Maisha ya depo

Maisha ya depo

mHAMAS-shaji

Senior Member
Joined
May 31, 2024
Posts
114
Reaction score
359
SEASON-1

EPISODE 01

Ilikuwa ni siku ya furaha kwa kila mmoja wetu kwa kufika hatua hiyo ya kumaliza elimu ya upili baada ya kumaliza mitihani ya kidato cha sita.

Kilichobaki kwa wakati huo ilikuwa ni kuagana👋 kwa kila mmoja wetu kwani tulijua ya kuwa hakuna kitu kingine cha kutukutanisha kwa namba kubwa kama ile tena, ilikuwa ni huzuni😥 miongoni mwetu kwani ule undugu tuliokuwa nao ndani ya miaka miwili ndiyo ulikuwa unakoma wakati huo.

Kwa kulitambua hilo lilitolewa wazo la kukutana pamoja katika shule hiyo wakati wa kufuata vyeti vya kidato cha sita pale vitakapotolewa na wazo hilo liliungwa mkono na kila mmoja wetu.

Kipindi zikiendelea ratiba za kuagana kwa kupeana namba za simu na namna nyingine nilitizama saa🕖 na kugundua kuwa nina wastani wa masaa mawili na dakika zipatazo tano kabla tiketi iliyopo mikononi mwangu haijaisha muda wake.

Nilishugulisha kichwa changu kwa dakika moja nikagundua kuwa nikilaza damu hela💰 yangu nitakuwa nimemchangia mwarabu kijinga hivyo nikaona mambo yasiwe mengi mana kwetu ni pazuri na nilikwishapakumbuka.

Niliwatizama wahitimu wenzangu nikawaona bado wanaagana huku wengi wao wakiwa hawana tiketi kama mimi kwani mabasi ya kwenda kwao hayakuwepo mchana huo kutokana na umbali wa route yao uliokuwa ukiwahitaji masaa zaidi ya kumi hadi kufika makwao tofauti na kwetu ambako yalinitosha masaa sita pekee.

Kitu ambacho nilikuwa nikikisikia kwao walikuwa wakipanga kwenda kituo cha mabasi majira ya jioni kwa ajili ya kukata tiketi kwani hakukuwa na utaratibu wa shule kuandaa usafiri wa pamoja kwa wahitimu maana kulikuwa na mchanganyiko michepuo ya sayansi, sanaa na uchumi hali iliyopelekea kutomaliza kwa wakati sawa tofauti na wakati wa likizo za mihula ambapo wanafunzi wote humaliza mitihani kwa pamoja siku ya Ijumaa na kusafiri pamoja alfajiri ya Jumamosi.

Nikagundua hapo sina wa kuondoka naye hivyo niliiba muda wangu kidogo kwakuchukua namba za simu kama tatu ikiwemo ya dada mmoja mwenye urembo wake aliyefahamika kwa jina la Zainabu Khamis binafsi nilikuwa nikimwita Zaimisi.

Kulikuwepo na utaratibu wa kuchafuliana shati za shule kwa kuwa zilikwishakumaliza muda wa matumizi hivyo kila aliyeona shati la mwenzake likiwa safi ama likiwa na sehemu ya kuandika pasi nakuombwa alimsogelea na kuchukua kalamu ya kawaida ama makapeni🖍 na kuchora alichojisikia.

Lengo kubwa la kufanya hivyo ilikuwa ni kupeana namba za simu📱 kwani hakukuwa na mwenye simu ya kuhifadhi namba maana hatukuruhusiwa kuzimiliki kipindi cha masomo,📚📖 lakini mbali na hapo tulifanya hivyo kama sehemu ya kutunza kumbukumbu kwa wanadarasa kwani tuliandika namba za simu na majina yetu pamoja na kuweka saini zetu.

Kwa upande wangu sikuona umuhimu wa kuchafua shati la yeyote kwani sikuwa nikimiliki simu wala namba yake lakini pia muda ulikuwa ukiniendea matiti, hivyo basi pasi na kuaga mdogomdogo nilianza kujongea kuelekea lilipo bweni lililofahamika kwa jina la Mikumi.
Nikiwa nimepiga hatua kadhaa nilisikia sauti nyororo ikitamka “Hallow K baby”.

Waooh alikuwa ni mwanangu wa nguvu mwanadada Linda, msichana mwenye PCM yake ingawaje michepuo yetu ilikuwa ni kulia na kushoto lakini mara nyingi tulikuwa tukijisomea pamoja.
“Nambie mamdogo”,
nilimjibu huku nikimsubiri kwwani tayari alikuwa akipiga hatua kuupunguza umbali uliopo baina yetu.

“Mbona kama unajitenga mwanangu wapi unaelekea”,
aliendelea kuniuliza nami nikamjibu

“Oooh mummy so sorry, I do have a ticket to home on my hand and it is going to expire soon so nawahi kujiandaa mana I think kuna lisaa limoja na dakika chache kabla bus halijang’oa nanga”.

Maneno yale yalionekana kumhuzunisha Linda niligundua hilo kupitia uso wake naye akasema

“Mkaka una roho mbaya wewe yaani umekata tiketi hujaniambia haitoshi unaamua kuondoka kimyakimya bila kunijuza”.

Linda alinitupia shutuma hizo ambazo zilinifanya nijione mkatili mbele yake japo sikutaka kuonesha unyonge nikajitetea kwa kusema
“Jamani Linda ndo unapoteza kumbukumbu hivyo mbona nilikwambia tangu juzi kuwa nikimaliza mtihani wa mwisho sitoweza kulaza mbavu zangu hapa nikawanufaisha kunguni”.

Aliendelea kuniambia “Sawa ulisema na hiyo tiketi ulikata saa ngapi nisijue?”

Nikamjibu “Ni kweli sikukwambia ila tiketi yenyewe nimeipata leo asubuhi nilimuagiza jana jamaa wa dukani alipokwenda mjini kufungasha ndo leo kabla sijaingia kwenye mtihani nikaipitia kwahiyo jana ilikuwa vigumu kukwambia maana bado sikuwa na uhakika kama amepata au vinginevyo, samahani lakini mhandisi mama yangu mdogo kama nimekukwaza”.,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

EPISODE 02
Linda aliendelea kuhoji kwa kuniambia “Nakweli umenikwaza ila sawa tafanyaje tena, kwani huwezi ghairisha ukaondoka siku nyingine”.

Nami nikamjibu “Looh! Mamdogo nimeshakata tiketi now I can’t”,

Naye akanambia “I mean ughairishe mi ntakulipia iyo nauli siku nyingine, imagine unaondoka ntasoma na nani sasa kumaliza mitihani haimaanishi ndiyo uondoke na kutuacha kwenye mataa”.

Mwana PCM huyo alikuwa amebakiza mitihani kadhaa kwani wao walikuwa na mitihani mingi zaidi yetu ambapo tulikuwa na mitihani saba na wao walikuwa na mitihani tisa.

Niliweza kumshawishi na kuniruhusu kuondoka ila alinisisitiza nimuachie namba zangu za simu nilipomwambia sina kwa wakati huo alinipa namba yake ambayo aliiandika katika shati langu kwenye kifua.

Haikumtosha dada huyo alilitafuta shavu langu la kushoto na kuchora kitu ambacho sikuweza kugundua kwa urahisi ila nilihisi kama kuna kiduara.

Baada ya kuandikwa maneno hayo nilipewa sharti kuwa maandishi hayo yabaki mpaka pale nitakapofika kwetu na sikutakiwa kumuonesha mwanafunzi yeyote akanisomea kilichoandikwa na nikitekeleza hilo nitakuwa nimesamehewa kosa langu la kuondoka bila kuaga.

Nilitingisha kichwa nikiashiria kukubaliana naye lakini alinitaka niandike chochote kwenye shati lake mbali na namba ya simu, kabla ya kufanya hivyo nilimhoji ni kwanini alichafua shati hilo ilihali ya kuwa bado yuko na mitihani ya kufanya akanijibu kuwa anayo mawili.

Majibu yake yalinipa ruhusa ya kuandika, nikiwa natafuta sehemu ya kuandika bila kuchelewa Linda aliniambia

“Andika hapa nimepaacha kwa ajili yako” aliniambia huku akielekeza kidole kwenye mfuko wa shati.

Kwakweli alinipa kigugumizi maana mfuko wake ulikuwa karibu mno na chuchu ya ziwa lake la kushoto, huku nikiendelea kujiuliza Linda aliniambia.

“Kama unahisi hutaandika vizuri jaribu kupaweka sawa we pashike tu usiogope”.

Sikutaka kupoteza muda kwa kuweka majibizano zaidi na mwanadada yule hivyo nililivuta shati na kuandika “K-baby” wakati naandika nilipatwa na wakati mgumu mno mana eneo nililotakiwa niandike lilikuwa ni nyeti sana.

Nilijikaza na kulifanya hivyo kwa uharaka sana kwani nilikwisha ziona dalili za Linda kupandwa na hisia pindi nilipokuwa nikiandika.

Nilipokuwa nikiushusha mkono kuashiria kumaliza zoezi lile Linda alinikumbatia kwa haraka sana jambo ambalo sikutarajia litokee eneo la wazi lenye hadhira kama ile.

Kumbatio lile lilikuwa na maana kubwa mno kwake ambayo sikuweza kuielewa kwa wepesi, kwa wakati ule nilichukulia tu ni kama hisia za kuonana kwa mara ya mwisho kabla hatujaanza kuonana kwa kubahatisha.

Basi tukiwa katika kumbatio lile nilishtushwa na makofi yaliyokuwa yakipigwa na wanadarasa waliokuwa karibu na eneo lile, ikabidi tuachiane kutoka kwenye hali hiyo ambayo mimi na Linda tulikuwa kwenye dunia ya peke yetu.

Kila mtu aliongea alichojisikia huku wakisogea tulipo kana kwamba tuliwaita waje washuhudie jambo nasi hatukuwazuia wala kutaka kujitetea isipokuwa nilijiongeza na kuanza kuwakumbatia wanadarasa wengine huku nikiwaambia

” Ndugu zangu mi sikai hapa ndo naamsha hivyo tutaonana Mungu akipenda”.

Nilimtupia macho Linda naye nikamuona anafanya vilevile ila nikamsikia mnoko mmoja akisema

“Sawa mwanetu unatukumbatia vya mwisho mwisho ili uveshe home unasepa na Linda nini mana najua bado ana prac sasa na yeye anavyotuhagi vya mwisho mwisho mnakuwa mnanivuruga mjue”.

Ile anamaliza kusema vilianguka vicheko kama vyote kiasi cha kuwatoa kwenye mood ya kukumbatiana, basi nami nikautumia mwanya huohuo kuondoka eneo lile nikiwaacha na kucheka kwao.

Nilipofika bwenini wala sikuwa na mambo mengi mana kila kitu nilikwisha kiandaa nilijivutia zangu begi na kufungua zipu nikachomoa wallet, na kuikagua kama vitu vyangu muhimu bado vilikuwepo mana ingawaje kwenye bweni hilo tulikuwa tukiishi watu wa darasa moja lakini lilikuwa wazi muda mwingi mana si wanadarasa wote tulikuwa tukifanya mtihani mmoja kwani michepuo tulitofautiana.

