Maisha baada ya kumzika mwanangu

Maisha baada ya kumzika mwanangu

Binadam tumeambiwa kusahau, hiyo Hali itaisha baada ya muda. Ni kawaida kupitia Hali uliyonayo, Cha msingi usijidhuru.

Pole sana, hapa wengi tunaongea na kuelewa unachopitia lakini wewe binafsi ndio unajua uchungu na maumivu uliyonayo.

Sasa jiulize hili swali, wewe ni WA kwanza kufiwa na mtoto? Wewe ni WA kwanza kufiwa na ndugu? Majibu ya hayo maswali yote ni hapana, kama hao waliotangulia kufikwa na misiba wameendelea na maisha, elewa kwamba hata wewe hii Hali itapita baada ya muda.

Usiwaze kujidhuru Wala kutoa uhai wako, itaathiri utendaji wa kazi na maisha Yako usipokua makini.

Be Still
 
Habari ndugu zangu,

Asante kwa wote mliolia nami katika kifo cha binti yangu mpendwa aliefariki kwa uzembe wa watu wa afya, faraja yenu ilikuwa tiba sana sijaamini JamiiForums kuna watu wana roho nzuri hivi na wanaumia kwa matatizo ya watu.

Maisha baada ya maziko yamekuwa magumu sana muda wote nalia nimeshindwa kurejea kawaida, kwa sasa natamani kufa tu maana naona giza kuna njia yoyote ya kusaidia kuondoka hali niliyonayo?

Naishi peke yangu mama yake tulikuwa hatukai pamoja ila yeye baada ya msiba amehama mkoa kabisa.

Pia soma - Kifo cha mwanangu kipenzi kimetokana na uzembe
Naishi peke yangu mama yake tulikuwa hatukai pamoja ila yeye baada ya msiba amehama mkoa kabisa.

hii kauli sijaielewa.
 
Nature ya kila kiumbe chenye uhai mwisho wake ni kifo,tunaumia kwa kuondokewa coz ya mazowea tu.

Jichanganye na watu mkuu,usipende kukaa peke yako.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom