Hapa tusiwe ma "motivational speakers", hiko ulichoandika asimilia kubwa ya vijana tumepitia,tutapitia na tunapitia
Na hapo ulipo huwezi kujitoa wewe mwenyewe,ni UONGO
Hii ni siri niliyoanza kujifunza,unahitaji pesa,sawa?
Hakuna anayeweza kukupa pesa yake bure,eti kwa kumuelezea tu matatizo yako,probability ya watu kama hao ni almost zero
Hivi umeshawahi kujiuliza watu wanatoaje pesa?
Wape kitu kinachoongeza "value" kwenye maisha yao,njoo na bidhaa au idea yenye uwezo wa kutengeneza value kwenye maisha yao
Assume una Tsh 0.00,ila una ubongo
Fikiria kitu gani ukinambia Mimi kwenye Tsh 5,000 mkononi kitanifanya nikupe Tsh 1,000 yangu
Njoo na wazo au kitu kitakacho nipa mimi mwenye Tsh 5,000 value ya Tsh 3,000 halafu niuzie hiko kitu au hilo wazo kwa Tsh 2,000
Hapo tutakua tumetengeneza Tsh 1,000 out of nothing, na kesho nitawambia wezangu wenye Tsh 5,000 na zaidi kuhusu wewe
Huna pesa,usilalamike na kukataa tamaa,hii dunia haina huruma
Ndio maana hata binadam alitengeneza "After Life" kwa ajiri yake tu,ushawahi jiuliza "Sokwe" wakifa wanaenda wapi?
Jifunze kutengeneza pesa out of nothing, jifunze kutengeneza kitu chenye "value"
Jifunze valuable skills,kuwa best kwenye hio skill
Watu watakupa pesa tu