Maisha yamenishinda nahama mjini

Maisha yamenishinda nahama mjini

ulivyokuwa unashinda baa ulitegemea nini?????????????????? Kwa heri, hakikisha umenunua jembe, panga shoka mundu, mkuki , hizo noi baadhi ya zana zitumikazo kijijini kila siku

kuna watu hupaswi kabisa kuwaomba ushauri fikiria huu ndo ushauri unapewa?!
 
Pole mkuu. Umeandika kwa hisia sana, usikate tamaa kwani hapa mjini ulikua unajihusisha na nini? Kwanini umeshindwa? Wateja hamna? Usiondoke mjini hiyo slogan ya chama wala isikuumize kichwa
 
Wapendwa! Habari za jioni, poleni kwa pilika na majukumu ya mchana kutwa. Pamoja na hayo naomba niungane nanyi katika kutoa ushauri kwa huyu Mpendwa ambaye ameweka mada yake mbele yetu. Hata hivyo niombe tuwe makini katika kumshauri, kwani nachelea kama tunamshauri kwa utani, nadhani itakuwa haina maana kwake na kwa wengine ambao labda wana tatizo kama lake.

Kwa Upande wa Kereng'ende, naomba nikushauri kuwa, suala la maisha ni changamoto kwa kila mwanadamu chini ya jua hili, hivyo una wajibu wa kujiuliza je ni kwa namna gani unajipanga na kukabiliana na changamoto hiyo. Inawezekana ukaona kurudi kijijijni ni suala bora, mimi sikatai, lakini ni lazima ujiulize, je unakwenda kijijini kufanya nini, hapa kinachotakiwa ni kwa namna gani unajibidisha na kujipangilia mikakati ya kimaendeleo, si wapi unajipangilia kupata hayo maendeleo.

Leo unapokuwa katika eneo fulani kama hujajibidisha ni sawa na kuwasha moto na kuweka pembeni, sufuria la maji ya ugali umeweka pembeni na pia unga na mwiko uko pembeni halafu unasubiri maji ya ugali yachemke ili usonge ugali. Hapo utakuwa unajidanganya kwani hautakaa ule ugali hata siku moja. Hapa lazima utumie Jiko (AKILI) yako kuwasha moto, Weka sufuria ya maji jioni (Fanya bidii kufanya kazi) na uweke unga na kusonga (Fanya maombi kwa Mungu), ukitumia vema neema ya Mungu iliyopo ndani yako.

Kwa namna utakavyojipanga leo ndivyo ambavyo maisha yako yatakavyokuwa kesho kwa neema ya Mungu, usilalamike wala kuona mfumo wa siasa una shida la! Jiulize wewe umefanya jitihada gani? Timiza wajibu wako!!
 
wana jf, mm nawashukuru kwa ushauri mzuri kwa huyu mdau. Tupo wengi wenye msongo wa mawazo kutokana na maisha magumu, jana usingizi umekata saa 5 halafu sijasinzia tena hd asubuhi, maswali mengi majibu hakuna. Leo nimemshirikisha jamaa yangu, kanishauri nikomae lkn niache tabia ya kujilinganisha na "mwenye maisha yao" bali nijipange kwa level yangu, vinginevyo nitadata. Najaribu kufanyia kazi, lkn dah, si mchezo wandugu! Nawashukuru wachina kurahisha hii technolojia nami kuweza kuzama hapa jamvini. Usiku mwema kwenu wote.
 
wana jf, mm nawashukuru kwa ushauri mzuri kwa huyu mdau. Tupo wengi wenye msongo wa mawazo kutokana na maisha magumu, jana usingizi umekata saa 5 halafu sijasinzia tena hd asubuhi, maswali mengi majibu hakuna. Leo nimemshirikisha jamaa yangu, kanishauri nikomae lkn niache tabia ya kujilinganisha na "mwenye maisha yao" bali nijipange kwa level yangu, vinginevyo nitadata. Najaribu kufanyia kazi, lkn dah, si mchezo wandugu! Nawashukuru wachina kurahisha hii technolojia nami kuweza kuzama hapa jamvini. Usiku mwema kwenu wote.

pole sana mkuu Mwenyezi Mungu akupe wepesi ,tuongeze maombi,imani na matumaini kwa Mungu tutafika pazuri siku moja!,
 
Dah.. Nimejifunza mengi kwenye hii thread kuhusu maisha kiujumla. Changamoto hazikimbiwi zaidi ya kupambana nazo tu na uende wapi bado utahitai pesa ya kununua chakula, maradhi na pakuegesha ubavu wako. Chamsingi nikujipanga upya na kutochoka kufanya kazi kwa bidii. Yote yanawezekana.
 
Akuna kukata tamaa kwenye maisha haya komaa kama umeamia kjjn poa tu lkn tambua ulichoendea huko utafanikiwa pa1 sana
 
Maisha ni safar ndefu ya taka moyo mkuu na jitihada? Zako yani kutafuta bila kuchoka..
 
Sio mbaya rudi bushi kapumzishe akili, usibweteke tu. Zichange kiaina then rudi mjini. Ila ukirudi mjini njo na plan mpya inayotekelezeka. Ukiona unataka mtaji wa haraka haraka piga selli hiyo kibanda yako, then kamata biashara utakayofikiria inalipa. Hizo ni chzngz,oto za maisha tuuuuu, usikate tamaaaa.
 
Kijijin ndo majanga kabsa!kama hujawah kuish humo, wenzio wanatoka kijijin wanakuja mjin!we unataka ufanye kinyume chake, thnk twice abt ths mkuu,maisha ni kuparangana,tumezaliwa kupambana!usikate tamaa...#okbye
 
ushawahi kujiuliza kwann wa kijijini wanakimbilia mjini!?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom