Mahayatollah wajiandae kudondoshwa

Mahayatollah wajiandae kudondoshwa

The Father of All

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2012
Posts
11,100
Reaction score
13,693
1767478504380.jpeg

Kinachoendelea Venezuela chaweza kuwa kutisha mahayatollaj wa Iran ak kuiandaa dunia kwa anguko la serkali ya kikatili ya Iran. Waiting na Idi Amin Mama angekuwa kwenye kundi hili. Achunge mashehena wake wasimponze.
Najisemea.
 
Unaua, unadhulumu wananchi wako kama Samuya, Ayatollah’s na madulo, lazima wahuni kama Trump wakufanye mbaya tuu, sijui kwanini watu wanashindwa kujua siri kubwa ya maendeleo ni haki kwa kila mtu kwanza,utajiri na amani vyote ni matokeo ya haki, bila haki umaskini ni lazima
 
Huyo ana rada zake Baharini kamuweka muyemeni, mlangoni yupo Iraq, mbavuni Lebanon Ayatollah hawatathubutu ile mashariki ya kati itanuka yote hio gharama Kwa Sasa US na Ulaya Bado hawaiwezi. Mfano ni like jaribio la juni24 vumbi mpaka Qatar lilitimka.
 
apo atasubiria sana, huyo anaongeaga mara 1 tu
Ayatollah na utawala wa Mullah wa Iran lazima wang'olewe kabla ya Trump hajaondoka madarakani. Tunza hii post

Sasa hivi Trump na watu wake wamejifungia situation room wanasuka mipango ya jinsi ya kuiendesha Iran baada ya kuwatoa mamullah
 
Ayatollah na utawala wa Mullah wa Iran lazima wang'olewe kabla ya Trump hajaondoka madarakani. Tunza hii post

Sasa hivi Trump na watu wake wamejifungia situation room wanasuka mipango ya jinsi ya kuiendesha Iran baada ya kuwatoa mamullah
Iran sio Venezuela
 
Tofauti kati ya Iran na Venezuela ni jambo moja: IRGC.

Kikosi cha Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ni kikosi sambamba cha kijeshi kilichoundwa na kutengenezwa kulinda uongozi wa Jamhuri ya Kiislamu na kusafirisha itikadi ya Kishia nje ya mipaka ya Iran.

Uislamu wa Jihadi si ukomunisti "laini". Ni wa kujiua na mkatili.

Isipokuwa waandamanaji wa Iran watapata msaada wa moja kwa moja na mkubwa wa kijeshi - haswa hatua zinazopunguza na kupooza IRGC - kwa bahati mbaya, kuna uwezekano wa kushuhudia mauaji makubwa.
 
Haya hata MO29 yalitokea sana

Ujumbe kutoka Iran:

“Mpendwa Amir, nafanya kazi katika hospitali ya ***** huko Tehran.

Kwa usalama wangu, siwezi kufichua utambulisho wangu. Kuna kamera za usalama hata ndani ya *, na kuwasiliana nawe huniweka hatarini. Naweza kusema tu kwamba mimi ni fundi wa *.

Tangu maandamano yaanze, wagonjwa kutoka miji mingi wameletwa kwetu. Watoto wadogo kama miaka mitano na wanawake zaidi ya sabini. Walipigwa risasi machoni kwa chembechembe za chuma. Tunafanya kazi ya kuwaondoa, lakini wengi huacha vipofu kabisa.

Huu si ukatili wa nasibu. Ni wa makusudi. Ninachokiona kila siku ni uhalifu dhidi ya ubinadamu.

Watu wa Iran hawana ulinzi na sauti. Tunakandamizwa kimya kimya.

Tafadhali nisaidie kushiriki hili na ulimwengu.”

Kwa usalama wake, niliondoa jina la hospitali na nafasi yake halisi hapo.
 
Back
Top Bottom