Dingswayo
JF-Expert Member
- May 26, 2009
- 4,019
- 2,923
Mbunge wa Segerea (CCM), jijini Dar es Salaam Dk. Makongoro Mahanga, amesema bado CCM haijajivua gamba na ameitahadharisha kuwa isipojisafisha na tope la rushwa na ufisadi kama ilivyoagizwa na Halmasahuri Kuu (NEC) itapigwa mweleka kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.
Amesema kupungua kwa kura za urais mwaka jana ni kielelezo kuwa chama kinaweza kuanguka hivyo jitihada za makusudi zinahitajika kwa ajili ya kukinusuru.
Aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati akizungumza na wanachama wa chama hicho tawi la Ugombolwa kata ya Segerea, ambayo inaongozwa na diwani wa Chadema.
Hii si dalili nzuri hata kidogo na wala tusijidanganye kuwa CCM itatawala milele na tukalala, makundi bado yako tuyavunje maana haya yakiendelea tujue mwaka 2015 tutapigwa mweleka, alisema Dk. Mahanga ambaye pia ni Naibu Waziri wa Kazi na Ajira.
Alisema mwaka 2005 chama hicho kilipata ushindi wa kimbunga wa asilimia zaidi ya 80 kwa nafasi ya urais, lakini kushuka hadi asilimia 61 mwaka jana ni dalili ya hatari kubwa mbele ya safari.
Tujiulize, mwaka 2005 tulipata asilimia zaidi ya 80, mwaka 2010 asilimia 61, je mwaka 2015 tukishuka na kupata asilimia 40 kutakuwa na chama hapo jamani, kwa hiyo tusibweteke na kuona hii asilimia 20 iliyopongua uchaguzi wa mwaka jana kuwa ni ndogo, alisema Dk. Mahanga.
Ndugu zangu tufanye kazi la sivyo mambo yatazidi kuharibika huko tuendako, mnakumbuka uchaguzi wa mwaka jana hapa palikuwa hapatoshi, mimi mwenyewe nimeshinda kwa hatihati, katika asilimia za ushindi wa nafasi ya ubunge, jimbo letu la Segerea liko nafasi ya tatu kutoka chini, maana nilimshinda mpinzani wangu kwa kura 4,000, tu inamaana hawa wapinzani wangeungana nisingekuwa mbunge leo, alisema.
Dk. Mahanga alisema kuna wanachama wa chama hicho wamekuwa na chuki zisizo na kikomo ingawa mchakato wa uchaguzi ulishamalizika na ndio wanakihujumu chama.
Makundi wakati wa kura za maoni ndani ya chama ruksa, maana kila mtu anakuwa na wapambe wake, lakini nilipopitishwa na NEC mlipaswa kumaliza makundi, cha kushangaza humu humu CCM kuna watu walikuwa wamenuna na inaonekana walikuwa wanashabikia upinzani, na wakasababisha uchaguzi kuwa mgumu sana alisema.
Alisema hatua ya sekretarieti kuu kujiuzulu na kuwekwa mpya si kujivua gamba kwani huo ni mwanzo wa kuelekea kujivua gamba na isitafsiriwe kuwa mambo sasa yameshanyooka.
Alisema kujivua gamba ni pale ambapo viongozi watajirekebisha na kuhakikisha chama hakipati tena tuhuma za ufisadi.
"Kuondoka kwa Makamba (Yusuf) na ujio wa Katibu Mkuu mpya Mukama (Wilson) si kwamba ndo tumeshajivua gamba, hapana huo ni mwanzo wa safari tunapaswa kujirekebisha kuokoa chama chetu," alisema.
Kadhalika, Dk. Mahanga alisema kujivua gamba kwa chama hicho si kufukuzana ndani ya chama kama wanavyodhani baadhi ya watu bali ni kujirudi na kujirekebisha kwa wanachama wote wa chama hicho.
Alisema dhana pana na ya ukweli ya kujivua gamba ni wanaCCM wote kujiuliza, kujirudi na kujirekebisha na kuwa na mtazamo chanya wa kukijenga upya chama hicho.
Alisema tatizo lingine ambalo lilikiathiri chama hicho mwaka jana na ambalo lilizungumzwa kwa kirefu kwenye mkutano wa NEC Dodoma ni rushwa na ufisadi.
