Mahakama kwa kulinda Integrity na Trust ya Mahakama itisheni faili ya Kesi ya CHADEMA inayosimamiwa na Jaji Hamidu mfanye mapitio

Mahakama kwa kulinda Integrity na Trust ya Mahakama itisheni faili ya Kesi ya CHADEMA inayosimamiwa na Jaji Hamidu mfanye mapitio

Lord Denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
23,494
Reaction score
57,869
Nakujua vizuri wewe ni msabato safi unayependa Haki pamoja na mapungufu yako kama binadamu.

Sidhani kama mnajua picha mnayojenga Mhimili wa Mahakama hasa kwenye kuaminika na kutenda Haki kwa Wananchi na Wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kutokana na mwenendo mliokuwa nao miaka ya hivi karibuni hasa kipindi hichi cha sasa.

Sidhani kama mnaona kama kwa kadri Mhimili wa Mahakama unavyoonesha kuwa compromised basi suala hili linawachochea Wananchi kuanza kufikiria njia sisizo za Kisheria katika kutafuta Haki

Tunaomjua Jaji Hamidu Mwanga hatushangazwi na haya maamuzi yake. Ni mtu wa kujisikia, kupenda kuonyesha ubabe, mdini na Kujifanya yeye ni system na kupenda kukomoa. Hii ni hulka yake na kila siku huwa nashangaa ilikuwaje akawa Jaji. Ni vile tu mifumo yetu ya Vetting imekufa maana kigezo kikuu cha Mtu kuwa Jaji kwenye nchi zenye ustaarabu sio kisomo tu ila ni Hekima na Busara. Nisiende sana huko, hapa leo nazungumzia Kesi anayosimamia dhidi ya Bodi ya Wadhamini wa Chadema.

Inawezekana mkawa hamuoni bomu mnalolitengeneza mbele, ila ushauri wangu. Itisheni faili la hii kesi anayosimamia Jaji huyu na mfanye mapitio iki kuhakikisha Haki inatendeka kwa Chadema.

Pia soma > GE2025 - Jaji Hamidu Mwanga akataa kujitoa kwenye kesi ya CHADEMA
 
nawashangaa watu wanaohusika (moja kwa moja) na Usalama wa Taifa wako kimya wanaangalia tu mhimili wa kutoa haki unachezewa. Hali hii ni ya hatari sana. Je wao hawalioni hilo?

Taifa ambalo Mahakama haziaminiki sio taifa hilo

JESUS IS LORD&SAVIOR
 
Tunakaribisha Colombia na Haiti ijayo , watu watajiamlia kufanya jambo sababu wanajua Mahakamani hakuna haki , hili hata Makonda akiwa Mwenezi CCM aliwahi Kusema kuwa Mahakama za Tanzania hazitendi haki
 
Back
Top Bottom