Mahakama watishia kugoma

Mtabiri

Senior Member
Jun 23, 2009
152
4
ONGEZEKO la mishahara ya majaji na mahakimu, limeibua mgogoro unatokana na watumishi wa idara hiyo ambao si mahakimu, kuipa serikali muda wa siku 60, kurekebisha viwango vyao vya mishahara vinginevyo, wataendesha mgomo nchi nzima. Waraka huo unaonyesha kuwa kiwango cha mshahara wa hakimu wa mahakama ya mwanzo daraja la kwanza, umepanda kutoka Sh193,340 hadi kufikia Sh400,000 wakati mishahara ya majaji imepanda kutoka Sh2,160,000 hadi kufikia Sh3,645,000. Source: http://mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=14998
 
wana haki kugoma kani bila wao hakimu au jaji hawezi tenda kazi yake vizuri.
 
hiyo ndivyo tz ilivyo. Hata ktk idara ya afya ukiangalia gap lililoko kati ya madaktari na hao watumishi wengine utaona huruma! Ila wangepandisha mishahara kwa idara nzima. Kama ni idara ya mahakama basi wapandishwe wote kuanzia mfagiaji hadi judge, kama ni idara ya afya vivyo hivyo, kama ni idara ya elimu basi wakiwaongeza walimu waongeze mpaka kwa wale wanaotunza mazingira ya shule na maabara. Kutofanya hivyo ni kuleta conflict/chuki baina ya watendaji walioko ktk sehemu/ofisi moja. Hakimu na karani wa mahakama wanafanya kazi mazingira hayo hayo(rushwa etc wanashawishika wote) kwanini uongeze mshahara wa hakimu peke yake? Kama kigezo ni elimu yake basi ongezeni kwa kufuata elimu hiyo(eg.degree) kwa watumishi wote wa serikali kwa kiwango sawa! Kwani mahakamu ndio wanaofanya kazi zaidi ya idara zingine zote? walimu,madaktari,maaskari,wahasibu, na wengine hawana mchango ktk maendeleo ya nchi hii au vipi?
 
migomo ,watu kulala barabarani na kufunga njia ni dalili mbaya sana katika uongozi wa taifa na kwa kweli uongozi makini popote duniani hauwezi kuruhusu hali kama hii iendelee.Lakini Tanzania ya leo ,viongozi hawana habari ndo kwanza wanatukataza tusivae suti bali tuvae batiki
 
migomo ,watu kulala barabarani na kufunga njia ni dalili mbaya sana katika uongozi wa taifa na kwa kweli uongozi makini popote duniani hauwezi kuruhusu hali kama hii iendelee.Lakini Tanzania ya leo ,viongozi hawana habari ndo kwanza wanatukataza tusivae suti bali tuvae batiki

Hili nalo litagomewa?.
Mashangingi yalikatazwa, mbona bado yananunuliwa sembuse kuvaa ile kitu wewe nataka?!
 
hiyo ndivyo tz ilivyo. Hata ktk idara ya afya ukiangalia gap lililoko kati ya madaktari na hao watumishi wengine utaona huruma! Ila wangepandisha mishahara kwa idara nzima. Kama ni idara ya mahakama basi wapandishwe wote kuanzia mfagiaji hadi judge, kama ni idara ya afya vivyo hivyo, kama ni idara ya elimu basi wakiwaongeza walimu waongeze mpaka kwa wale wanaotunza mazingira ya shule na maabara. Kutofanya hivyo ni kuleta conflict/chuki baina ya watendaji walioko ktk sehemu/ofisi moja. Hakimu na karani wa mahakama wanafanya kazi mazingira hayo hayo(rushwa etc wanashawishika wote) kwanini uongeze mshahara wa hakimu peke yake? Kama kigezo ni elimu yake basi ongezeni kwa kufuata elimu hiyo(eg.degree) kwa watumishi wote wa serikali kwa kiwango sawa! Kwani mahakamu ndio wanaofanya kazi zaidi ya idara zingine zote? walimu,madaktari,maaskari,wahasibu, na wengine hawana mchango ktk maendeleo ya nchi hii au vipi?

Rushwa haitamalizwa kwa kuongeza mshahara maana hizo lakini nne hazimzuii kupokea milioni, Milion nne hazimkatazi/hazimzuii kupokea milion kumi etc.
Katika nchi iliyojaa ufisadi wa kutisha, kadiri mtu anavyoongeza kipato, ndivyo matanuzi yake yanavyoongezeka na kuhitaji nyingi pesa zaidi.Hili linafanya mwenye tabia ya kupokea rushwa kuomba kiwango kikubwa zaidi.Cha msingi ni kuhakikisha kuwa wafanyakazi wote wanalipwa mshahara wa kutosha kuishi ( living wage).
 
migomo ,watu kulala barabarani na kufunga njia ni dalili mbaya sana katika uongozi wa taifa na kwa kweli uongozi makini popote duniani hauwezi kuruhusu hali kama hii iendelee.Lakini Tanzania ya leo ,viongozi hawana habari ndo kwanza wanatukataza tusivae suti bali tuvae batiki

Unafikiri wanalijua hilo? TZ that is part and parcel of life kuanzia kwa wanafunzi mpaka kwa watumishi. Madaktari na walimu ni migomo kila mara lakini no body takes that thing serious na sasa hiyo inaenda kwa mahakama! Hivi tunaenda wapi?
 
Back
Top Bottom