Uchaguzi 2020 Magufuli Tunamuhitaji sana ila hawa wabunge wa CCM wengi hatuwahitaji kabisa

Zero Hours

JF-Expert Member
Apr 1, 2011
12,944
18,654
Naomba nianze na kudeclare interest. Mimi sio mshabiki wa CCm wala Magufuli. Ni mshabiki wa vyama vingi. Napenda utawala wenye viongozi wenye maono au challenge mbalimbali.

Tunavyoelekea uchaguzi mkuu mwaka huu. Naomba nitoe mapendekezo binafsi kwa watanzania wenzangu tunaojiandaa kushiriki uchaguzi wa viongozi wetu.

Utawala wa Rais Magufuli ni utawala wenye Mazuri mengi huku mabaya nayo yakiwa mengi. Maana yake anahitaji kukosolewa na kushauriwa sana.

Kitu nachoweza sifia utawala huu ni kuweza kusimamia rasilimali za nchi hii ili kukuza uchumi wa Tanzania. Kweli tumeona maendeleoa mengi yamefanyika.

Hii maana yake Watanzania Tunamuhitaji Magufuli sana aendelee kuwepo ili Tupate manufaa ya Utawala wake. ( Simaanishi aendelee kutawala zaidi ya miaka 10)

Ila tatizo linakuja kwenye Hawa wabunge wa CCM. Wengi ni Pasua kichwa. Sioni wanachomsaidia Rais Magufuli zaidi ya Kumsifia na kumtukuza ilimradi waendelee kukaa kwenye viti vyao vya ubunge au wapate teuzi mbali mbali.

Wabunge wa CCM sasa wamebadilisha Mbinu ya kuendelea kukaa madarakani. Badala ya kutetea wananchi na kupigania maendeleo katika majimbo yao. Wamebaki kuwa waimba mapambio tu bungeni na Kutukana wapinzani wakiongozwa na spika wao wa bunge ambye ninamashaka sana kama psychologically yupo vizuri

Mh Rais, Unahitaji wabunge wa Upinzani sana kuliko hawa wa chama chako. Hawakusaidii chochote zaidi ya kukupaka mafuta kwa mgongo wa chupa ili waendelee kula tena wengi wanatafuta mianya ya kukuibia tu.

Wananchi nao hatuoni utendaji wa hawa wabunge, nje na ndani ya Bunge. Kwa kifupi hawa wabunge wapo bungeni lakini hawajuu wajibu wao kama wabunge.

Kazi kuu za Bunge ni:

1) Kumhoji waziri yeyote kuhusu masuala ya umma yaliyo ndani ya dhamana yake katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
2) Kujadili utendaji wa kila wizara wakati wa kikao cha mwaka cha Bunge la bajeti;
3)Kujadili na kuidhinisha mpango wowote wa muda mrefu au mfupi unaotakiwa kutekelezwa katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
4)Kutunga Sheria pale ambapo utekelezaji unahitaji sheria na;
5) Kujadili na kuridhia mikataba na makubaliano ambayo Jamhuri ya Muungano ni mhusika na masharti yake yanahitaji idhini.

Wananchi wenzangu nawashauri Tukienda kwenye uchaguzi, tuhakikishe Rais Magufuli Tunampa kura zote ila wabunge mizigo wengi tuwakate mapema. Hatuhitaji Bunge lenye sauti moja ni bora lisiwepo kabisaa posho zao zikafanya maendeleo mengine.
 
Kama unamhitaji nenda kanywe nae chai,acha kujizungusha zungusha
 
Ukipenda boga....... Usimpompatia wabunge wa kutosha anaweza kushindwa kufanya anayokusudia kuyafanya kwani yatakwama bungeni, Wabunge waliopo yafaa waendelee maana hawajamkwamisha rais! si unajua bolt na nut lazima viwe na uwiano sahihi!
 
