Mahakama na kesi za UHUJUMU UCHUMI (UFISADI)!

Nnauye Jr

Nafikiri ujumbe wako unagusa sana kesi inayowakabili mawaziri wa zamani Daniel Yona na Basil Mramba... Hivi ina miaka mingapi sasa?
 
Last edited by a moderator:
Yaani akili yako ndo imeishia hapo? Uelewe kuwa haki inayoharakishwa inaweza kuwa haki inayofanywa kwa kulipua, hivyo utampa mwanya yule mshitakiwa kukata rufaa na kushinda, pia kesi zinazoendeshwa si hizo tu, kuna watu wengine wa makosa ya kawaida tu wamekaa ndani miaka mingi, wanahitaji na wao kesi zao ziende haraka, ukiona kesi ya mkurugenzi pekee ndo iende haraka halafu ya mkulima aliyeacha watoto saba kijijini iende polepole utakuwa una ubaguzi kwa wananchi, kwasababu kwa yule mkulima watoto wanamtegemea, kumbe yule mkurugenzi ana mapesa kwenye account waifu anaenda tu ATM kuchukua na kununua vitu watoto hawalali njaa.

Pia maslahi ya mahakimu na wanasheria wa serikali ni madogo sana. kingine ni kwamba kesi ni nyingi mno, na mahakimu wachache sana, pia waendesha mashitaka wachache, amini usiamini hadi leo ofisi za attorney General hazijasambaa mikoa yote, achilia wilayani kote hakuna ofisi hizi kwasababu serikali haina pesa kuajili.

Hivyo maeneo mengi sana waendesha mashitaka wanakuwa polisi ambao hawana elimu ya sheria vizuri na ajabu ni kwamba wao wenyewe ndo wakamataji na wao ndo washitaki kitu ambacho kinaleta conflict of interest sana, na polisi wote usimwamini hata mmoja, ukiwahonga hata elfu mbili wanakubali, nao ni kwasababu maslahi yao ni madogo mno..kuna mambo mengi yanayosababisha kesi kuchelewa ningeandika hapa ningejaza page yote.
 
nakupongeza kwa kuona hili
ongezeni basi bajeti ktk mahakama na boresheni mishahara ya mahakimu na majaji
wapeni na nyenzo zote stahiki za kufanyia kazi
na pia sheria zibadilishwe kama cilvi procedure na criminal procedure
yapo mengi ya kuondoa ktk hizi sheria na pia advocate ordinance..act nayo ifanyiwe marekebisho ili kuwe na kipengele cha penalty kwa mawakili wazembe
mkiweza haya wewe na serikali ya chama chako mtakuwa mmesaidia watanzania wengi
Iko haja ya kuangalia upya mfumo wa mahakama zetu! Kesi za utumiaji mbaya wa madaraka, rushwa, ufisadi na uhujumu uchumi zisichukue muda mrefu bila kutolewa maamuzi. Kwanza ni hasara kwa serikali na nchi na haitoi mafunzo kwa kizazi kichanga kuona kuwa haya ni matendo maovu katika jamii!

Kama tumeweza kuwa na utaratibu wa kushughulikia kesi za uchaguzi ndani ya muda flani kwanini tushindwe kwenye kesi hizi za uhujumu uchumi?!. Chukua mfano wa Mkurugenzi ambaye amesimamishwa kazi na kupelekwa mahakamani kwa ubadhirifu, kesi ikiendelea kwa miaka sita , anaendelea kupokea mshahara, tunalipa mawakili wa serikali, mtuhumiwa ana dunda tu barabarani!! Ipo haja ya kuangalia upya mfumo wa kushughulikia kesi za namna hii!..

Ziko taarifa za kesi za wakurugenzi wa wilaya ambao wako mahakamani toka mwaka 2004 maana yake ni zaidi ya miaka nane sasa wako mahakamani tu na kesi zinaendeshwa kwa muda wote huu. Ukiacha hasara kwa serikali na Taifa, ukiacha sura mbaya kwa kizazi kichanga/ kipya, hivi kwanini kesi hii ichukue miaka zaidi ya nane? Ushahidi gani unaosumbua kuhukumu?!! Mwisho wa siku anashinda kesi anaidai serikali.... Huu nao ni ufisadi mwingine.
 
Back
Top Bottom