Basi baada ya kujiridhisha na hali ya begi nilizipiga macho sehemu mbalimbali za ndani ya bweni lile kama ishara ya kulitazama kwa mara ya mwisho sehemu hiyo ambayo sasa itakua imebaki hadithi kwamba niliwahi kupaishi mahala hapo.

Nilipotosheka nilinyanyua begi na kuliweka begani zikawa zinahesabika sekunde tu kabla ya kuachana kabisa na maeneo ya shule ile, hatua mojamoja kutoka bwenini kuelekea nje ya shule ndicho kilifuata. ,,,,,,,,,,,


EPISODE 03

Niliwasiri kituo cha mabasi mnamo saa 7:52 na kama ulivyo utaratibu wa temino nyingine nilivamiwa na madalali wapatao wanne ambao kila mmoja alikuwa akinishawishi kuchagua kampuni ya mabasi aliyokuwa akiitumikia pasi na kujua ni wapi niendako.

Ilinichukua muda kuwapunguza mana hata nilipo wafahamisha kuwa nimekwishakata tiketi walishindwa kuniamini mpaka pale nilipoitwaa kutoka mfukoni mwangu na kuwaonesha nikaona mmojammoja anajipunguza na mmoja wao akanikabidhisha kwa wakala wa basi ambalo nimekata tiketi.

Nilifika nyumbani majira ya saa 2:33 nikawakuta wanafamilia wakinisubiri kwa hamu kwani walikuwa na shauku ya kuniona ikizingatiwa kuwa hapo kabla tulipokuwa tukiwasiliana walikuwa wakiniuliza siku ya kumaliza mtihani.

Lakini pia nikaja kugundua baadaye waliiwekea alama kwenye kalenda siku ile na waliandika mpaka muda wa kumaliza mtihani hivyo haikuwa kazi ngumu kwao kujua kuwa ningefika siku hiyo na hata hivyo niliwasiliana nao nilipokuwa safarini ambapo nilimuomba mmoja wa abiria tuliyepanda basi moja.

Nilisalimiana nao huku nikijitahidi kuuficha upande ule ulioandikwa na Linda mana sikuwa na imani yeyote kama alichokiandika kinastahili kuonekana na familia yangu.

Nilijifanya kama nasikia joto sana na uchovu ili nisikae nao kwa muda mrefu nikawapa nafasi ya kunikagua hivyo niliingia zangu chumbani na kubadili nguo kwa ajili ya kwenda kuoga.

Baada ya kujitazama kwenye kioo niligundua kuwa binti yule alinichora kijikopa ndani yake kilichoandikwa “Remember the name, lovely LINDA”.

Kwa kweli nilishukuru sana kwa akili niliyoipata ya kuuficha upande ule wa shavu maana tangu nipo safarini niliona ishara za abiria wenzangu kunitupia macho mara kwa mara.

Nilienda kuoga na baadaye nikaelekea mezani kula huku stori za hapa na pale zikiendelea mpaka majira ya saa tano za usiku nilipowaaga kwenda kulala.

Tayari nilikuwa na uchovu ambao ulinipelekea kusinzia na kwakua nilionekana kama msemaji mkuu usiku huo hata ile kasi ya masimulizi ilianza kupungua kwahiyo hakukuwa na namna zaidi ya kufunga kikao hicho.

Baada ya kupita siku tano tayari nilikwishapata kifaa cha mawasiliano ambacho hakikuwa na mbwembwe nyingi na mtaani kilifahamika kama kiswaswadu.

Kitu cha awali kabisa ilikuwa ni namba ya mwana wa Khamisi yaani Zainabu wa Mzee Khamisi classmate ambaye ningejutia sana ningekosa mawasiliano naye.

Kama kawaida nikaisave ZAIMISS, nilimtafuta kwa mara kadhaa nikaishia kujibiwa na yule mdada mwenye sauti nzuri akisema “Namba unayopiga haipatikani kwasasa tafadhali jaribu tena baadaye, mwachie ujumbe wa sauti voice mail baada ya mlio gharama za kawaida zitatozwa”.

Basi mwendo ukawa ni huohuo mpaka nikahisi dada yule atakuwa amenipa namba ya gari yaani namba ya mchongo ama ya uongo kama ifahamikavyo katika Kiswahili sahihi.

Kwa kipindi hicho nilikuwa nikiwasiliana sana na mwanangu mmoja afahamikaye kwa jina la Shabani ambaye yeye alisomea uchumi alikuwa simu kubwa iliyomuwezesha kupata taarifa nyingi kwa wakati mmoja na kufanya kazi zaidi ya moja mbali ya mawasiliano yaani smartphone.

Shebi alikuwa akinipa taarifa nyingi za wanadarasa na aliniambia kwa wakati huo bado baadhi ya wanadarasa hawajarudi haswa wale wa masomo ya Sayansi.

Bado kuna watu walikuwa na practical ya biology sijajua kama ni B au C lakini tayari kuna wanafunzi walishafanya Biology 3A yaani practical ya Biolojia mkupuo A.

Aliniambia kuwa kuna jamaa wa PCB ambaye ndiye anayelichangamsha group la whatsapp mpaka kufikia wakati huo alikuwa bado hajarudi ndipo nikahisi kuwa huenda hata huyu Zaimiss akawa bado hajarudi ndiyo mana simpati kwenye simu.

Usiku mmoja nikiwa kitandani nilipokea meseji kutoka kwenye namba ngeni “Hellow K” vyovyote nikajua atakuwa ni Linda.

Nilifikiria kwa muda nijibu kitu gani kifupi nilitamani nisijibu mana nilijua kutakuwa na mrundikano wa kesi za kujibu kwani aliniachia namba yake ya simu na wala sikuthubutu kumtafuta ingali yakuwa hapo kabla kisingizio ilikuwa ni kukosa simu na sasa ninayo.

Niliona ni bora nikamjibu kuliko kukaa kimya hali ambayo ingeniongezea namba ya maswali, basi nika reply “Waoooh mamdogo”.

Kilichofuata baada ya hapo niliona namba ileile kabla ya kuisave ikiita niliipokea na kuongea naye baada ya salamu hakuna kingine zaidi ya lawama kama nilivyokuwa nikifikiri kwani nilimfahamu vizuri mwanadada huyo kwa kulalamika.,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

EPISODE 04

Mlume nilijitetea kwa kumwambia kuwa

“Namba siioni na hata leo hii mchana nimejitahidi kufukunyua kwenye begi lakini wapi, hata hivyo ile siku natoka pale bweni la Mikumi mpaka napanda basi la kuja nyumbani ilikuwa ni shughuli Mamdogo. Nilipofika nyumbani begi lenyewe nilipokelewa nimekuja kulishika siku ya pili yaani kurupushani zilikuwa ni zaidi ya nyingi wala sijafanya kusudi kutokukutafuta”.

Baada ya maneno hayo nilisikia sauti ya Kichaga ikisema “Ewe Mungu wa majeshi embu shuka duniani uje umnusuru mtu wako huyu aliyejawa na damu ya uwongo kwenye mishipa yake, yaani anavyoongea ni kana kwamba ile namba nilimuandikia kwenye kikaratasi” kwakweli nilijichanganya hali iliyonifanya nibaki kimya na kumuacha aongee yeye tu.

Linda aliendelea kuongea na kuniuliza “umeshindwaje kuomba kwa mtu jamani, mbona wana wengi tu wanayo”.

Nikapata nguvu za kumjibu ila kwa sauti ya upole sana nikamwambia “Samahani sikuwa na wazo hilo ila nilikuwa naamini ninayo hivyo ipo siku ningeiona tu”.

Basi mazungumzo yalikuwa ni mengi ila kikubwa ilikuwa ni kwanini sikumtafuta siku zote hizo, kwakua nilikuwa nikimfahamu vizuri sikuhitajika kutumia nguvu nyingi kujitetea nilichofanya nilimtuliza nikampooza na hatimaye jazba likamshuka.

Nilijaribu kumdodosa Linda kama kuna watu bado hawajamaliza mitihani, aliniambia kuwa wamewaacha PCB na CBG wanasubiri practical ya Biology ila kesho yake ndiyo wanamalizia.

Maneno hayo yalinipa matumaini ya kwamba huenda Zai hakunipa namba ya uongo ila bado yuko shule na ndiyo maana hapatikani kwenye simu.

Nilitamani kumuuliza Linda kama kweli Zai naye ni miongoni mwa wale aliowaacha ila nikaona ni bora niache maana ataniona kama namjali Zai kuliko yeye kitu ambacho hakipendi na zaidi ya hapo ni kuwa tumetoka kumaliza swala kama hilo la kutomjali yeye.

Niliendelea kufanya juhudi za kumtafuta Zai pasi na mafanikio kwani hata pale nilipoulizia kama wamekwisharudi nyumbani wanafunzi wote waliomaliza kidato cha sita niliambiwa wamerudi ila kila nilipompigia msichana yule majibu yalikuwa ni yale yale “hapatikani”.

Siku moja nilipokuwa naongea na Shebi nilijaribu kumdodosa kuhusu Zainabu

“oya hivi Zainabu unaongea naye kweli”

“Zainabu yupi?”

“Zainabu Khamisi yule dada wa CBG tumemaliza naye pale kiskuli”

“Anhaah yule hapana nasikia kwenye simu hapatikani hata mimi kuna siku nilimpigia ila sikumpata, vipi kwani shemeji yetu nini”.

“Hapana ni mwana tu nimempigia sana ila naona kila nikipiga hapatikani nikaona nikuulize afisa habari huenda labda una namba nyingine au mnakutana kwenye group la class whatsapp siunajua sisi wengine tunamiliki viswaswadu”.

“Akipatikana au akijoin kwa group ntakustua ila kwa sasa sina mawasiliano naye, ila mbona kama unamsaka kwa udi na uvumba hivyo kwema kweli”.

“Duuh mwanangu Shebi mbona umenishikia shilingi hivyo wala hakuna shida yoyote ile nimekwambia ni mwana tu au kwa sababu ni wa kike ndo mana unanikabia kwa juu hivyo”.

“Basi usiwaze tukimpata tutakwambia sema ungetuweka wazi tujue kama amemaliza na kichanga chetu tumboni tuongeze juhudi maradufu ya kumtafuta”.

“Hamna mwanangu amini kwamba, ni mwana tu”

“Sawa nimukuelewa mwanangu nilikuwa nakuzingua tu kwani unafikiri hatujui kuwa umekufa kwa Linda”

“Linda tena?”

“Acha uhuni baba Linda kwahiyo unataka umkane Linda mbele yangu kuwa siyo demu wako?”

“Asa mi sindo nakupangilia yule mi mshikaji wangu tu tulikua tunapeana sapoti kwenye kusoma na vitu vidogovidogo ila swala la mahusiano na yeye kwakweli halipo”

“Aah we jamaa kwakukana umenishinda tabia wakati kila mtu pale class anajua juu ya uhusiano wenu Linda mwenyewe hata ukimpigia sasa hivi ukamuita mama K anafurahi kweli na anapenda kinoma ila wewe mwanangu sababu hayupo karibu na hawezi kutusikia ndo unajifanya kumkana siyo fair hivyo”.

