Maini ya kitimoto yanafaa kwa lishe ya mtoto?

Maini ya kitimoto yanafaa kwa lishe ya mtoto?

Ramea

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2015
Posts
2,146
Reaction score
4,090
Nina twins wenye miezi tisa. Katika kuzaliwa kwao kulikuwa na complication kidogo hasa kwa Doto, ambaye alikaa vibaya na tulitegemea atatoka kwa operation, lakini Mungu akatia wepesi, wote walizaliwa kwa njia ya kawaida. Aligeuka vizuri baada ya mwenzake kutoka, Mana yeye alilala kiubavu.

Nirudi kwenye mada, huyu wa kwanza kuzaliwa ana afya Njema tu amemzidi mwenzie kama kilo moja na gram 400 hivi. Katika mahudhurio yao clinic Nesi ameshauri tutumie Maini Kama lishe kwa mama na watoto. Kiukweli hapa nyumbani maini ya kitimoto hayaishagi (hata leo yapo nimenunua kilo na nusu) ila sijawahi kuwapa watoto, tunakula tu wenyewe.

Je, haya yanafaa kwa watoto? Mana Nesi kasema tu 'maini' hajawa specific, kama ya mbuzi, ng'ombe, kitimoto au kuku.
 
Usije kumpa maini ya kitomoto kwani hayo maini ukija kumpa mwanao anaweza kudhurika na kupatwa na maradhi. Kwani Maini au nyama ya kitomoto hata uchemshe vipi wadudu aka Bacteria wake hawafi wakati wa kula utawala na hao Bacteria wa kitomoto wana sababisha maradhi mwilini mwa binadamu.Usijaribu kumpa hayo Maini ya kitomoto. Mpe maini ya ng'ombe. Na huyo mtoto wako ana muda gani tangu azaliwe?
 
Usije kumpa maini ya kitomoto kwani hayo maini ukija kumpa mwanao anaweza kudhurika na kupatwa na maradhi. Kwani Maini au nyama ya kitomoto hata uchemshe vipi wadudu aka Bacteria wake hawafi wakati wa kula utawala na hao Bacteria wa kitomoto wana sababisha maradhi mwilini mwa binadamu.Usijaribu kumpa hayo Maini ya kitomoto. Mpe maini ya ng'ombe. Na huyo mtoto wako ana muda gani tangu azaliwe?
Hujamaliza kusoma hapo juu. Nimesema wana miezi tisa.
Asante kwa ushauri mkuu.
 
Inaweza kua nacho kushauri hakiko kiutalaamu kiundani lakini siku-recommend umpe mtoto maini yeyote haijalishi yawe ya ng'ombe au mnyama gani.

Maini ni kama filter, kila taka yenye sumu hufikia pake hili ni muhimu kulijua so mpaka unampa mtoto ale ujue kabisa unamlisha nyama ya namna gani.

Na kwa upande wa nguruwe sidhani kama asilimia kubwa ya wanao chinjwa hufanyiwa (check-up) vipimo vya magonjwa na madaktari wa mifugo kabla hawaja chinjwa. so kuna opportunity kubwa kula nyama ya mnyama ambaye alikufa kwa kula sumu au matatizo mengine
 
Aisee usimpe mtoto maini hujui yale kazi yake kuchuja simu mwilini, wape samaki kwa wingi, nunua samaki wachemshe, wachambue kabisa kusiwe na nwiba hata mmoja then pika mtori wa ndizi bukoba, changanya na huo mchambuko wa samaki za kutosha tia carrots, hoho, vitunguu .. deliciosoooo kwa mtoto
 
Usiwape!

Ni huku bongo sababu ya ufahamu juu ya mambo ya lishe kuwa chini Ndiyo maana utashangaa Eti bei ya maini ya ng’ombe / mbuzi kuwa juu kuliko hata nyama yenyewe!

Lakini kwa nchi zenye kufanya tafiti za kisayansi kabla wenyewe nyama za ndani ya mnyama kama vile ng’ombe /mbuzi utumbo, maini huwa hawahangaini navyo na hata bei zao ni za chini sana!

Tena hayo maini ya nguruwe ndo kabisa hayafai afadhali kidogo ya ng’ombe au mbuzi
 
Aisee usimpe mtoto maini hujui yale kazi yake kuchuja simu mwilini, wape samaki kwa wingi, nunua samaki wachemshe, wachambue kabisa kusiwe na nwiba hata mmoja then pika mtori wa ndizi bukoba, changanya na huo mchambuko wa samaki za kutosha tia carrots, hoho, vitunguu .. deliciosoooo kwa mtoto
Hii nimeipenda.
 
Usiwape!

Ni huku bongo sababu ya ufahamu juu ya mambo ya lishe kuwa chini Ndiyo maana utashangaa Eti bei ya maini ya ng’ombe / mbuzi kuwa juu kuliko hata nyama yenyewe!..
Mtaalam wa afya kashauri lishe ya maini. Asante kwa mawazo yako.
 
Hayafai kabisa ndani ya maini wanyama kuna minyoo usijaribu kabisa hata wewe kuyala
 
usiwe na haraka madaktari wapo humu utapata ushauri mzuri tu kua na subra
 
Mmmmh........hivi ana maini eeh....
Namtumia sana ila sikuwaza kama anayo......
Na figo je....?
Mimi nachukua viungo adimu vya kitimoto. Maini, moyo, figo na ulimi. Jamaa akichinja tu lazima anipigie kujua Kama nitachukua.
 
Mimi nachukua viungo adimu vya kitimoto. Maini, moyo, figo na ulimi. Jamaa akichinja tu lazima anipigie kujua Kama nitachukua.

Ni kwa ajili ya dawa au nini......?
Sijawahi kuvisikia hivi viungo kwenye menu pendwa ya huyu mwanambuzi.....
 
Ni kwa ajili ya dawa au nini......?
Sijawahi kuvisikia hivi viungo kwenye menu pendwa ya huyu mwanambuzi.....
Hapana, hiyo ni nyama pendwa, tunauziwa watu wenye ukaribu na bucha. Mara nyingi maini huliwa na wachinjaji/wafugaji wenyewe.
 
Back
Top Bottom