kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
Serikali imesema haijashtushwa na matokeo mabaya ya shule za sekondari za kata na imewashangaa watu wanaozibeza shule hizo.
Hayo yalisemwa jana jijini Dar es salaam na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mwantumu Mahiza, wakati wa uzinduzi wa harambee ya kuchangia elimu Wilaya ya Kisarawe, iliyoandaliwa na Fashion for Education Benefit.
Alisema serikali inaona changamoto ya shule hizo kuwa ni mafanikio makubwa kwake.
Wakati tunaanza mpango wa kujenga shule zile tulijua kabisa ni vigumu kukamilisha kila kitu, maabara, nyumba za walimu na walimu wa kutosha, hivyo yanayosemwa juu ya shule hizo ni changamoto ya kusonga mbele, alisema.
Alisema serikali imeweka mkakati wa kuziimarisha shule hizo ili zipate maabara, nyumba za walimu, vitabu vya kutosha, nyumba za walimu na walimu bora. Alisema wanaozibeza shule hizo hawajui watendalo kwani miaka michache ijayo angalau kila kata nchini itakuwa na wahitimu wa kidato cha nne.
Hivi nyinyi mlitaka tuendelee na utaratibu wa kujenga shule moja moja tungefika hapa tulipofika angalau kwa sasa, hamuoni kwamba shule hizi zitawasaidia watu wengi wa kipato cha chini kwenda shule, tufanye wewe ndo ungekuwa Rais halafu asilimia 75 ya watoto wanaopaswa kwenda sekondari hawaendi ungejisikiaje? Tunaomba mtuunge mkono maana mpango huu ni ukombozi kwa watanzania jamani, alisema.
Aliongeza kuwa shule hizo ndizo zitasaidia kwa kiwango kikubwa kuondoa tatizo la mimba za utotoni kwa kuwa wasichana wengi watakuwa shule. Alisema pia zitaondoa tatizo la wanaume kuoa vibinti vidogo kwani wazazi walio wengi watamudu kuwapeleka shule.
Hata muendelee kuzipa majina ya aina gani, shule hizi zipo na zitaendelea kuwepo na ndizo mkombozi wenu kama hamfahamu, alisema.
Jumla ya Shilingi bilioni 10 zinatarajiwa kupatikana katika harambee hiyo ya kuzichangia shule za sekondari za kata.
Hayo yalisemwa jana jijini Dar es salaam na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mwantumu Mahiza, wakati wa uzinduzi wa harambee ya kuchangia elimu Wilaya ya Kisarawe, iliyoandaliwa na Fashion for Education Benefit.
Alisema serikali inaona changamoto ya shule hizo kuwa ni mafanikio makubwa kwake.
Wakati tunaanza mpango wa kujenga shule zile tulijua kabisa ni vigumu kukamilisha kila kitu, maabara, nyumba za walimu na walimu wa kutosha, hivyo yanayosemwa juu ya shule hizo ni changamoto ya kusonga mbele, alisema.
Alisema serikali imeweka mkakati wa kuziimarisha shule hizo ili zipate maabara, nyumba za walimu, vitabu vya kutosha, nyumba za walimu na walimu bora. Alisema wanaozibeza shule hizo hawajui watendalo kwani miaka michache ijayo angalau kila kata nchini itakuwa na wahitimu wa kidato cha nne.
Hivi nyinyi mlitaka tuendelee na utaratibu wa kujenga shule moja moja tungefika hapa tulipofika angalau kwa sasa, hamuoni kwamba shule hizi zitawasaidia watu wengi wa kipato cha chini kwenda shule, tufanye wewe ndo ungekuwa Rais halafu asilimia 75 ya watoto wanaopaswa kwenda sekondari hawaendi ungejisikiaje? Tunaomba mtuunge mkono maana mpango huu ni ukombozi kwa watanzania jamani, alisema.
Aliongeza kuwa shule hizo ndizo zitasaidia kwa kiwango kikubwa kuondoa tatizo la mimba za utotoni kwa kuwa wasichana wengi watakuwa shule. Alisema pia zitaondoa tatizo la wanaume kuoa vibinti vidogo kwani wazazi walio wengi watamudu kuwapeleka shule.
Hata muendelee kuzipa majina ya aina gani, shule hizi zipo na zitaendelea kuwepo na ndizo mkombozi wenu kama hamfahamu, alisema.
Jumla ya Shilingi bilioni 10 zinatarajiwa kupatikana katika harambee hiyo ya kuzichangia shule za sekondari za kata.