“Siyo kwamba anafurahi ila anakucheka kwa maana hujui juu ya unachokisema ila ni mshikaji, ni mwana ni kampani ndo ilikuwa inatufanya tuwe karibu vile wala hakuna cha ziada”

“Sawa ngoja nimuunganishe kwenye simu afu umkane akisikia wewe siunajikuta Petro unaweza kukana watu kweupe”

“Oya Shebi kwani leo umekula nini mbona umeniamulia hivyo tatizo ni nini kwani"

“Tatizo ni kwamba unawakana wadada za watu kwasababu tu hawapo subiri nifanye mpango nimuunge akusikie”

“Kausha Shebi usimuunganishe bana usije kuniletea msala nishaichoka mimi”

“Umeona eeh hutaki kumbe kweli ni demu wako”.

Siku ziliendelea kusonga mithili ya maji yaliyopita kwenye mkondo wake, siku moja jamaa yangu mmoja aitwaye Ambrose alinitafuta kwenye simu na kunipa taarifa ya kuwa nimekuwa miongoni mwa wanafunzi waliochaguliwa na Jeshi la kujenga taifa kuhudhuria mafunzo ya kijeshi kama ilivyo sera ya elimu kwa wanafunzi wanaohitimu kidato cha sita nchini Tanzania. ,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

EPISODE 05

Binafsi haikuwa taarifa nzuri kwangu, sikuipokea siyo tu kwa mikono miwili bali hata kwa kidole kimoja sikuweza kuipokea taarifa ile hata kwa moyo mmoja.

Mpaka muda huo sikuwa nalipenda jeshi kwa ujumla, nilizisikia taarifa nyingi ambazo zilinifanya nilichukie jeshi.

Ugumu wa kazi na mazoezi yaliyopelekea ulemavu na vifo ni miongoni mwa mambo yaliyonifanya nikalichukia jeshi hilo.

Kwangu sikuhitaji kuwa maiti ndiyo nizijue mbivu na mbichi za kaburi, wala sikuhitaji niingie kati nicheze ndiyo niweze kuzijua raha za ngoma, fununu nilizozisikia mtaani zilinitosha kuhitimisha kuwa mafunzo ya jeshi ni njia ya kwenda kuzimu.

Kwakuwa Ambrose yeye alikuwa na simu ya kisasa alipata orodha ya baadhi ya wanadarasa waliochaguliwa kwenda mafunzoni.

Alinijuza miongoni mwao na kunifahamisha kuwa mimi, yeye na Linda ni miongoni mwa tuliopangiwa kushiriki mafunzo hayo kwenye kambi moja.

Nilijaribu kumuuliza kuhusu Zai naye kama kapangwa kambi sawa nasi ila aliniambia hakumuona kwenye orodha na nilipomuuliza kama anawasiliana naye majibu alinipa yaleyale ya kila siku kuwa namba aliyonayo haipatikani.

Basi bwana mrembo Zai aliendelea kuwa bidhaa adimu kwangu, hali iliyonizidishia hamu ya kutolipenda jeshi mana mbali ya kuwa nafsi iliamua kuwa sitohudhuria mafunzo ila ikitokea Zai akapangiwa kambi moja na mimi nisingesita kwenda hata kama ningekutana na kifo changu huko basi ningekuwa radhi kufa ili mradi nipate ukaribu naye mana niliamini kuwa bado ninahitaji muda wa kuwa karibu naye.

Taarifa zile ziliwafikia nyumbani ambako licha ya kujifanya sijui kinachoendelea huku nikisingizia uwezo wa simu niliyo nayo wao walitumia simu zao kufuatilia kwa undani kama nimepangiwa ama vinginevyo.

Walifanya hivyo mpaka pale walipofanikiwa kuliona jina langu na kunijuza nami sikusita kuwaambia msimamo wangu kuwa sipo tayari kwenda.

Msimamo huo ulizua mtafaruku nyumbani ingawaje wapo baadhi walitaka nisikilizwe ila shida ilikuwa kwa mkuu wa kaya ambaye yeye alitaka niende huko.

Baba mjengo huyo aliyekuwa akifahamika kwa jina la Mzee Mjuzi yeye aliamini kuwa mafunzo ya kijeshi yangenifanya niwe mkakamavu na mzalendo kwa taifa hivyo kuwa tayari wakati wowote kulitumikia taifa.

Alikuwa akiniambia kuwa serikali ina maana yake kufanya hivyo na siwezi jua mana huenda siku za mbele wale waliohudhuria mafunzo hayo wakawa ni kipaumbele kwa upande wa ajira.

Alinithibitishia hilo kwa kunipa mifano ya viongozi mbalimbali wa juu nchini wamehudhuria mafunzo ya kijeshi hivyo huenda ikawa kuna ngazi ya utawala ama uongozi wa nchi nisingeweza kuzihudumu pasi na kuwa na cheti ama historia ya kupitia mafunzo hayo kwasababu wanaamini hao watakuwa na uzalendo kwa taifa.

Mzee alinisisitiza kuwa siwezi jua mana wakati mwingine taasisi mbalimbali za kijeshi na usalama wa taifa hutumia Jeshi la kujenga taifa kupata watumishi wapya pengine ingeniangukia bahati na ikawa njia fupi kwangu ya kupata ajira ya kudumu.

Baada ya kikao hicho kikuu viliendelea vikao vidogodogo lengo likiwa ni kunisisitiza kufanya maandalizi mana siku za kuripoti zilikuwa zikikaribia.

Hakuna kauli ambazo ziliniumiza kutoka kwa mzee huyo pale aliponiambia nikienda jeshini nitakuwa mkakamavu na mzalendo.

Nafsini nilijiambia huenda nikawa siyo mzalendo kweli lakini je ameniona mimi ni legelege kiasi hicho kiasi cha kwenda kufanywa kuwa mkakamavu.

Nilichukia sana ila nilihitimisha kwa kujisemea moyoni kuwa mshua jau kauli ambayo ilinipunguza hasira juu ya kauli zake.

Wakati yote hayo yakiendelea nilikuwa nikiwasiliana na Linda ambaye yeye alifurahi mno kupangwa kambi moja na mimi na aliniambia kuwa hapo awali hakuwa tayari kwenda jeshini na wazazi wake waliriridhia.

Linda aliniambia kuwa kama itatokea niko tayari kwenda basi na yeye angekuwa tayari kuwaambia wazazi wake kuwa amebadili msimamo wake na hatimaye angekwenda.

Ama kweli penye miti hapana wajenzi yaani utayari wangu wa kwenda mafunzoni kwa ajili ya Zainabu hautofatiani na wa Linda kwangu ila ugumu uko hapo tu Linda yupo tayari kwenda kwa ajili yangu ila mimi sipo tayari kwenda kwaajili yake na kinyume chake niko tayari kwenda kwaajili ya Zainabu ingawaje sikufahamu utayari wa Zainabu kwangu.

Kifupi nilitamani sana Linda awe Zainabu ili jambo liwe jepesi.

Kadri siku zilivyokuwa zikiongeza namba ndivyo maudhi yalikuwa yakizidi maana kikubwa ilikuwa ni ukakamavu, nidhamu na uzalendo kana kwamba ni vitu ambavyo sina.

Niliamua kukaa chini na kufanya tafakuri ya kina nikaona nikiendelea kukaa humo nitakuwa nikigombana na watu wasiostahili kila siku mana hata wale waliokuwa wakiniunga mkono walinisihi sana kumsikiliza mshua kwa maana kuwa kumpinga yeye ni sawa na kumdharau. ,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

EPISODE 06

Nikiwa natafuta suluhisho juu ya hilo niliwaza baadhi ya vitu haswa juu ya nadharia ya kuwa kuhudhuria mafunzo ya jeshi ni njia ya kwenda kuzimu.

Nilijiambia kama kweli ni njia ya kuzimu je, ina maana wanajeshi wote wameajiriwa wakitokea wapi? kuzimu au makaburini? nikaona hapana hakuna ukweli katika hilo.

Lakini pia nikaona namba kubwa ya wanadarasa tuliochaguliwakambi moja walikuwa na utayari wa kuhudhuria mafunzo hivyo suluhisho la zile dhihaka, dharau na maugomvi ya kila siku ni kwenda jeshini.

Mtu wa kwanza kumjuza hili alikuwa ni swahiba wangu Linda ambaye alionekana kufurahi zaidi. Aliniambia alikwisha wabadili mawazo wazazi wake mara baada ya kujua kuwa tumepangwa kambi moja akijua ya kwamba nami nisingekataa hivyo alisubiri muda tu ufike.

Sikumwambia juu ya kilichokuwa kinaendelea nyumbani ila niliamua kumpongeza kwa ushawishi wake ili aone kama niko pamoja naye na mwenye thamani kwangu.

Kazi kubwa ilikuwa ni namna ya kuwajuza nyumbani kuwa nimebadili msimamo na niko tayari kwenda jeshini.

Basi nikiwa natafuta namna ambayo nitawaambia ilifika ile siku ya wanafunzi kuripoti kwenye kambi walizopangiwa.

Siku hiyo asubuhi yake nilijichelewesha kuamka makusudi nikijua kwamba kwa namna yoyote ile Mzee Mjuzi lazima angenigombeza hukuakilitilia mkazo swala la kwenda jeshini.

Mzee Mjuzi ana kawaida ya kuja mpaka vyumbani kutuamsha pale anapoamka na kugundua bado tumelala hivyo nilijua kuwa angekuja tu.

Kwakuwa kilikuwa ni kipindi cha likizo nyumba ilikuwa na utajiri wa watoto ambao walikuwa wanasaidia kazi ndogondogo za nyumbani kama vile kufagia, kudeki kuosha vyombo n.k.

Kwa mbali nilisikia sauti ya mshua ikinena “embu niamshieni huyo mtoto wa mfalme anayelala kama yupo kwenye kasri la Malikia Elizabeth”.

Niliposikia nikajisemea moyoni “Kumekucha kumekucha” mshua alikuwa haishiwi na maneno ya kejeli na maudhi nilijitahisdi kumzoea ila ilikua ni vigumu kumzoea ila niliweza kuzivumilia tu.

Alikuja kuniamsha mdogo wangu aitwaye Amiri na kunijuza kuwa baba mwenye nyumba kasema niamke, nilimtingishia kichwa kuashiria kuwa nimeelewa. Zilinichukua dakika kama kumi kutoka mule ndani nikiwa na mswaki mkononi nikifuata dawa ya meno iliyokuwa jikoni.

Nilimuona mshua akiangalia uchambuzi wa habari kwenye televisheni iliyopo sebuleni ambako ndiko iliko dawa ya meno.

Niliamua kupita jikoni kwanza ili nikiweka dawa nitoke nje moja kwa moja ingawaje niliweza kufanya kinyume chake yaani nianze kuweka dawa alafu nifuate maji jikoni na kutokea mlango wa jikoni ila kwa kuwa lengo lango ni kumchangamsha mzee baba nikaamua nitokee mlango wa mbele.

Nilipofika sebuleni nilimsalimia baba aliyeitika na kunitaka nisogee kule aliko niliweka dawa na kumfuata nilipofika tu nilianza kusomewa mashitaka.

