Mahojiano ya Msigwa na Lema KTN: Serikali iongeze msisitizo kwenye somo la Kiingereza

Wakenya walioangalia hiyo interview hawaongelei lugha tatizo nyie watanzania na uchama wenu ndio mnaona lugha zaidi na si kingine. poleni
aah we jamaa bana, hujaona tatizo?? hapo wanasnza tu msigwa kaulizwa kuhusu lissu anaendeleaje akajibu " atleast today he got a little bit of tea" yaan hapo hujaona tatzo?? kweli???
 
Tatizo kubwa ni kuwa Mh. Msigwa na Mh. Lema ni weupe kichwani, I am very sorry to say that, Sasa changanya na Lugha, oh my God! Unawaona wachina hawajui kiingereza lakini akisema point yake hata kwa kuvunja lugha lakini ikawa ina maantink- Yaani Logic, it is far better. Kuliko vyote mweupe, Amini nikuambiacho!

hivi kuna mtu kichwa maji kama yule ambae kipindi wenzake wana majonzi na wanahitaji maneno ya faraja na matumaini, yeye anawaambia kazi yao ni kupiga "katerero"? and yet he dares kuita wengine vilaza!
 
Bungeni anachapia maneno machache ili aonekane anajua English sasa Kenya kaanikwa. Ni wale wale, Bata!
Haha haha haha haha haha umenichekesha sana. Ni kweli kabisa mkuu ukiona mtu kila akiongea Kiswahili anatoa neno moja bombastic la English, jua kabisa huyo lugha aipo ukimbana ukaongea nae moja kwa moja kwa English apo ni chalii
 
Mahojiano ya Lema na Msigwa ndani ya KTN, nadhani Lema na Msigwa walikuwa wana mambo mengi ya kuiambia dunia lakini ukosefu wa maneno kadhaa ya kiiengereza kumewaficha sana.

Mfano neno dictator uchwara ukiliongea kwa kiingereza linapoteza uzito.

Lema kaongea 'actually' mara 83 kwnye interview ya dk 24.



Tunapotaka kuongelea kiingereza cha Rais inabidi tuangalie kwanza wapi tumekanyaga.

hahahahahahahahahahahahah balaaaaaa kubwa sana
 
Siku nyingine aitwe na mbowe na sugu nao waongee

Sent using Jamii Forums mobile app
Na Mwita waitara na Heche wachape lugha uone lugha itakayozungymzwa apo ni utumbo mtupu
Watanzania waliokuwa wanaongea lugha nzuri wengi wapo kwenye Umri wa miaka ya 65 na kuendelea waliosoma kwa mkoloni lakini wengi waliofata ni upuuzi na upupu katika lugha ya English. Madokta na Maprofesa wengi tuuu lugha ya English ni tatizo, sio swala la kushangaa kwa sababu hatutumii lugha ya English katika maofisini au mashuleni. Hata walimu waliopo masekondari na primary hawajui lugha ya English
 
Kuna haja kubwa sana ya hao viongozi kwenye mahojiano haya kujitazama upya kwenye: 1. Umahiri wa maudhui, 2. Matumizi ya lugha - hawakuwa huru na kiingereza, walikuwa wanyonge, hakukuwa na lazima ya kutumia lugha wasiyoifahamu, 3. Ufahamu. Kwa ujumla wana ufahamu mdogo sana wa masuala mbalimbali. Huyu waziri kivuli wa mambo ya nje ajifunze zaidi (aache kufikiri anajua wakati hajui masuala mengi), 5. Maandalizi ya mahojiano: Ni kuwa hawakujiandaa au walifikiri mahojiano ni kitu kidogo. Sifikirii kuwa wataruhusiwa tena kuhojiwa na vyombo vya habari vya nje.
 
Mkuu mtake radhi mwenyekiti museveni, anabonga kiinglish cha malkia lakini kwa lafudhi ya kiganda, sisi wabongo tuliokwenda shule 99 asilimia hatuwezi kuongea hata kwa dakika 1 tu mfululizo. Tuko vizuri kwenye swanglish Yaani unaongea kiswahili maneno ma 5 unakumbuka moja la kukariri darasani.
Museveni yuko vizuri sana kwenye hii lugha ya Malkia. Mtu aliyekuwa anaivunja si mwingine bali ni Iddi Amin Dadaa!

Museveni anaongea Ugandan English famously known as UGLISH.
 
Wow...I overlooked that.

Msigwa kweli ndiye shadow foreign minister eeh?

Kama watu wenyewe wa kushika dola ndo hawa basi CHADEMA bado sana kuweza kushika dola.

Lakini kwa wakati huo huo, Msigwa ana tofauti gani kubwa na Magufuli katika uelewa wa mambo?
Tofauti ni kubwa sana. Nadhani Msigwa angekuwa na busara angetafuta mkalimani
 
Mahojiano ya Lema na Msigwa ndani ya KTN, nadhani Lema na Msigwa walikuwa wana mambo mengi ya kuiambia dunia lakini ukosefu wa maneno kadhaa ya kiiengereza kumewaficha sana.

