boyson onlye
JF-Expert Member
- Sep 13, 2015
- 1,109
- 1,398
Nawasalimu,
Kuna ile Hasira iliyoko ndani yangu ya mafanikio kuna yale mawazo yaliyoko katika ubongo wangu wa namna ya kupata mafanikio, kila nikijaribu nafanikiwaje sioni njia, unakata tamaa asubuhi unajipa moyo labda leo itakuwa siku ya furaha, lakini wapi ukipita barabara unajiuliza mtu amewezaje kupata pesa mpaka akanunua pikipiki mwingine amewezaje kupata pesa mpaka akanunua gari na huyu anapataje pesa ya kujenga unakaa unafikiria inakatisha tamaa.
Unadaiwa na watu wako wote wa karibu unaona kabisa upendo wa ndugu umepungua unajihisi wewe ni binadamu usiye na akili duniani maana unashindwa kufikiria njia ya kupata pesa kama wengine wanavyopata, unaishi mwenyewe hakuna kijana mtu wa makamo hata Mzee wa kukutia moyo na kukushauri, unajihisi mpweke dunia imekuelemea, ukienda kwenye Nyumba za ibada unaona wenzako wanaenda kutoa sadaka wewe unashindwa hata kunyanyuka, unaona namna ambavyo wana ahidi michango mikubwa na mafungu ya kumi ni mamilioni ila unashindwa kutoa elfu moja maisha yanachosha.
Washikaji wanashindwa kukuonyesha hata njia au kukupa madili unaachwa na mchumba kisa unaonekana huna future (angejua yaliko kichwani) hakika asingewaza hayo yote.
Maisha yanachosha umejitahidi kusoma na mpaka sasa yule uliyemzidi elimu amepata mpenyo wa pesa ila ww huna chochote cha kuuza ukiwa na shida, Maswali kichwani hayaishi nifanye nini, nipataje pesa, nitakuwaje tajiri, nitaishi hivi mpaka lini? Nitakuja kuwa na familia siku moja itaishije kama hali yenyewe ndio hii.
Akili imechoka moyo umeondoa tumaini mbili huna nguvu, unatamani kuzima simu maana ukipigiwa simu ni mtu anakumbusha Deni lake.
Maisha yanachosha
Kuna ile Hasira iliyoko ndani yangu ya mafanikio kuna yale mawazo yaliyoko katika ubongo wangu wa namna ya kupata mafanikio, kila nikijaribu nafanikiwaje sioni njia, unakata tamaa asubuhi unajipa moyo labda leo itakuwa siku ya furaha, lakini wapi ukipita barabara unajiuliza mtu amewezaje kupata pesa mpaka akanunua pikipiki mwingine amewezaje kupata pesa mpaka akanunua gari na huyu anapataje pesa ya kujenga unakaa unafikiria inakatisha tamaa.
Unadaiwa na watu wako wote wa karibu unaona kabisa upendo wa ndugu umepungua unajihisi wewe ni binadamu usiye na akili duniani maana unashindwa kufikiria njia ya kupata pesa kama wengine wanavyopata, unaishi mwenyewe hakuna kijana mtu wa makamo hata Mzee wa kukutia moyo na kukushauri, unajihisi mpweke dunia imekuelemea, ukienda kwenye Nyumba za ibada unaona wenzako wanaenda kutoa sadaka wewe unashindwa hata kunyanyuka, unaona namna ambavyo wana ahidi michango mikubwa na mafungu ya kumi ni mamilioni ila unashindwa kutoa elfu moja maisha yanachosha.
Washikaji wanashindwa kukuonyesha hata njia au kukupa madili unaachwa na mchumba kisa unaonekana huna future (angejua yaliko kichwani) hakika asingewaza hayo yote.
Maisha yanachosha umejitahidi kusoma na mpaka sasa yule uliyemzidi elimu amepata mpenyo wa pesa ila ww huna chochote cha kuuza ukiwa na shida, Maswali kichwani hayaishi nifanye nini, nipataje pesa, nitakuwaje tajiri, nitaishi hivi mpaka lini? Nitakuja kuwa na familia siku moja itaishije kama hali yenyewe ndio hii.
Akili imechoka moyo umeondoa tumaini mbili huna nguvu, unatamani kuzima simu maana ukipigiwa simu ni mtu anakumbusha Deni lake.
Maisha yanachosha