“Naona siku hizi umeshaota mapembe unaamka muda unaotaka husaidii kazi unachoweza wewe kula, kulala na kuzurura tu. Namtuma mdogo wako akuite bado unakuja kwa kujisikia umekua siku hizi siyo? au unaona hatuna cha kukufanya, humuogopi yeyote? Sawa Sasa nataka uniambie vyenye kueleweka utaenda jeshini au unataka kubaki hapa na kuishi kifalme kama utakavyo".

"Na kwa mfumo huo uutakao kwangu hapana labda uende kwa bibi yako nasikia ameanza kuvuna nafikiri huko ndiko kunako kufaa”.

Naam kifupi mshua alitema nyongo na povu lilimtoka haswa, tulikaa kikao kwa muda na nilimweleza kwamba niko tayari kwenda ingawaje sijapenda ila nitaenda kwasababu ametaka.

Alionekana kufurahi na akaniambia nijiandae mchana niende mjini nikanunue vifaa vinavyohitajika jeshini likiwemo shuka za rangi ya samawati, pea ya viatu na tisheti ya rangi ya kijani sambamba na kaptula ya rangi ya buluu ya kuiva, sanduku la chuma (tranker), truck suit n.k.

Mzee Mjuzi aliniachia kiasi cha pesa ambapo mchana wake nilikwenda mjini kutafuta vitu hivyo. Vitu vilionekana kuwa adimu sokoni na hata vilipopatikana vilikuwa bei juu yaani wafanyabiashara hawajawahiiacha fursa yeyote ile iwapite.

Nilirudi nyumbani nikiwa nimefanikiwa kupata shuka na viatu vya kijani ya mchongo yaani nilijitwalia zangu viatu vyenye doa la kijanimaana nilizurura vya kutosha mpaka jua likaanza kuzama.

Asubuhi yake ilikuwa ni siku ya mnada kwenye moja gulio karibu na nyumbani. Niliongozana na mzee aliyekuwa anahisi nimekosa vitu hivyo kwa makusudi kwakuwa sikuwa na nia ya kwenda kujibizana naye kwasababu hakuwepo hivyo nilimwacha akajionee.

Tulifika gulioni na kilichotokea ilikuwa ni kivumbi na jasho yaani vitu vilikuwa adimu na vilivyopatikana vilipatikana kwa bei iliyochangamka.,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

EPISODE 07

Tulirudi nyumbani mchana tukiwa tumechoka sana, nilitakiwa kuondoka siku hiyo mchana lakini ilibidi tughairishe.

Tulipata baadhi ya vitu na vingine tuliambiwa kuwa tunaweza vipata kulekule jeshini.

Basi siku ya pili ilikatika na angalau ilimalizika vizuri ukilinganisha na siku za nyuma tangu itoke orodha ya majina kujiunga JKT.

Usiku nilifanya maandalizi ya mwisho na kiliandaliwa chakula maalum kwa ajili ya kuagwa kifupi ulikuwa ni usiku mzuri ukiachilia mbali na mapochopocho yaliyokuwa mezani bali ni furaha ya kila mmoja wetu japo furaha yangu ilikuwa ni ya kuigiza.

Safari ilianza mapema tu kulipokucha niliwaaga nyumbani na kuongozana na mshua mpaka kilipo kituao cha mabasi ya mkoa.

Alinikatia tiketi na kunichia pesa ya kujikimu na safari ilianza mnamo saa 1:30 asubuhi yaani mzee ilibidi ahakikishe basi linaondoka maana nafikiri alihisi ningeweza kubadili ruti na kwenda sehemu nyingine.

Safari ilikuwa ni ndefu kwa upande wangu kwani ukiachilia mbali na kuchukua muda mrefu njiani lakini pia nilikuwa na mawazo mengi juu ya dhana zilizojengeka mtaani kuhusiana na mafunzo ya kijeshi.

Safari ilifika ukomo mnamo saa tisa ya alasiri ambapo tuliwasili kituo cha mabasi, tuliteremka kutoka kwenye basi na kila mmoja kuendelea na ustaarabu wake.

Kwakuwa nilikuwa na ugeni mwingi eneo hilo ilinibidi niulizie kwa wapiga debe unakopatikana usafiri wa kuelekea iliko kambi.

Nilijuzwa kuwa ni mwendo wa saa moja mpaka kufika eneo husika na usafiri upo mpaka mishale ya saa mbili za usiku.

Kwa maelezo hayo tayari nilikuwa na uhakika wa kuendelea kubaki mtaani kwa muda na kufanya niliyobakiza kabla sijaenda kujitupa kwa makamanda hata hivyo sikupenda kufika mapema niliona ni vyema nikajichelewesha kidogo.

Niliacha sanduku langu kwa moja ya ofisi ya ajenti wa kampuni ya mabasi na kutoka nje ambako nilipata wasaa wa kwenda nyumba ya ibada kumuomba Mwenyezi Mungu anijalie safari njema katika maisha ambayo sikuwahi kufikiria kuja kuyapitia na hakika nilipofika huko nilikaa kitako haswa.

Nilipomaliza nilipita saluni ambako nilikwenda kutoa nywele kichwani kuendana na mazingira ya kule niendako yaani nilienda kuangusha dongo kichwani.

Kinyozi hakuwa akiniamini nilipomwambia kuwa aninyoe para ila baadaye alinielewa alipogundua kuwa naelekea jeshini.

Nilipomaliza nilitoka na kuelekea sehemu moja ambayo watu walikuwa wakipooza nafsi zao na kumwagilia mioyo.

Niliagiza kinywaji kimoja laini ambacho hakikuwa na shida kushuka kwenye kolomeo langu yaani soda.

Niliinywa soda hiyo kwa mafungu huku nikijiuliza hivi ni kweli naenda jeshini? Ni kwa matakwa yangu mwenyewe au kuna mtu kanishikia akili? Je, itakuwaje mwisho wa siku nitarudi nikiwa hai kweli au ndo naenda kukabidhisha roho kwa malaika wavaa kombati? Maswali yalikuwa ni mengi kiasi kwamba nilikosa majibu sahihi ila lilikuja hitimisho kuwa liwalo na liwe acha niende nikirudi salama Alhamdulillah na ikitokea tofauti Familillah.

Basi nilipomaliza hapo nikaongoza kituo cha mabasi ambako yule ajenti alimuita bodaboda aliyenipeleka moja kwa moja kilipo kituo kidogo cha magari yanayoelekea kambini.

Safari iliwadia na mnamo majira ya saa kumi na moja tulifika na kushuka watu kadhaa pale kituoni.

Nilijikokota na kukaa kwenye banda la chipsi lililokuwepo eneo hilo, nilikaa kwa muda nikitafakari juu ya safari niliyokuwa nikiiendea mana ilionekana kama bado akili haijakubaliana na ninachokifanya.

Halmashauri ya kichwa ilifika hatua ikaniambia “mpaka hapa ulipofika ni hatua nyingi umeziendea huwezi kurudi nyuma malizia hizi chache ulizobakiza”.

Nafsi nayo haikusita kunena na moyo ukauambia “Hapa ndiyo bagamoyo rafiki yangu, sehemu ambayo watu kutoka bara walifika na kuibwaga mioyo yao pindi ambapo walipokutana na ngalawa zilizokuwa zikiwasubiri pwani ya Afrika mashariki zama za utumwa”.

Naam huo ndiyo ukweli niliotakiwa kuupokea kwa wakati huo ilibidi nami niubwage moyo wangu pale stendi ambapo mbele yangu niliona watu waliovaa sare wakielekea njia moja ambapo niliamini wanakwenda kambini.

Nikiwa najishauri kuondoka alitokea jamaa mmoja na kuniambia.

“Oya niaje”

“Fresh, nambie” nikamjibu

“Kama kawa si unaelekea JKT”

“Ndio vipi kwani”

“Hamna nakustua tu twende wote mi mwenyewe naelekea hukohuko”

“Basi poa twenzao”. ,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

Itaendelea...........................

Mwisho wa Msimu wa kwaza wa simulizi ya MAISHA YA DEPO, tukutane msimu wa pili

LogoMakerCa-1736810083860_1.jpg
 
SEASON-1

EPISODE 02

Linda aliendelea kuhoji kwa kuniambia
“Nakweli umenikwaza haswa ila sawa tafanyaje tena, kwani huwezi ghairisha ukaondoka siku nyingine”.

Nami nikamjibu “Looh! Mamdogo nimeshakata tiketi I can’t for now” naye akanambia
“Imean ughairishe mi ntakulipia iyo nauli siku nyingine, imagine unaondoka ntasoma na nani sasa au unataka nifeli uende chuo pekeako, kumaliza mitihani haimaanishi ndiyo uondoke na kutuacha kwenye mataa”.

Mwana PCM huyo alikuwa amebakiza mitihani kadhaa kwani wao walikuwa na mitihani mingi zaidi yetu tuliokuwa na mitihani saba wao walikuwa na mitihani tisa.

Nilimshawishi na hatimaye aliniruhusu kuondoka ila alinisisitiza nimuachie namba zangu za simu nilipomwambia sina alinivuta shati na kuniandikia yake kwenye kifua.

Haikumtosha dada huyo alilitafuta shavu langu la kushoto na kuchora kitu ambacho sikuweza kugundua kwa urahisi ila nilihisi kama kuna kiduara kilichorwa kikifuatwa na maneno ambayo nayo sikuyatambua kwa urahisi.

Baada ya kuandikwa maneno hayo nilipewa sharti kuwa maandishi hayo yabaki mpaka pale nitakapofika kwetu na sikutakiwa kumuonesha mwanafunzi yeyote akanisomea kilichoandikwa na nikitekeleza hilo nitakuwa nimesamehewa kosa langu la kuondoka bila kuaga
.
Nilitingisha kichwa nikiashiria kukubaliana naye lakini alinitaka niandike chochote kwenye shati lake mbali na namba ya simu.

Kabla ya kufanya hivyo nilimhoji ni kwanini alichafua shati hilo ilihali ya kuwa bado yuko na mitihani ya kufanya akanijibu kuwa anayo mawili.

Majibu yake yalinipa ruhusa ya kuandika, nikiwa natafuta sehemu ya kuandika bila kuchelewa Linda aliniambia
“Andika hapa nimepaacha kwa ajili yako” aliniambia huku akielekeza kidole kwenye mfuko wa shati.Kwakweli alinipa kigugumizi maana mfuko wake ulikuwa karibu mno na chuchu ya ziwa lake la kushoto.

Huku nikiendelea kujiuliza Linda aliniambia
“Kama unahisi hutaandika vizuri jaribu kupaweka sawa we pashike tu usiogope”.

Sikutaka kupoteza muda kwa kuweka majibizano zaidi na mwanadada yule hivyo nililivuta shati na kuandika “K-baby” wakati naandika nilipatwa na wakati mgumu mno mana eneo nililotakiwa niandike lilikuwa ni nyeti sana.

Nilijikaza na kulifanya hivyo kwa uharaka sana kwani nilikwisha ziona dalili za Linda kupandwa na hisia pindi nilipokuwa nikiandika.Nilipokuwa nikiushusha mkono kuashiria kumaliza zoezi lile Linda alinikumbatia kwa haraka sana jambo ambalo sikutarajia litokee eneo la wazi lenye hadhira kama ile.