Mfano neno dictator uchwara ukiliongea kwa kiingereza linapoteza uzito.

Lema kaongea 'actually' mara 83 kwnye interview ya dk 24.



Tunapotaka kuongelea kiingereza cha Rais inabidi tuangalie kwanza wapi tumekanyaga.

ziszis I mean I mean actually actually kibao hiyo ndio chadema
 
Na Mwita waitara na Heche wachape lugha uone lugha itakayozungymzwa apo ni utumbo mtupu
Watanzania waliokuwa wanaongea lugha nzuri wengi wapo kwenye Umri wa miaka ya 65 na kuendelea waliosoma kwa mkoloni lakini wengi waliofata ni upuuzi na upupu katika lugha ya English. Madokta na Maprofesa wengi tuuu lugha ya English ni tatizo, sio swala la kushangaa kwa sababu hatutumii lugha ya English katika maofisini au mashuleni. Hata walimu waliopo masekondari na primary hawajui lugha ya English
Mbona unaanza kumtusi raiss wako
 
aah we jamaa bana, hujaona tatizo?? hapo wanasnza tu msigwa kaulizwa kuhusu lissu anaendeleaje akajibu " atleast today he got a little bit of tea" yaan hapo hujaona tatzo?? kweli???
Akikosea mungu wenu huwa mnasema hakuna tatizo maana yy ni mtanzania
Lkn MSIGWA kajitahidi zaidi yake mnaponda
Mtumwa yupo radhi hata kumpisha bwana ake kitanda alale na mkewe ili tu asifiwe na ajiendekeze
 
Msaga Sumu lugha ni kama njia tu ya kufikisha ujumbe kwa hadhira.

Haiyumkini Watanzania huwa tunapata shida sana inapofika suala la Lugha, nina mifano mingi tu inayoonyesha wenzetu huko tunakotaka kuwaiga huwa wanatumia sana Lugha zao, mfano Wachina, waarabu, warusi, wajerumani nk, ni ajabu sisi tunachekana mtu asipojua Kiingereza kulikoni?
 
Eric Omondi, comedian wa Kenya,ana comedy skit yakemoja nzuri sanaanawasema wanariadha wa Kenya wanavyoiaibisha Kenya nje kwa kusema Kiingereza wasichokijua vizuri.

Unaweza kusema Eric ana kasumba ya kulinganisha ujuzi wa Kiingereza na usomi/werevu.

Lakinipoint ya Eric sikwamba wanariadha wale hawajui Kiingereza, la.Point yake nikwamba wanariadha wale wamekosea mara mbili.

Mara ya kwanza wamekosea kwa kutakakujieleza kwalugha wasiyoijua vizuri. Wangeweza kujieleza vizuri zaidi kwa kutumia lugha wanayoijua zaidi kamaKiswahili au hata lugha zao za makabila.

Lakinipoint ya piliya Eric, ambayo ni kubwa zaidi kwangu, ni kwamba hawa wanariadha wanajishusha hadhi yao ya ubingwa. Kwamba bingwa mzima anahangaikakuongea lugha asiyoijua vizuri wakati dunia nzimainataka kumsikiliza yeye,ujinga huo. Bingwa anatakiwa awe huru kuongea hata Kikamba ama Kikikuyu, wanahabari wa dunia watatafuta mkalimanitu kama wanataka kujua bingwa anatakakusema nini.

Obviously Eric was being a bit dramatic toemploy the comedic effect. But I can't find fault with the core of his logic.

Katika kujitutumua tuonekane tunajua sana kwa kuongea Kiingereza tusichokijua, tunajishuasha.

Kwa kujishusha kuongea lugha tunazozijua na hata kuwekewa wakalimani, tunajitambua umuhimu wetu.
 
Kwa karne ukimkuta mtu bado anazungumzia kujua lugha za kigeni ndio jambo la maana sana mshangaa sana ni makosa makubwa na na ni upungufu wa watu kujua kwamba unapoongea lugha unayoilewa kwa ukamilivu ndio unaweza kumpa mtu kilicho sahihi zaidi tubadilike tu hata kama unajua kiingereza kwa ufasaha tutumie kiswahili kwa nguvu zote HONGERA WACHINA
 
Mahojiano ya Lema na Msigwa ndani ya KTN, nadhani Lema na Msigwa walikuwa wana mambo mengi ya kuiambia dunia lakini ukosefu wa maneno kadhaa ya kiiengereza kumewaficha sana.

Mfano neno dictator uchwara ukiliongea kwa kiingereza linapoteza uzito.

Lema kaongea 'actually' mara 83 kwnye interview ya dk 24.



Tunapotaka kuongelea kiingereza cha Rais inabidi tuangalie kwanza wapi tumekanyaga.

Mleta maada wewe ni mnafiki. Kiingereza cha waheshimiwa siyo kibaya ki vile, ukizingatia lugha hii si ya kwetu. Mimi nimekaa na watu toka russia, na nchi zingine za ulaya mashariki wana kiingereza kibovu sana. Mi nawapa heko, wamejitahidi kwa kiwango chao.
 
Back
Top Bottom