Alisema NEC iliazimia kuwa sasa ni wakati mwafaka wa chama kujisafisha kutoka kwenye tope la rushwa na ufisadi.
CHANZO: NIPASHE
Amesema kupungua kwa kura za urais mwaka jana ni kielelezo kuwa chama kinaweza kuanguka hivyo jitihada za makusudi zinahitajika kwa ajili ya kukinusuru.
Aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati akizungumza na wanachama wa chama hicho tawi la Ugombolwa kata ya Segerea, ambayo inaongozwa na diwani wa Chadema.
Hii si dalili nzuri hata kidogo na wala tusijidanganye kuwa CCM itatawala milele na tukalala, makundi bado yako tuyavunje maana haya yakiendelea tujue mwaka 2015 tutapigwa mweleka, alisema Dk. Mahanga ambaye pia ni Naibu Waziri wa Kazi na Ajira.
Alisema mwaka 2005 chama hicho kilipata ushindi wa kimbunga wa asilimia zaidi ya 80 kwa nafasi ya urais, lakini kushuka hadi asilimia 61 mwaka jana ni dalili ya hatari kubwa mbele ya safari.
Tujiulize, mwaka 2005 tulipata asilimia zaidi ya 80, mwaka 2010 asilimia 61, je mwaka 2015 tukishuka na kupata asilimia 40 kutakuwa na chama hapo jamani, kwa hiyo tusibweteke na kuona hii asilimia 20 iliyopongua uchaguzi wa mwaka jana kuwa ni ndogo, alisema Dk. Mahanga.
Ndugu zangu tufanye kazi la sivyo mambo yatazidi kuharibika huko tuendako, mnakumbuka uchaguzi wa mwaka jana hapa palikuwa hapatoshi, mimi mwenyewe nimeshinda kwa hatihati, katika asilimia za ushindi wa nafasi ya ubunge, jimbo letu la Segerea liko nafasi ya tatu kutoka chini, maana nilimshinda mpinzani wangu kwa kura 4,000, tu inamaana hawa wapinzani wangeungana nisingekuwa mbunge leo, alisema.
Dk. Mahanga alisema kuna wanachama wa chama hicho wamekuwa na chuki zisizo na kikomo ingawa mchakato wa uchaguzi ulishamalizika na ndio wanakihujumu chama.
Makundi wakati wa kura za maoni ndani ya chama ruksa, maana kila mtu anakuwa na wapambe wake, lakini nilipopitishwa na NEC mlipaswa kumaliza makundi, cha kushangaza humu humu CCM kuna watu walikuwa wamenuna na inaonekana walikuwa wanashabikia upinzani, na wakasababisha uchaguzi kuwa mgumu sana alisema.
Alisema hatua ya sekretarieti kuu kujiuzulu na kuwekwa mpya si kujivua gamba kwani huo ni mwanzo wa kuelekea kujivua gamba na isitafsiriwe kuwa mambo sasa yameshanyooka.
Alisema kujivua gamba ni pale ambapo viongozi watajirekebisha na kuhakikisha chama hakipati tena tuhuma za ufisadi.
"Kuondoka kwa Makamba (Yusuf) na ujio wa Katibu Mkuu mpya Mukama (Wilson) si kwamba ndo tumeshajivua gamba, hapana huo ni mwanzo wa safari tunapaswa kujirekebisha kuokoa chama chetu," alisema.
Kadhalika, Dk. Mahanga alisema kujivua gamba kwa chama hicho si kufukuzana ndani ya chama kama wanavyodhani baadhi ya watu bali ni kujirudi na kujirekebisha kwa wanachama wote wa chama hicho.
Alisema dhana pana na ya ukweli ya kujivua gamba ni wanaCCM wote kujiuliza, kujirudi na kujirekebisha na kuwa na mtazamo chanya wa kukijenga upya chama hicho.
Alisema tatizo lingine ambalo lilikiathiri chama hicho mwaka jana na ambalo lilizungumzwa kwa kirefu kwenye mkutano wa NEC Dodoma ni rushwa na ufisadi.
Alisema NEC iliazimia kuwa sasa ni wakati mwafaka wa chama kujisafisha kutoka kwenye tope la rushwa na ufisadi.
CHANZO: NIPASHE