Kumbatio lile lilikuwa na maana kubwa mno kwake ambayo sikuweza kuielewa kwa wepesi, kwa wakati ule nilichukulia tu ni kama hisia za kuonana kwa mara ya mwisho kabla hatujaanza kuonana kwa kubahatisha.

Basi tukiwa katika kumbatio lile nilishtushwa na makofi yaliyokuwa yakipigwa na wanadarasa waliokuwa karibu na eneo lile, ikabidi tuachiane kutoka kwenye hali hiyo ambayo mimi na Linda tulikuwa kwenye dunia ya peke yetu.

Kila mtu aliongea alichojisikia huku wakisogea tulipo kana kwamba tuliwaita waje washuhudie jambo nasi hatukuwazuia wala kutaka kujitetea isipokuwa nilijiongeza na kuanza kuwakumbatia wanadarasa wengine huku nikiwaambia
” Ndugu zangu mi sikai hapa ndo naamsha hivyo tutaonana Mungu akipenda”.

Nilimtupia macho Linda naye nikamuona anafanya vilevile ila nikamsikia mnoko mmoja akisema
“Sawa mwanetu unatukumbatia vya mwisho mwisho ili uveshe home unasepa na Linda nini mana najua bado ana prac sasa na yeye anavyotuhagi vya mwisho mwisho mnakuwa mnanivuruga mjue”.

Ile anamaliza kusema vilianguka vicheko kama vyote kiasi cha kuwatoa kwenye mood ya kukumbatiana, basi nami nikautumia mwanya huohuo kuondoka eneo lile nikiwaacha na kucheka kwao.

Nilipofika bwenini wala sikuwa na mambo mengi mana kila kitu nilikwisha kiandaa nilijivutia zangu begi na kufungua zipu nikachomoa wallet.

Niliikagua kama vitu vyangu muhimu bado vilikuwepo mana ingawaje kwenye bweni hilo tulikuwa tukiishi watu wa darasa moja lakini lilikuwa wazi muda mwingi mana si wanadarasa wote tulikuwa tukifanya mtihani mmoja kwani michepuo tulitofautiana.

Basi baada ya kujiridhisha na hali ya begi nilizipiga macho sehemu mbalimbali za ndani ya bweni lile kama ishara ya kulitazama kwa mara ya mwisho sehemu hiyo ambayo sasa itakua imebaki hadithi kwamba niliwahi kupaishi mahala hapo.

Nilipotosheka nilinyanyua begi na kuliweka begani zikawa zinahesabika sekunde tu kabla ya kuachana kabisa na maeneo ya shule ile, hatua mojamoja kutoka bwenini kuelekea nje ya shule ndicho kilifuata.,,,,,,,,,,,,

Itaendelea…………...
 
SEASON-1

EPISODE 01

Ilikuwa ni siku ya furaha kwa kila mmoja wetu kwa kufika hatua hiyo ya kumaliza elimu ya upili baada ya kumaliza mitihani ya kidato cha sita.

Kilichobaki kwa wakati huo ilikuwa ni kuagana👋 kwa kila mmoja wetu kwani tulijua ya kuwa hakuna kitu kingine cha kutukutanisha kwa namba kubwa kama ile tena, ilikuwa ni huzuni😥 miongoni mwetu kwani ule undugu tuliokuwa nao ndani ya miaka miwili ndiyo ulikuwa unakoma wakati huo.

Kwa kulitambua hilo lilitolewa wazo la kukutana pamoja katika shule hiyo wakati wa kufuata vyeti vya kidato cha sita pale vitakapotolewa na wazo hilo liliungwa mkono na kila mmoja wetu.

Kipindi zikiendelea ratiba za kuagana kwa kupeana namba za simu na namna nyingine nilitizama saa🕖 na kugundua kuwa nina wastani wa masaa mawili na dakika zipatazo tano kabla tiketi iliyopo mikononi mwangu haijaisha muda wake.

Nilishugulisha kichwa changu kwa dakika moja nikagundua kuwa nikilaza damu hela💰 yangu nitakuwa nimemchangia mwarabu kijinga hivyo nikaona mambo yasiwe mengi mana kwetu ni pazuri na nilikwishapakumbuka.

Niliwatizama wahitimu wenzangu nikawaona bado wanaagana huku wengi wao wakiwa hawana tiketi kama mimi kwani mabasi ya kwenda kwao hayakuwepo mchana huo kutokana na umbali wa route yao uliokuwa ukiwahitaji masaa zaidi ya kumi hadi kufika makwao tofauti na kwetu ambako yalinitosha masaa sita pekee.

Kitu ambacho nilikuwa nikikisikia kwao walikuwa wakipanga kwenda kituo cha mabasi majira ya jioni kwa ajili ya kukata tiketi kwani hakukuwa na utaratibu wa shule kuandaa usafiri wa pamoja kwa wahitimu maana kulikuwa na mchanganyiko michepuo ya sayansi, sanaa na uchumi hali iliyopelekea kutomaliza kwa wakati sawa tofauti na wakati wa likizo za mihula ambapo wanafunzi wote humaliza mitihani kwa pamoja siku ya Ijumaa na kusafiri pamoja alfajiri ya Jumamosi.

Nikagundua hapo sina wa kuondoka naye hivyo niliiba muda wangu kidogo kwakuchukua namba za simu kama tatu ikiwemo ya dada mmoja mwenye urembo wake aliyefahamika kwa jina la Zainabu Khamis binafsi nilikuwa nikimwita Zaimisi.

Kulikuwepo na utaratibu wa kuchafuliana shati za shule kwa kuwa zilikwishakumaliza muda wa matumizi hivyo kila aliyeona shati la mwenzake likiwa safi ama likiwa na sehemu ya kuandika pasi nakuombwa alimsogelea na kuchukua kalamu ya kawaida ama makapeni🖍 na kuchora alichojisikia.

Lengo kubwa la kufanya hivyo ilikuwa ni kupeana namba za simu📱 kwani hakukuwa na mwenye simu ya kuhifadhi namba maana hatukuruhusiwa kuzimiliki kipindi cha masomo,📚📖 lakini mbali na hapo tulifanya hivyo kama sehemu ya kutunza kumbukumbu kwa wanadarasa kwani tuliandika namba za simu na majina yetu pamoja na kuweka saini zetu.

Kwa upande wangu sikuona umuhimu wa kuchafua shati la yeyote kwani sikuwa nikimiliki simu wala namba yake lakini pia muda ulikuwa ukiniendea matiti, hivyo basi pasi na kuaga mdogomdogo nilianza kujongea kuelekea lilipo bweni lililofahamika kwa jina la Mikumi.
Nikiwa nimepiga hatua kadhaa nilisikia sauti nyororo ikitamka “Hallow K baby”.

Waooh alikuwa ni mwanangu wa nguvu mwanadada Linda, msichana mwenye PCM yake ingawaje michepuo yetu ilikuwa ni kulia na kushoto lakini mara nyingi tulikuwa tukijisomea pamoja.
“Nambie mamdogo”,
nilimjibu huku nikimsubiri kwwani tayari alikuwa akipiga hatua kuupunguza umbali uliopo baina yetu.

“Mbona kama unajitenga mwanangu wapi unaelekea”,
aliendelea kuniuliza nami nikamjibu

“Oooh mummy so sorry, I do have a ticket to home on my hand and it is going to expire soon so nawahi kujiandaa mana I think kuna lisaa limoja na dakika chache kabla bus halijang’oa nanga”.

Maneno yale yalionekana kumhuzunisha Linda niligundua hilo kupitia uso wake naye akasema

“Mkaka una roho mbaya wewe yaani umekata tiketi hujaniambia haitoshi unaamua kuondoka kimyakimya bila kunijuza”.

Linda alinitupia shutuma hizo ambazo zilinifanya nijione mkatili mbele yake japo sikutaka kuonesha unyonge nikajitetea kwa kusema
“Jamani Linda ndo unapoteza kumbukumbu hivyo mbona nilikwambia tangu juzi kuwa nikimaliza mtihani wa mwisho sitoweza kulaza mbavu zangu hapa nikawanufaisha kunguni”.

Aliendelea kuniambia “Sawa ulisema na hiyo tiketi ulikata saa ngapi nisijue?”

Nikamjibu “Ni kweli sikukwambia ila tiketi yenyewe nimeipata leo asubuhi nilimuagiza jana jamaa wa dukani alipokwenda mjini kufungasha ndo leo kabla sijaingia kwenye mtihani nikaipitia kwahiyo jana ilikuwa vigumu kukwambia maana bado sikuwa na uhakika kama amepata au vinginevyo, samahani lakini mhandisi mama yangu mdogo kama nimekukwaza”.,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

Itaendelea...........................View attachment 3202479
Ulevi wangu huu 😜😜😜Vistory stori 😍😍
 
SEASON-1

EPISODE 01

Ilikuwa ni siku ya furaha kwa kila mmoja wetu kwa kufika hatua hiyo ya kumaliza elimu ya upili baada ya kumaliza mitihani ya kidato cha sita.

Kilichobaki kwa wakati huo ilikuwa ni kuagana👋 kwa kila mmoja wetu kwani tulijua ya kuwa hakuna kitu kingine cha kutukutanisha kwa namba kubwa kama ile tena, ilikuwa ni huzuni😥 miongoni mwetu kwani ule undugu tuliokuwa nao ndani ya miaka miwili ndiyo ulikuwa unakoma wakati huo.

Kwa kulitambua hilo lilitolewa wazo la kukutana pamoja katika shule hiyo wakati wa kufuata vyeti vya kidato cha sita pale vitakapotolewa na wazo hilo liliungwa mkono na kila mmoja wetu.

Kipindi zikiendelea ratiba za kuagana kwa kupeana namba za simu na namna nyingine nilitizama saa🕖 na kugundua kuwa nina wastani wa masaa mawili na dakika zipatazo tano kabla tiketi iliyopo mikononi mwangu haijaisha muda wake.

Nilishugulisha kichwa changu kwa dakika moja nikagundua kuwa nikilaza damu hela💰 yangu nitakuwa nimemchangia mwarabu kijinga hivyo nikaona mambo yasiwe mengi mana kwetu ni pazuri na nilikwishapakumbuka.

Niliwatizama wahitimu wenzangu nikawaona bado wanaagana huku wengi wao wakiwa hawana tiketi kama mimi kwani mabasi ya kwenda kwao hayakuwepo mchana huo kutokana na umbali wa route yao uliokuwa ukiwahitaji masaa zaidi ya kumi hadi kufika makwao tofauti na kwetu ambako yalinitosha masaa sita pekee.

Kitu ambacho nilikuwa nikikisikia kwao walikuwa wakipanga kwenda kituo cha mabasi majira ya jioni kwa ajili ya kukata tiketi kwani hakukuwa na utaratibu wa shule kuandaa usafiri wa pamoja kwa wahitimu maana kulikuwa na mchanganyiko michepuo ya sayansi, sanaa na uchumi hali iliyopelekea kutomaliza kwa wakati sawa tofauti na wakati wa likizo za mihula ambapo wanafunzi wote humaliza mitihani kwa pamoja siku ya Ijumaa na kusafiri pamoja alfajiri ya Jumamosi.

