Mahakama yatoa hati ya kumwita Mbowe na wenzake leo kuendelea na kesi

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,502
9,282
Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi imetoa hati kumwita Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na wenzake watatu kuendelea kusikiliza kesi ya uhujumu uchumi inayowakabili.

Mbowe na wenzake wanatakiwa kuwa mahakamani hapo leo baada ya kesi yao kusimama kwa siku nne kutokana na Jaji Elinaza Luvanda kujitoa kuisikiliza. Jaji huyo alijitoa Jumatatu baada ya washtakiwa kutokuwa na imani naye kwamba hawaamini kama atawatendea haki baada ya kutupilia mbali mapingamizi waliyoweka.

Mahakama sasa imemteua Jaji Mustapha Siyani kusikiliza kesi hiyo. Kwa mujibu wa hati ya wito, kesi itaendelea leo mahakamani hapo

Mwananchi
 
je atamkataa na huyo?
Wote ni wale wale tu. Hakuna uhuru wa Mahakama nchi hii.

Jaji makini hawezi kuendelea na kesi batili. Tunajua atazuga aonekane yuko neutral kutokana na malalamiko ya watu ila hatokuwa na tofauti unless wameamua vinginevyo.
 
Kesi hadi sasa hivi haina hati genuine ya mashtaka na ndiyo maana Mahakama imetoa hati ya wito sababu wanajua yupo nyumbani kwake na si gelezani.

Leo ndio atasomewa mashitaka upya kwa hati mpya !! sasa jiulize toka majuzi alishikiwaje kwa kosa lipi? wakati hati haipo mahakamani.
 
Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi imetoa hati kumwita Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na wenzake watatu kuendelea kusikiliza kesi ya uhujumu uchumi inayowakabili.

Mbowe na wenzake wanatakiwa kuwa mahakamani hapo leo baada ya kesi yao kusimama kwa siku nne kutokana na Jaji Elinaza Luvanda kujitoa kuisikiliza. Jaji huyo alijitoa Jumatatu baada ya washtakiwa kutokuwa na imani naye kwamba hawaamini kama atawatendea haki baada ya kutupilia mbali mapingamizi waliyoweka.

Mahakama sasa imemteua Jaji Mustapha Siyani kusikiliza kesi hiyo. Kwa mujibu wa hati ya wito, kesi itaendelea leo mahakamani hapo

Mwananchi
Safi sn
 
Kuna kesi gani hapo zaidi uzushi?
kwa hiyo mmesha amua kabla hata mahakama haijafanya kazi yake?!
Mbona wafuasi wa Mbowe mnayumba sana?
Mara hamna imani na Jaji, mara ohhh hakuna kesi hapo ni uzushi!
wananchi tunataka kusikiliza hiyo kesi ili tujue siri zilizo kuwa zinafanywa kwa siri.
tuache mahakama ifanye jukumu lake.
 
kwa hiyo mmesha amua kabla hata mahakama haijafanya kazi yake?!
Mbona wafuasi wa Mbowe mnayumba sana?
Mara hamna imani na Jaji, mara ohhh hakuna kesi hapo ni uzushi!
wananchi tunataka kusikiliza hiyo kesi ili tujue siri zilizo kuwa zinafanywa kwa siri.
tuache mahakama ifanye jukumu lake.
MATAGA siku zote ni kujitoa ufahamu tuuu!!! Una maana huelewi?
 
Kitu ambacho watu hawajui ni kwamba tumesahau katiba. Ambalo ndo lengu kuu la kumtia hatiani Mbowe. Siku wakiona inafaa watafuta kesi, tutashangilia kumbe lengo limekamilika
 
Kesi hadi sasa hivi haina hati genuine ya mashtaka na ndiyo maana Mahakama imetoa hati ya wito sababu wanajua yupo nyumbani kwake na si gelezani.

Leo ndio atasomewa mashitaka upya kwa hati mpya !! sasa jiulize toka majuzi alishikiwaje kwa kosa lipi? wakati hati haipo mahakamani.
Bwege kabisa. Utaratibu ni kwamba akija jaji mpya anatakiwa aitishe faili husika upya. Ndio maana kaitwa
 
Bwege kabisa. Utaratibu ni kwamba akija jaji mpya anatakiwa aitishe faili husika upya. Ndio maana kaitwa
jibu hoja badala ya matusi, Ni hati ipi ilimshikilia Mbowe tangu majuzi baada ya ile ya kwanza Jaji kuitolea ruling kwamba ni Void.
 
Back
Top Bottom