mapesa yamejaa
JF-Expert Member
- Dec 29, 2021
- 1,412
- 3,403
Baadhi ya maeneo Dar es salamu wanaishi maisha magumu sana hasa wilaya ya Ubungo hasahasa jimbo la kibamba. Ukifika maeneo haya ya jimbo la kibamba kama kule kanisa katoliki msakuzi, kwa lubaba, lipelanya dolphin, mpiji magoe,mbezi misumi n.k maisha ya watu wa kule ni sawa na maisha ya watu walioishi miaka ya 1800.
Yaani sehemu kubwa ya jimbo la kibamba hakuna maji. Wananchi wanavuna maji ya mvua inaponyesha na msimu wa masika ukipita kila mtu atajua kivyake atakapopata maji. Kama ni kufuata kimara au huko mbali yalikoishia maji ya dawasa. Dawasa wao hawana muda wa kupeleja maji huko.
Barabara nayo ni shida tupu. Ukitokea mbezi stand kuu kuelekea mpiji au njia panda ya Goba kwenda Mbezi Misumi na Msakuzi ukiwa na gari yako ni mwendo wa kurukaruka kwenye gari kutokana na mashimo makubwa ya barabarani hadi mwisho wa safari.
Hospitali jimbo zima hakuna. Ukiumwa inabidi uende hosipitali za binafsi au uende SINZA zaidi ya km30.
Nimetoka zangu mikoani kuja kumtembelea ndugu yangu lakini yamenishangaza sana maisha ya huku maana ni zaidi ya jehanamu.
Nimejiuliza maswali mengi, hivi wanaowasifu viongizi kama waziri wa maji, miundombinu na afya kwa watu wa jimbo la Kibamba wanawaelewa kweli?
Poleni sana wakazi wa Dar es salaamu. Serikali wasaidieni watu wa jimbo la kibamba wamechoka kusikia kila taarifa ya CAG kuwa Tanroad wamefisadi zaidi ya trillioni moja ambapo hiyo ingepelekwa huko ingemaliza changamoto za huko.
Yaani sehemu kubwa ya jimbo la kibamba hakuna maji. Wananchi wanavuna maji ya mvua inaponyesha na msimu wa masika ukipita kila mtu atajua kivyake atakapopata maji. Kama ni kufuata kimara au huko mbali yalikoishia maji ya dawasa. Dawasa wao hawana muda wa kupeleja maji huko.
Barabara nayo ni shida tupu. Ukitokea mbezi stand kuu kuelekea mpiji au njia panda ya Goba kwenda Mbezi Misumi na Msakuzi ukiwa na gari yako ni mwendo wa kurukaruka kwenye gari kutokana na mashimo makubwa ya barabarani hadi mwisho wa safari.
Hospitali jimbo zima hakuna. Ukiumwa inabidi uende hosipitali za binafsi au uende SINZA zaidi ya km30.
Nimetoka zangu mikoani kuja kumtembelea ndugu yangu lakini yamenishangaza sana maisha ya huku maana ni zaidi ya jehanamu.
Nimejiuliza maswali mengi, hivi wanaowasifu viongizi kama waziri wa maji, miundombinu na afya kwa watu wa jimbo la Kibamba wanawaelewa kweli?
Poleni sana wakazi wa Dar es salaamu. Serikali wasaidieni watu wa jimbo la kibamba wamechoka kusikia kila taarifa ya CAG kuwa Tanroad wamefisadi zaidi ya trillioni moja ambapo hiyo ingepelekwa huko ingemaliza changamoto za huko.