Nikagundua hapo sina wa kuondoka naye hivyo niliiba muda wangu kidogo kwakuchukua namba za simu kama tatu ikiwemo ya dada mmoja mwenye urembo wake aliyefahamika kwa jina la Zainabu Khamis binafsi nilikuwa nikimwita Zaimisi.

Kulikuwepo na utaratibu wa kuchafuliana shati za shule kwa kuwa zilikwishakumaliza muda wa matumizi hivyo kila aliyeona shati la mwenzake likiwa safi ama likiwa na sehemu ya kuandika pasi nakuombwa alimsogelea na kuchukua kalamu ya kawaida ama makapeni🖍 na kuchora alichojisikia.

Lengo kubwa la kufanya hivyo ilikuwa ni kupeana namba za simu📱 kwani hakukuwa na mwenye simu ya kuhifadhi namba maana hatukuruhusiwa kuzimiliki kipindi cha masomo,📚📖 lakini mbali na hapo tulifanya hivyo kama sehemu ya kutunza kumbukumbu kwa wanadarasa kwani tuliandika namba za simu na majina yetu pamoja na kuweka saini zetu.

Kwa upande wangu sikuona umuhimu wa kuchafua shati la yeyote kwani sikuwa nikimiliki simu wala namba yake lakini pia muda ulikuwa ukiniendea matiti, hivyo basi pasi na kuaga mdogomdogo nilianza kujongea kuelekea lilipo bweni lililofahamika kwa jina la Mikumi.
Nikiwa nimepiga hatua kadhaa nilisikia sauti nyororo ikitamka “Hallow K baby”.

Waooh alikuwa ni mwanangu wa nguvu mwanadada Linda, msichana mwenye PCM yake ingawaje michepuo yetu ilikuwa ni kulia na kushoto lakini mara nyingi tulikuwa tukijisomea pamoja.
“Nambie mamdogo”,
nilimjibu huku nikimsubiri kwwani tayari alikuwa akipiga hatua kuupunguza umbali uliopo baina yetu.

“Mbona kama unajitenga mwanangu wapi unaelekea”,
aliendelea kuniuliza nami nikamjibu

“Oooh mummy so sorry, I do have a ticket to home on my hand and it is going to expire soon so nawahi kujiandaa mana I think kuna lisaa limoja na dakika chache kabla bus halijang’oa nanga”.

Maneno yale yalionekana kumhuzunisha Linda niligundua hilo kupitia uso wake naye akasema

“Mkaka una roho mbaya wewe yaani umekata tiketi hujaniambia haitoshi unaamua kuondoka kimyakimya bila kunijuza”.

Linda alinitupia shutuma hizo ambazo zilinifanya nijione mkatili mbele yake japo sikutaka kuonesha unyonge nikajitetea kwa kusema
“Jamani Linda ndo unapoteza kumbukumbu hivyo mbona nilikwambia tangu juzi kuwa nikimaliza mtihani wa mwisho sitoweza kulaza mbavu zangu hapa nikawanufaisha kunguni”.

Aliendelea kuniambia “Sawa ulisema na hiyo tiketi ulikata saa ngapi nisijue?”

Nikamjibu “Ni kweli sikukwambia ila tiketi yenyewe nimeipata leo asubuhi nilimuagiza jana jamaa wa dukani alipokwenda mjini kufungasha ndo leo kabla sijaingia kwenye mtihani nikaipitia kwahiyo jana ilikuwa vigumu kukwambia maana bado sikuwa na uhakika kama amepata au vinginevyo, samahani lakini mhandisi mama yangu mdogo kama nimekukwaza”.,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

Itaendelea...........................View attachment 3202479
Leejay49 njoo chapu
 
SEASON-1

EPISODE 02

Linda aliendelea kuhoji kwa kuniambia
“Nakweli umenikwaza haswa ila sawa tafanyaje tena, kwani huwezi ghairisha ukaondoka siku nyingine”.

Nami nikamjibu “Looh! Mamdogo nimeshakata tiketi I can’t for now” naye akanambia
“Imean ughairishe mi ntakulipia iyo nauli siku nyingine, imagine unaondoka ntasoma na nani sasa au unataka nifeli uende chuo pekeako, kumaliza mitihani haimaanishi ndiyo uondoke na kutuacha kwenye mataa”.

Mwana PCM huyo alikuwa amebakiza mitihani kadhaa kwani wao walikuwa na mitihani mingi zaidi yetu tuliokuwa na mitihani saba wao walikuwa na mitihani tisa.

Nilimshawishi na hatimaye aliniruhusu kuondoka ila alinisisitiza nimuachie namba zangu za simu nilipomwambia sina alinivuta shati na kuniandikia yake kwenye kifua.

Haikumtosha dada huyo alilitafuta shavu langu la kushoto na kuchora kitu ambacho sikuweza kugundua kwa urahisi ila nilihisi kama kuna kiduara kilichorwa kikifuatwa na maneno ambayo nayo sikuyatambua kwa urahisi.

Baada ya kuandikwa maneno hayo nilipewa sharti kuwa maandishi hayo yabaki mpaka pale nitakapofika kwetu na sikutakiwa kumuonesha mwanafunzi yeyote akanisomea kilichoandikwa na nikitekeleza hilo nitakuwa nimesamehewa kosa langu la kuondoka bila kuaga
.
Nilitingisha kichwa nikiashiria kukubaliana naye lakini alinitaka niandike chochote kwenye shati lake mbali na namba ya simu.

Kabla ya kufanya hivyo nilimhoji ni kwanini alichafua shati hilo ilihali ya kuwa bado yuko na mitihani ya kufanya akanijibu kuwa anayo mawili.

Majibu yake yalinipa ruhusa ya kuandika, nikiwa natafuta sehemu ya kuandika bila kuchelewa Linda aliniambia
“Andika hapa nimepaacha kwa ajili yako” aliniambia huku akielekeza kidole kwenye mfuko wa shati.Kwakweli alinipa kigugumizi maana mfuko wake ulikuwa karibu mno na chuchu ya ziwa lake la kushoto.

Huku nikiendelea kujiuliza Linda aliniambia
“Kama unahisi hutaandika vizuri jaribu kupaweka sawa we pashike tu usiogope”.

Sikutaka kupoteza muda kwa kuweka majibizano zaidi na mwanadada yule hivyo nililivuta shati na kuandika “K-baby” wakati naandika nilipatwa na wakati mgumu mno mana eneo nililotakiwa niandike lilikuwa ni nyeti sana.

Nilijikaza na kulifanya hivyo kwa uharaka sana kwani nilikwisha ziona dalili za Linda kupandwa na hisia pindi nilipokuwa nikiandika.Nilipokuwa nikiushusha mkono kuashiria kumaliza zoezi lile Linda alinikumbatia kwa haraka sana jambo ambalo sikutarajia litokee eneo la wazi lenye hadhira kama ile.

Kumbatio lile lilikuwa na maana kubwa mno kwake ambayo sikuweza kuielewa kwa wepesi, kwa wakati ule nilichukulia tu ni kama hisia za kuonana kwa mara ya mwisho kabla hatujaanza kuonana kwa kubahatisha.

Basi tukiwa katika kumbatio lile nilishtushwa na makofi yaliyokuwa yakipigwa na wanadarasa waliokuwa karibu na eneo lile, ikabidi tuachiane kutoka kwenye hali hiyo ambayo mimi na Linda tulikuwa kwenye dunia ya peke yetu.

Kila mtu aliongea alichojisikia huku wakisogea tulipo kana kwamba tuliwaita waje washuhudie jambo nasi hatukuwazuia wala kutaka kujitetea isipokuwa nilijiongeza na kuanza kuwakumbatia wanadarasa wengine huku nikiwaambia
” Ndugu zangu mi sikai hapa ndo naamsha hivyo tutaonana Mungu akipenda”.

Nilimtupia macho Linda naye nikamuona anafanya vilevile ila nikamsikia mnoko mmoja akisema
“Sawa mwanetu unatukumbatia vya mwisho mwisho ili uveshe home unasepa na Linda nini mana najua bado ana prac sasa na yeye anavyotuhagi vya mwisho mwisho mnakuwa mnanivuruga mjue”.

Ile anamaliza kusema vilianguka vicheko kama vyote kiasi cha kuwatoa kwenye mood ya kukumbatiana, basi nami nikautumia mwanya huohuo kuondoka eneo lile nikiwaacha na kucheka kwao.

Nilipofika bwenini wala sikuwa na mambo mengi mana kila kitu nilikwisha kiandaa nilijivutia zangu begi na kufungua zipu nikachomoa wallet.

Niliikagua kama vitu vyangu muhimu bado vilikuwepo mana ingawaje kwenye bweni hilo tulikuwa tukiishi watu wa darasa moja lakini lilikuwa wazi muda mwingi mana si wanadarasa wote tulikuwa tukifanya mtihani mmoja kwani michepuo tulitofautiana.

Basi baada ya kujiridhisha na hali ya begi nilizipiga macho sehemu mbalimbali za ndani ya bweni lile kama ishara ya kulitazama kwa mara ya mwisho sehemu hiyo ambayo sasa itakua imebaki hadithi kwamba niliwahi kupaishi mahala hapo.

Nilipotosheka nilinyanyua begi na kuliweka begani zikawa zinahesabika sekunde tu kabla ya kuachana kabisa na maeneo ya shule ile, hatua mojamoja kutoka bwenini kuelekea nje ya shule ndicho kilifuata.,,,,,,,,,,,,

Itaendelea…………...
Linda 🙌🏼 anataka namba iandikwe kwenye mfuko wa Shati 👏🏻
 
Umemtaja Linda umenikumbusha pendo langu la kwanza.Kidogo nidhani unamuongelea Linda wangu.Penzi lake lilinitoa jashoo aisee.
Oiii.
 
SEASON-1

EPISODE 02

Linda aliendelea kuhoji kwa kuniambia
“Nakweli umenikwaza haswa ila sawa tafanyaje tena, kwani huwezi ghairisha ukaondoka siku nyingine”.

Nami nikamjibu “Looh! Mamdogo nimeshakata tiketi I can’t for now” naye akanambia
“Imean ughairishe mi ntakulipia iyo nauli siku nyingine, imagine unaondoka ntasoma na nani sasa au unataka nifeli uende chuo pekeako, kumaliza mitihani haimaanishi ndiyo uondoke na kutuacha kwenye mataa”.

Mwana PCM huyo alikuwa amebakiza mitihani kadhaa kwani wao walikuwa na mitihani mingi zaidi yetu tuliokuwa na mitihani saba wao walikuwa na mitihani tisa.

Nilimshawishi na hatimaye aliniruhusu kuondoka ila alinisisitiza nimuachie namba zangu za simu nilipomwambia sina alinivuta shati na kuniandikia yake kwenye kifua.

Haikumtosha dada huyo alilitafuta shavu langu la kushoto na kuchora kitu ambacho sikuweza kugundua kwa urahisi ila nilihisi kama kuna kiduara kilichorwa kikifuatwa na maneno ambayo nayo sikuyatambua kwa urahisi.