Zero Hours,

October hakuna cha magufuri wala nn...mwaga pombe na imwage na ccm yake. Kifupi hakuna mzr ndani ya CCM. Hatuhitaji rais asiyejitambua. Hatuhitaji rais mtekaji, hatuhitaji rais mvunja katiba, atuhitaji rais ambaye hajuu umuhimu wa mashirikiano ya kimataifa. October tunachinja kuanzia rais hadi diwani wa CCMmwisho kbs hatumhitaji rais dikteta na magufuri anasifa za udikteta...chonde chonde October tusirudie makosa ndg zangu, tuseme imetosha imetosha imetoshaaaaaaa
 
Lakini hata wapinzani wawe watu wa kujielewa.haiwezekani wanakuwa watu wa kupinga mambo ya maendeleo ya nchi.
 
Maendeleo gani?? Kuteka na kuua ni maendeleo??? Kubaka katiba ni maendeleo???
Hata wewe nadhani unaona maendeleo.kikubwa ni kwamba huwezi kuridhisha watu woote.lakini mambo ya msingi kama nchi Rais Magufuli anasimamia vema.
 
Hata wewe nadhani unaona maendeleo.kikubwa ni kwamba huwezi kuridhisha watu woote.lakini mambo ya msingi kama nchi Rais Magufuli anasimamia vema.
Hakuna kitu mazeee, hata ww huyaoni seme tu ndo lazima usifie ili mkono uende kinywani..bk 7 oyeeee
 
Hata mimi maono ya JPM nayakubali sana, ila JPM mwenyewe simpendi maana amefeli.
1. Kashindwa kumuondoa bashite,
2. Anapoteza muda mwingi sana na wapinzani tena ambao hata nguvu ya kumshinda hawana, we unadhani mwaka huu kuna mtu wa upinzani mwenye uwezo wa kumtoa JPM kweli? Kihalali anaweza chukua hata 80% ya kura, sema subiri uone wapinzani watakavyosumbuliwa.
3. Amejaa ego sana, akiona kitu wananchi wanataka anafanya tofauti kujionyesha mbabe hata kama anachofanya si sahihi, tuliiona kwa bashite, tumeona kwenye korona.
4. Hasikilizi chochote wanachomshauri, au wanaomshauri wanamuogopa so wanamwambia anachotaka kusikia maana wanajua kichwani alivyo
5. Ana hasira za kijinga, kama kiongozi inabidi awe chill, jiwe akiwa anakuchukia atakukasirikia miaka siku akipata nafasi ya kukuondoa kwisha habari tunakusahau, utasikia umehujumu uchumi au watu wasiojulikana.
6. Haheshimu katiba wala sheria, ya kila kitu ni on the fly tu, anafanya analojisikia
7. Amepanga watu washenzi, viongozi wengi wana mambo ya kijinga awamu hii imegeuka kua comedy, yule tako juzijuzi anasema usipohudhuria msiba upelekwe jela, wengine wanataka mahabusu wafanyishwe kazi, bashite hata sitaki kumuongelea maana ni tako namba moja.

Angekua hana hizi kasoro kura yangu ningempa tena na tena bila hata kufikiria mara mbili, wakimpa Lissu agombee mwaka huu nitampa pamoja na kua siamini watu wote wa CDM maana walijaribu kumsafisha sana Lowassa pamoja na kumpondea miaka nenda rudi.
 
Wabunge balada ya kusema mwaka ujao tutahakikisha wananchi wanaandisha katiba yao mpya na nzuri ili Mh Rais atawale vizuri na kuleta maendeleo wao wanasema watamwongea muda wa kutawala.
Tunae Spika wa Bunge bogus kuliko ata boga yenyewe.
 
Huu uzi umedoda kisa tu kumsifia magufuli. Kweli Mataga wanakazi nzito sana. Hata pesa wanayowqlipa ( buku 7) ni ndogo sana.
Screenshot_20200611-070513_Twitter.jpg
 
Back
Top Bottom