaa kusikia kwamba Majaliwa tayari amesajiliwa na serikali kwenye Jeshi la Zimamoto.
Na tayari yuko mbioni kupelekwa Handeni Tanga, kwa Mafunzo ya Miezi minne na baadae ataanza rasmi kazi yake katika ajira hiyo mpya!
Sasa nikajiuliza maswali haya ya msingi.
Hivi kwa Mafunzo ya miezi minne pekee, tayari mtu anakuwa Askari "Competent" wa uokoaji na Zimamoto?
Hivi kwa miezi minne pekee, unakuwa tayari umepitia mafunzo ya uokoaji wa Mioto ya aina zote, kuanzia
Hapo bado hatujaongelea mafunzo ya ukakamavu na ujasiri wa mbinu za kijeshi, kwa mtaala wa jeshi lao la zimamoto.
Kama hao askari wa zimamoto huwa wanafundishwa kwa mtindo na speed ya zimamoto ndiyo maana huwa tunawaona wakishindwa kwenye matukio na majanga mengi ya moto nchini.
Miezi minne ni muda mfupi sana kwa mafunzo ya kitengo nyeti kama jeshi la zimamoto!
Hiyo ilipaswa kuwa ni muda wa kukaa darasani pekee, ili kuzijua aina mbalimbali tofauti za mioto. Pamoja na jinsi ya kuzijua chemical husika kwa kila aina ya moto. Baadae ndio angepelekwa kwenye field training.
Lakini pia huyo kijana ni Diver na sio mzimamoto!
Alamsikhi!
10101
Majaliwa ni shujaa mzamiaji wa Majini
(Deep Water Diver), kwenye vina virefu vya Maji na siyo majumbani kwenye Swiming Pool au Kwenye Matundu ya vyoo ambako ndio hasa zimamoto wanawajibika.
Lakini pia nimeshangaa kusikia kwamba Majaliwa tayari amesajiliwa na serikali kwenye Jeshi la Zimamoto.
Na tayari yuko mbioni kupelekwa Handeni Tanga, kwa Mafunzo ya Miezi minne na baadae ataanza rasmi kazi yake katika ajira hiyo mpya!
Sasa nikajiuliza maswali haya ya msingi.
Hivi kwa Mafunzo ya miezi minne pekee, tayari mtu anakuwa Askari "Competent" wa uokoaji na Zimamoto?
Hivi kwa miezi minne pekee, unakuwa tayari umepitia mafunzo ya uokoaji wa Mioto ya aina zote, kuanzia
- Uokoaji na uzimaji mioto kwenye majengo Marefu
- Uokoaji na uzimaji moto Viwandani.
- Uokoaji na uzimaji mioto kwenye Sehemu zenye Msongamano mkubwa wa Majengo na watu.
- Uokoaji na uzima moto katika viwanja vya Ndege
- Uokoaji na Uzima moto katika vyombo vya Majini.
Hapo bado hatujaongelea mafunzo ya ukakamavu na ujasiri wa mbinu za kijeshi, kwa mtaala wa jeshi lao la zimamoto.
Kama hao askari wa zimamoto huwa wanafundishwa kwa mtindo na speed ya zimamoto ndiyo maana huwa tunawaona wakishindwa kwenye matukio na majanga mengi ya moto nchini.
Miezi minne ni muda mfupi sana kwa mafunzo ya kitengo nyeti kama jeshi la zimamoto!
Hiyo ilipaswa kuwa ni muda wa kukaa darasani pekee, ili kuzijua aina mbalimbali tofauti za mioto. Pamoja na jinsi ya kuzijua chemical husika kwa kila aina ya moto. Baadae ndio angepelekwa kwenye field training.
Lakini pia huyo kijana ni Diver na sio mzimamoto!
Alamsikhi!
10101


