Mahakama yatoa hati Masogange asakwe na akamatwe

Queen V

JF-Expert Member
Jan 19, 2012
776
1,330
agnes-masogange-2.jpg

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imetoa hati ya kumkamata msanii, Agnes Gerald maarufu kama Masogange kwa kushindwa kuhudhuria kwenye kesi ya kutumia dawa za kulevya inayomkabili.

Hati hiyo ilitolewa jana mbele ya Hakimu Mkazi mkuu, Wilbroad Mashauri, wakati kesi hiyo ilipotajwa.

masogange-agness.jpg


Wakili wa Serikali, Adolf Mkini alidai mahakamani hapo kwamba upelelezi wa kesi hiyo upo hatua za mwisho, lakini mshtakiwa, wadhamini wake na wakili wake hawakufika hivyo wakili Nkini akaomba mahakama itoe hati ya kumkamata mshtakiwa huyo kwa sababu ni mara ya pili ameshindwa kufika mahakamani hapo.

Hakimu Mashauri alikubali maombi ya wakili wa Serikali na kutoa hati ya kumkamata mshtakiwa ambaye ni Masogange.

Msanii huyo aliwahi kuonywa akitakiwa aheshimu mahakama kutokana na kutokuwapo kwenye kesi yake ilipotajwa.

Katika kesi hiyo namba 77 ya mwaka 2017, Masogange anadaiwa kuwa kati ya Februari 7 na 14 mwaka huu, katika maeneo yasiyojulikana ndani ya jiji la Dar es Salaam, alitumia dawa za kulevya aina ya heroin(Diacety Imophine). Pia inadaiwa kati ya Februari 7 na 14, 2017 alitumia dawa za kulevya aina ya oxazepam.


Chanzo: Mtanzania

=====

Mfululizo wa kukamatwa, kesi, hukumu na kuachiwa huru kwa Agnes Masogange kwenye kesi ya Madawa ya kulevya
Masogange ajisalimisha mwenyewe Mahakama a Kisutu
Kupandishwa kizimbani na kusomewa shitaka
Yaliyojili wakati wa kesi ya Masogange
Masogange kupelekwa kwa Mkemia Mkuu
Kesi kusikilizwa
Tetesi za kuachiwa huru
Hukumu
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imetoa hati ya kumkamata msanii, Agnes Gerald maarufu kama Masogange kwa kushindwa kuhudhuria kwenye kesi ya kutumia dawa za kulevya inayomkabili.

Hati hiyo ilitolewa jana mbele ya Hakimu Mkazi mkuu, Wilbroad Mashauri, wakati kesi hiyo ilipotajwa.

Wakili wa Serikali, Adolf Mkini alidai mahakamani hapo kwamba upelelezi wa kesi hiyo upo hatua za mwisho, lakini mshtakiwa, wadhamini wake na wakili wake hawakufika hivyo wakili Nkini akaomba mahakama itoe hati ya kumkamata mshtakiwa huyo kwa sababu ni mara ya pili ameshindwa kufika mahakamani hapo.

Hakimu Mashauri alikubali maombi ya wakili wa Serikali na kutoa hati ya kumkamata mshtakiwa ambaye ni Masogange.

Msanii huyo aliwahi kuonywa akitakiwa aheshimu mahakama kutokana na kutokuwapo kwenye kesi yake ilipotajwa.

Katika kesi hiyo namba 77 ya mwaka 2017, Masogange anadaiwa kuwa kati ya Februari 7 na 14 mwaka huu, katika maeneo yasiyojulikana ndani ya jiji la Dar es Salaam, alitumia dawa za kulevya aina ya heroin(Diacety Imophine). Pia inadaiwa kati ya Februari 7 na 14, 2017 alitumia dawa za kulevya aina ya oxazepam.


Chanzo: Mtanzania

Hivi wanajuaje kama alitumia kati ya tarehe hizo
 
Hizi ndizo dharau alizofanyiwa Mwakyembe!!
 

Attachments

  • 11835308_1148847975141970_416717682_n.mp4
    936 KB · Views: 21
  • Thanks
Reactions: SDG
Dah.....Bashite hajasoma vizuri,kaiba vyeti,kampiga mzee warioba kaiba simu ndani ya bunge la katiba lakini anatumbua hilo limzigo kwa kutumia cheo chake cha uRC ....bongo bwana!
sasa hata mahawara zake wanakula bata hakuna aliye juu yake.
 
Kwa mwendo ule WA kidondora hata Mimi sikuachi wacha nifukuzwe hata kazi yaani nitavyokulamba hata mwana mbuzi aliyetoka kuzaliwa anasubiri hasa pachuchi na ule wekundu WA nyanya na najaribu kufumba macho kuvuta hisia na ile radha ya ugwadu mithili ya mtindi duh sibanduki kama ruba kweli bashite anafaidi...
 
Back
Top Bottom