Baada ya kuandikwa maneno hayo nilipewa sharti kuwa maandishi hayo yabaki mpaka pale nitakapofika kwetu na sikutakiwa kumuonesha mwanafunzi yeyote akanisomea kilichoandikwa na nikitekeleza hilo nitakuwa nimesamehewa kosa langu la kuondoka bila kuaga
.
Nilitingisha kichwa nikiashiria kukubaliana naye lakini alinitaka niandike chochote kwenye shati lake mbali na namba ya simu.

Kabla ya kufanya hivyo nilimhoji ni kwanini alichafua shati hilo ilihali ya kuwa bado yuko na mitihani ya kufanya akanijibu kuwa anayo mawili.

Majibu yake yalinipa ruhusa ya kuandika, nikiwa natafuta sehemu ya kuandika bila kuchelewa Linda aliniambia
“Andika hapa nimepaacha kwa ajili yako” aliniambia huku akielekeza kidole kwenye mfuko wa shati.Kwakweli alinipa kigugumizi maana mfuko wake ulikuwa karibu mno na chuchu ya ziwa lake la kushoto.

Huku nikiendelea kujiuliza Linda aliniambia
“Kama unahisi hutaandika vizuri jaribu kupaweka sawa we pashike tu usiogope”.

Sikutaka kupoteza muda kwa kuweka majibizano zaidi na mwanadada yule hivyo nililivuta shati na kuandika “K-baby” wakati naandika nilipatwa na wakati mgumu mno mana eneo nililotakiwa niandike lilikuwa ni nyeti sana.

Nilijikaza na kulifanya hivyo kwa uharaka sana kwani nilikwisha ziona dalili za Linda kupandwa na hisia pindi nilipokuwa nikiandika.Nilipokuwa nikiushusha mkono kuashiria kumaliza zoezi lile Linda alinikumbatia kwa haraka sana jambo ambalo sikutarajia litokee eneo la wazi lenye hadhira kama ile.

Kumbatio lile lilikuwa na maana kubwa mno kwake ambayo sikuweza kuielewa kwa wepesi, kwa wakati ule nilichukulia tu ni kama hisia za kuonana kwa mara ya mwisho kabla hatujaanza kuonana kwa kubahatisha.

Basi tukiwa katika kumbatio lile nilishtushwa na makofi yaliyokuwa yakipigwa na wanadarasa waliokuwa karibu na eneo lile, ikabidi tuachiane kutoka kwenye hali hiyo ambayo mimi na Linda tulikuwa kwenye dunia ya peke yetu.

Kila mtu aliongea alichojisikia huku wakisogea tulipo kana kwamba tuliwaita waje washuhudie jambo nasi hatukuwazuia wala kutaka kujitetea isipokuwa nilijiongeza na kuanza kuwakumbatia wanadarasa wengine huku nikiwaambia
” Ndugu zangu mi sikai hapa ndo naamsha hivyo tutaonana Mungu akipenda”.

Nilimtupia macho Linda naye nikamuona anafanya vilevile ila nikamsikia mnoko mmoja akisema
“Sawa mwanetu unatukumbatia vya mwisho mwisho ili uveshe home unasepa na Linda nini mana najua bado ana prac sasa na yeye anavyotuhagi vya mwisho mwisho mnakuwa mnanivuruga mjue”.

Ile anamaliza kusema vilianguka vicheko kama vyote kiasi cha kuwatoa kwenye mood ya kukumbatiana, basi nami nikautumia mwanya huohuo kuondoka eneo lile nikiwaacha na kucheka kwao.

Nilipofika bwenini wala sikuwa na mambo mengi mana kila kitu nilikwisha kiandaa nilijivutia zangu begi na kufungua zipu nikachomoa wallet.

Niliikagua kama vitu vyangu muhimu bado vilikuwepo mana ingawaje kwenye bweni hilo tulikuwa tukiishi watu wa darasa moja lakini lilikuwa wazi muda mwingi mana si wanadarasa wote tulikuwa tukifanya mtihani mmoja kwani michepuo tulitofautiana.

Basi baada ya kujiridhisha na hali ya begi nilizipiga macho sehemu mbalimbali za ndani ya bweni lile kama ishara ya kulitazama kwa mara ya mwisho sehemu hiyo ambayo sasa itakua imebaki hadithi kwamba niliwahi kupaishi mahala hapo.

Nilipotosheka nilinyanyua begi na kuliweka begani zikawa zinahesabika sekunde tu kabla ya kuachana kabisa na maeneo ya shule ile, hatua mojamoja kutoka bwenini kuelekea nje ya shule ndicho kilifuata.,,,,,,,,,,,,

Itaendelea…………...
MAISHA YA DEPO

SEASON-1

EPISODE 03

Niliwasiri kituo cha mabasi mnamo saa 7:52 na kama ulivyo utaratibu wa temino nyingine nilivamiwa na madalali wapatao wanne ambao kila mmoja alikuwa akinishawishi kuchagua kampuni ya mabasi aliyokuwa akiitumikia pasi na kujua ni wapi niendako.

Ilinichukua muda kuwapunguza mana hata nilipo wafahamisha kuwa nimekwishakata tiketi walishindwa kuniamini mpaka pale nilipoitwaa kutoka mfukoni mwangu na kuwaonesha nikaona mmojammoja anajipunguza na mmoja wao akanikabidhisha kwa wakala wa basi ambalo nimekata tiketi.

Nilifika nyumbani majira ya saa 2:33 nikawakuta wanafamilia wakinisubiri kwa hamu kwani walikuwa na shauku ya kuniona ikizingatiwa kuwa hapo kabla tulipokuwa tukiwasiliana walikuwa wakiniuliza siku ya kumaliza mtihani.

Lakini pia nikaja kugundua baadaye waliiwekea alama kwenye kalenda siku ile na waliandika mpaka muda wa kumaliza mtihani hivyo haikuwa kazi ngumu kwao kujua kuwa ningefika siku hiyo na hata hivyo niliwasiliana nao nilipokuwa safarini ambapo nilimuomba mmoja wa abiria tuliyepanda basi moja.

Nilisalimiana nao huku nikijitahidi kuuficha upande ule ulioandikwa na Linda mana sikuwa na imani yeyote kama alichokiandika kinastahili kuonekana na familia yangu.

Nilijifanya kama nasikia joto sana na uchovu ili nisikae nao kwa muda mrefu nikawapa nafasi ya kunikagua hivyo niliingia zangu chumbani na kubadili nguo kwa ajili ya kwenda kuoga.Baada ya kujitazama kwenye kioo niligundua kuwa binti yule alinichora kijikopa ndani yake kilichoandikwa
“Remember the name, lovely LINDA”.

Kwa kweli nilishukuru sana kwa akili niliyoipata ya kuuficha upande ule wa shavu maana tangu nipo safarini niliona ishara za abiria wenzangu kunitupia macho mara kwa mara.

Nilienda kuoga na baadaye nikaelekea mezani kula huku stori za hapa na pale zikiendelea mpaka majira ya saa tano za usiku nilipowaaga kwenda kulala.

Tayari nilikuwa na uchovu ambao ulinipelekea kusinzia na kwakua nilionekana kama msemaji mkuu usiku huo hata ile kasi ya masimulizi ilianza kupungua kwahiyo hakukuwa na namna zaidi ya kufunga kikao hicho.

Baada ya kupita siku tano tayari nilikwishapata kifaa cha mawasiliano ambacho hakikuwa na mbwembwe nyingi na mtaani kilifahamika kama kiswaswadu.

Kitu cha awali kabisa ilikuwa ni namba ya mwana wa Khamisi yaani Zainabu wa Mzee Khamisi classmate ambaye ningejutia sana ningekosa mawasiliano naye.

Kama kawaida nikaisave ZAIMISS, nilimtafuta kwa mara kadhaa nikaishia kujibiwa na yule mdada mwenye sauti nzuri akisema

“Namba unayopiga haipatikani kwasasa tafadhali jaribu tena baadaye, mwachie ujumbe wa sauti voice mail baada ya mlio gharama za kawaida zitatozwa”.

Basi mwendo ukawa ni huohuo mpaka nikahisi dada yule atakuwa amenipa namba ya gari yaani namba ya mchongo ama ya uongo kama ifahamikavyo katika Kiswahili sahihi.

Kwa kipindi hicho nilikuwa nikiwasiliana sana na mwanangu mmoja afahamikaye kwa jina la Shabani ambaye yeye alisomea uchumi alikuwa simu kubwa iliyomuwezesha kupata taarifa nyingi kwa wakati mmoja na kufanya kazi zaidi ya moja mbali ya mawasiliano yaani smartphone.

Shebi alikuwa akinipa taarifa nyingi za wanadarasa na aliniambia kwa wakati huo bado baadhi ya wanadarasa hawajarudi haswa wale wa masomo ya Sayansi.

Bado kuna watu walikuwa na practical ya biology sijajua kama ni B au C lakini tayari kuna wanafunzi walishafanya Biology 3A yaani practical ya Biolojia mkupuo A.

Aliniambia kuwa kuna jamaa wa PCB ambaye ndiye anayelichangamsha group la whatsapp mpaka kufikia wakati huo alikuwa bado hajarudi ndipo nikahisi kuwa huenda hata huyu Zaimiss akawa bado hajarudi ndiyo mana simpati kwenye simu.

Usiku mmoja nikiwa kitandani nilipokea meseji kutoka kwenye namba ngeni “Hellow K” vyovyote nikajua atakuwa ni Linda.

Nilifikiria kwa muda nijibu kitu gani kifupi nilitamani nisijibu mana nilijua kutakuwa na mrundikano wa kesi za kujibu kwani aliniachia namba yake ya simu na wala sikuthubutu kumtafuta ingali yakuwa hapo kabla kisingizio ilikuwa ni kukosa simu na sasa ninayo.

Niliona ni bora nikamjibu kuliko kukaa kimya hali ambayo ingeniongezea namba ya maswali, basi nika reply “Waoooh mamdogo”.

Kilichofuata baada ya hapo niliona namba ileile kabla ya kuisave ikiita niliipokea na kuongea naye baada ya salamu hakuna kingine zaidi ya lawama kama nilivyokuwa nikifikiri kwani nilimfahamu vizuri mwanadada huyo kwa kulalamika.,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

Itaendelea.......................
 
MAISHA YA DEPO

SEASON-1

EPISODE 03

Niliwasiri kituo cha mabasi mnamo saa 7:52 na kama ulivyo utaratibu wa temino nyingine nilivamiwa na madalali wapatao wanne ambao kila mmoja alikuwa akinishawishi kuchagua kampuni ya mabasi aliyokuwa akiitumikia pasi na kujua ni wapi niendako.

Ilinichukua muda kuwapunguza mana hata nilipo wafahamisha kuwa nimekwishakata tiketi walishindwa kuniamini mpaka pale nilipoitwaa kutoka mfukoni mwangu na kuwaonesha nikaona mmojammoja anajipunguza na mmoja wao akanikabidhisha kwa wakala wa basi ambalo nimekata tiketi.

