Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,174
Uchaguzi umekwisha, tuchape kazi - Mahanga
na Mwandishi wetu
MBUNGE wa Jimbo la Segerea, Makongoro Mahanga (CCM), amewataka wananchi na viongozi waache kutumia muda mwingi kuzungumzia masuala ya uchaguzi mkuu uliopita bali wajikite kwenye shughuli za maendeleo.
Mahanga alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki jijini Dar es salaam alipokuwa akiwashukuru wananchi wa Kata ya Kiwalani kwa kumchagua kuwa mbunge pamoja na kuwachagua madiwani wa CCM katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 30 mwaka jana.
Alisema kuwa viongozi waliochaguliwa wana wajibu mkubwa wa kutekeleza majukumu yao na ahadi walizozitoa wakati wa kampeni.
Aliongeza kuwa pamoja na wajibu huo ni vema hivi sasa wananchi kwa kushirikiana na viongozi waliochaguliwa wakajikita katika shughuli za maendeleo badala ya kujikita kwenye malumbano ya uchaguzi.
Alisema atahakikisha anakuwa mstari wa mbele kushirikiana na wananchi bila kujali tofauti za kiitikadi kwa kuwa kiongozi yeyote anapochaguliwa hapaswi kuwabagua wapigakura.
Sitabagua mtu yeyote eti kwa kuwa hakunipigia kura, maendeleo hayawezi kupatikana kwa namna hiyo, uchaguzi umekwisha tuache porojo zake, tuchape kazi, alisema.
Mahanga, alisema wananchi wamewaamini viongozi walioko madarakani hivi sasa hivyo ni busara kwa viongozi hao kuwatumikia ili kutovunja imani iliyoonyeshwa kwao.
Naye Khadija Juma, mkazi wa Kiwalani, alisema kama viongozi walioko sasa hawatajikita katika kutatua kero za wananchi mwaka 2015 wasihangaike kuomba kura.
na Mwandishi wetu
Mahanga alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki jijini Dar es salaam alipokuwa akiwashukuru wananchi wa Kata ya Kiwalani kwa kumchagua kuwa mbunge pamoja na kuwachagua madiwani wa CCM katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 30 mwaka jana.
Alisema kuwa viongozi waliochaguliwa wana wajibu mkubwa wa kutekeleza majukumu yao na ahadi walizozitoa wakati wa kampeni.
Aliongeza kuwa pamoja na wajibu huo ni vema hivi sasa wananchi kwa kushirikiana na viongozi waliochaguliwa wakajikita katika shughuli za maendeleo badala ya kujikita kwenye malumbano ya uchaguzi.
Alisema atahakikisha anakuwa mstari wa mbele kushirikiana na wananchi bila kujali tofauti za kiitikadi kwa kuwa kiongozi yeyote anapochaguliwa hapaswi kuwabagua wapigakura.
Sitabagua mtu yeyote eti kwa kuwa hakunipigia kura, maendeleo hayawezi kupatikana kwa namna hiyo, uchaguzi umekwisha tuache porojo zake, tuchape kazi, alisema.
Mahanga, alisema wananchi wamewaamini viongozi walioko madarakani hivi sasa hivyo ni busara kwa viongozi hao kuwatumikia ili kutovunja imani iliyoonyeshwa kwao.
Naye Khadija Juma, mkazi wa Kiwalani, alisema kama viongozi walioko sasa hawatajikita katika kutatua kero za wananchi mwaka 2015 wasihangaike kuomba kura.