Ni siku chache tu zimepita tangu fagia fagia ilipopita na watu wengine kumwagwa kwenye vyeo na nafasi mbalimbali. Sasa, leo nilikuwa nafanya kazi zangu ofisini, mara napigiwa simu na namba ngeni. Kumbe ni bosi wangu katumia namba ambayo mimi sina. Akaniita kuwa nahitajika kwa bosi mwingine (bosi wake). Mara nikakumbuka ile kauli kuwa siku hizi ukiitwa na bosi unaweza kujiunga na wale wazee wa TRA au Bandari, job inayeyuka fasta bila kutarajia. Aisee, na bosi mwenyewe mkalii, ilibidi nipitie maliwato kwanza kuweka mambo sawa.
Nilipofika kumbe napewa cheo kingine, daaaaaah!!!
Hii Magufuli phobia sijui itaisha lini
Nilipofika kumbe napewa cheo kingine, daaaaaah!!!
Hii Magufuli phobia sijui itaisha lini