Nilifika nyumbani majira ya saa 2:33 nikawakuta wanafamilia wakinisubiri kwa hamu kwani walikuwa na shauku ya kuniona ikizingatiwa kuwa hapo kabla tulipokuwa tukiwasiliana walikuwa wakiniuliza siku ya kumaliza mtihani.

Lakini pia nikaja kugundua baadaye waliiwekea alama kwenye kalenda siku ile na waliandika mpaka muda wa kumaliza mtihani hivyo haikuwa kazi ngumu kwao kujua kuwa ningefika siku hiyo na hata hivyo niliwasiliana nao nilipokuwa safarini ambapo nilimuomba mmoja wa abiria tuliyepanda basi moja.

Nilisalimiana nao huku nikijitahidi kuuficha upande ule ulioandikwa na Linda mana sikuwa na imani yeyote kama alichokiandika kinastahili kuonekana na familia yangu.

Nilijifanya kama nasikia joto sana na uchovu ili nisikae nao kwa muda mrefu nikawapa nafasi ya kunikagua hivyo niliingia zangu chumbani na kubadili nguo kwa ajili ya kwenda kuoga.Baada ya kujitazama kwenye kioo niligundua kuwa binti yule alinichora kijikopa ndani yake kilichoandikwa
“Remember the name, lovely LINDA”.

Kwa kweli nilishukuru sana kwa akili niliyoipata ya kuuficha upande ule wa shavu maana tangu nipo safarini niliona ishara za abiria wenzangu kunitupia macho mara kwa mara.

Nilienda kuoga na baadaye nikaelekea mezani kula huku stori za hapa na pale zikiendelea mpaka majira ya saa tano za usiku nilipowaaga kwenda kulala.

Tayari nilikuwa na uchovu ambao ulinipelekea kusinzia na kwakua nilionekana kama msemaji mkuu usiku huo hata ile kasi ya masimulizi ilianza kupungua kwahiyo hakukuwa na namna zaidi ya kufunga kikao hicho.

Baada ya kupita siku tano tayari nilikwishapata kifaa cha mawasiliano ambacho hakikuwa na mbwembwe nyingi na mtaani kilifahamika kama kiswaswadu.

Kitu cha awali kabisa ilikuwa ni namba ya mwana wa Khamisi yaani Zainabu wa Mzee Khamisi classmate ambaye ningejutia sana ningekosa mawasiliano naye.

Kama kawaida nikaisave ZAIMISS, nilimtafuta kwa mara kadhaa nikaishia kujibiwa na yule mdada mwenye sauti nzuri akisema

“Namba unayopiga haipatikani kwasasa tafadhali jaribu tena baadaye, mwachie ujumbe wa sauti voice mail baada ya mlio gharama za kawaida zitatozwa”.

Basi mwendo ukawa ni huohuo mpaka nikahisi dada yule atakuwa amenipa namba ya gari yaani namba ya mchongo ama ya uongo kama ifahamikavyo katika Kiswahili sahihi.

Kwa kipindi hicho nilikuwa nikiwasiliana sana na mwanangu mmoja afahamikaye kwa jina la Shabani ambaye yeye alisomea uchumi alikuwa simu kubwa iliyomuwezesha kupata taarifa nyingi kwa wakati mmoja na kufanya kazi zaidi ya moja mbali ya mawasiliano yaani smartphone.

Shebi alikuwa akinipa taarifa nyingi za wanadarasa na aliniambia kwa wakati huo bado baadhi ya wanadarasa hawajarudi haswa wale wa masomo ya Sayansi.

Bado kuna watu walikuwa na practical ya biology sijajua kama ni B au C lakini tayari kuna wanafunzi walishafanya Biology 3A yaani practical ya Biolojia mkupuo A.

Aliniambia kuwa kuna jamaa wa PCB ambaye ndiye anayelichangamsha group la whatsapp mpaka kufikia wakati huo alikuwa bado hajarudi ndipo nikahisi kuwa huenda hata huyu Zaimiss akawa bado hajarudi ndiyo mana simpati kwenye simu.

Usiku mmoja nikiwa kitandani nilipokea meseji kutoka kwenye namba ngeni “Hellow K” vyovyote nikajua atakuwa ni Linda.

Nilifikiria kwa muda nijibu kitu gani kifupi nilitamani nisijibu mana nilijua kutakuwa na mrundikano wa kesi za kujibu kwani aliniachia namba yake ya simu na wala sikuthubutu kumtafuta ingali yakuwa hapo kabla kisingizio ilikuwa ni kukosa simu na sasa ninayo.

Niliona ni bora nikamjibu kuliko kukaa kimya hali ambayo ingeniongezea namba ya maswali, basi nika reply “Waoooh mamdogo”.

Kilichofuata baada ya hapo niliona namba ileile kabla ya kuisave ikiita niliipokea na kuongea naye baada ya salamu hakuna kingine zaidi ya lawama kama nilivyokuwa nikifikiri kwani nilimfahamu vizuri mwanadada huyo kwa kulalamika.,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

MAISHA YA DEPO

SEASON-1

EPISODE 04

Nilijitetea kwa kumwambia kuwa “Namba siioni na hata leo hii mchana nimejitahidi kufukunyua kwenye begi lakini wapi, hata hivyo ile siku natoka pale bweni la Mikumi mpaka napanda basi la kuja nyumbani ilikuwa ni shughuli Mamdogo.

Nilipofika nyumbani begi lenyewe nilipokelewa nimekuja kulishika siku ya pili yaani kurupushani zilikuwa ni zaidi ya nyingi wala sijafanya kusudi kutokukutafuta”.

Baada ya maneno hayo nilisikia sauti ya Kichaga ikisema “Ewe Mungu wa majeshi embu shuka duniani uje umnusuru mtu wako huyu aliyejawa na damu ya uwongo kwenye mishipa yake, yaani anavyoongea ni kana kwamba ile namba nilimuandikia kwenye kikaratasi”
kwakweli nilijichanganya hali iliyonifanya nibaki kimya na kumuacha aongee yeye tu.

Linda aliendelea kuongea na kuniuliza “umeshindwaje kuomba kwa mtu jamani, mbona wana wengi tu wanayo”.

Nikapata nguvu za kumjibu ila kwa sauti ya upole sana nikamwambia “Samahani sikuwa na wazo hilo ila nilikuwa naamini ninayo hivyo ipo siku ningeiona tu”.

Basi mazungumzo yalikuwa ni mengi ila kikubwa ilikuwa ni kwanini sikumtafuta siku zote hizo, kwakua nilikuwa nikimfahamu vizuri sikuhitajika kutumia nguvu nyingi kujitetea nilichofanya nilimtuliza nikampooza na hatimaye jazba likamshuka.

Nilijaribu kumdodosa Linda kama kuna watu bado hawajamaliza mitihani, aliniambia kuwa wamewaacha PCB na CBG wanasubiri practical ya Biology ila kesho yake ndiyo wanamalizia.

Maneno hayo yalinipa matumaini ya kwamba huenda Zai hakunipa namba ya uongo ila bado yuko shule na ndiyo maana hapatikani kwenye simu.

Nilitamani kumuuliza Linda kama kweli Zai naye ni miongoni mwa wale aliowaacha ila nikaona ni bora niache maana ataniona kama namjali Zai kuliko yeye kitu ambacho hakipendi na zaidi ya hapo ni kuwa tumetoka kumaliza swala kama hilo la kutomjali yeye.

Niliendelea kufanya juhudi za kumtafuta Zai pasi na mafanikio kwani hata pale nilipoulizia kama wamekwisharudi nyumbani wanafunzi wote waliomaliza kidato cha sita niliambiwa wamerudi ila kila nilipompigia msichana yule majibu yalikuwa ni yale yale “hapatikani”.

Siku moja nilipokuwa naongea na Shebi nilijaribu kumdodosa kuhusu Zainabu “oya hivi Zainabu unaongea naye kweli”“Zainabu yupi?”“Zainabu Khamisi yule dada wa CBG tumemaliza naye pale kiskuli”“Anhaah yule hapana nasikia kwenye simu hapatikani hata mimi kuna siku nilimpigia ila sikumpata, vipi kwani shemeji yetu nini”.

“Hapana ni mwana tu nimempigia sana ila naona kila nikipiga hapatikani nikaona nikuulize afisa habari huenda labda una namba nyingine au mnakutana kwenye group la class whatsapp siunajua sisi wengine tunamiliki viswaswadu”.

“Akipatikana au akijoin kwa group ntakustua ila kwa sasa sina mawasiliano naye, ila mbona kama unamsaka kwa udi na uvumba hivyo kwema kweli”.

“Duuh mwanangu Shebi mbona umenishikia shilingi hivyo wala hakuna shida yoyote ile nimekwambia ni mwana tu au kwa sababu ni wa kike ndo mana unanikabia kwa juu hivyo”.

“Basi usiwaze tukimpata tutakwambia sema ungetuweka wazi tujue kama amemaliza na kichanga chetu tumboni tuongeze juhudi maradufu ya kumtafuta”.

“Hamna mwanangu amini kwamba, ni mwana tu”

“Sawa nimekuelewa mwanangu nilikuwa nakuzingua tu kwani unafikiri hatujui kuwa umekufa kwa Linda”

“Linda tena?”

“Acha uhuni baba Linda kwahiyo unataka umkane Linda mbele yangu kuwa siyo demu wako?”

“Asa mi sindo nakupangilia yule mi mshikaji wangu tu tulikua tunapeana sapoti kwenye kusoma na vitu vidogovidogo ila swala la mahusiano na yeye kwakweli halipo”

“Aah we jamaa kwakukana umenishinda tabia wakati kila mtu pale class anajua juu ya uhusiano wenu Linda mwenyewe hata ukimpigia sasa hivi ukamuita mama K anafurahi kweli na anapenda kinoma ila wewe mwanangu sababu hayupo karibu na hawezi kutusikia ndo unajifanya kumkana siyo fair hivyo”.

“Siyo kwamba anafurahi ila anakucheka kwa maana hujui juu ya unachokisema ila ni mshikaji, ni mwana ni kampani ndo ilikuwa inatufanya tuwe karibu vile wala hakuna cha ziada”

“Sawa ngoja nimuunganishe kwenye simu afu umkane akisikia wewe siunajikuta Petro unaweza kukana watu kweupe”

“Oya Shebi kwani leo umekula nini mbona umeniamulia hivyo tatizo ni nini kwani"

“Tatizo ni kwamba unawakana wadada za watu kwasababu tu hawapo subiri nifanye mpango nimuunge akusikie”

“Kausha Shebi usimuunganishe bana usije kuniletea msala nishaichoka mimi”

“Umeona eeh hutaki kumbe kweli ni demu wako”.

Siku ziliendelea kusonga mithili ya maji yaliyopita kwenye mkondo wake, siku moja jamaa yangu mmoja aitwaye Ambrose alinitafuta kwenye simu na kunipa taarifa ya kuwa nimekuwa miongoni mwa wanafunzi waliochaguliwa na Jeshi la kujenga taifa kuhudhuria mafunzo ya kijeshi kama ilivyo sera ya elimu kwa wanafunzi wanaohitimu kidato cha sita nchini Tanzania. ,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

Itaendelea……………………………………………
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom