Magufuli msikilize huyu Mzungu!

Ndg yangu unatetea mzungu wa maua? Hawa wakulima wa maua WANATAKIWA kufukuzwa kwa sababu hizi;
Wanalipa mshahara mdogo kati ya 100,000 na 150,000/,
Wafanyakazi karibu wote wanaathirika na dawa hadi wengine kupata tb na kufariki ni pamoja na majirani wengi weathirika sana, mfano kitongoji cha magadirisho usa river wengi wanafariki kwa tb kutokana na shamba la lolionndo.
Sababu nyingine maeneo jirani huwa mvua hazinyeshi sawa na maeneo mengine kwani inasadikika hawa jamaa hurusha mabom juu sana hasa isiku na kuitawanya mvua..watu wanaoishi jiran na mashamba haya wanaweza kuthibitisha
 
Ndg yangu unatetea mzungu wa maua? Hawa wakulima wa maua WANATAKIWA kufukuzwa kwa sababu hizi;
Wanalipa mshahara mdogo kati ya 100,000 na 150,000/,
Wafanyakazi karibu wote wanaathirika na dawa hadi wengine kupata tb na kufariki ni pamoja na majirani wengi weathirika sana, mfano kitongoji cha magadirisho usa river wengi wanafariki kwa tb kutokana na shamba la lolionndo.
Sababu nyingine maeneo jirani huwa mvua hazinyeshi sawa na maeneo mengine kwani inasadikika hawa jamaa hurusha mabom juu sana hasa isiku na kuitawanya mvua..watu wanaoishi jiran na mashamba haya wanaweza kuthibitisha


Hata wewe pia kama mwenzako hauelewi capitalistic economic system inavyofanya kazi!
Ni hivi kipato cha mfanyakazi kinaendana na uzalishaji (productivity) yaani jinsi uzalishashaji unavyoongezeka ndivyo kipato kinavyoongezeka na ndio maana kuna nchi za kipato cha chini, cha kati na juu kabisa, ukienda Uchina hapo mwanzo ilikuwa ni nchi ya kipato cha chini wakapiga kazi bila ya kulala na sasa wamepanda na kuwa kipato cha kati na wanaedelea kupiga kazi kuelekea kipato cha juu!
Ukienda Uchina kuna watu wanalala kwenye mabweni asubuhi wanaamkia kazini jioni wanarudi bweni na hawa wametoka vijijini huko lkn wanafanya tena kwa kipato kidogo sana unajua ni kwanini bado wanafanya kazi kwa kujituma? Ni kwa sababu wanajua ili waweze kupata kipato kikubwa ni lazima kwanza waongeze uzalishaji ili kiwanda kiweze kupata fedha zaidi na hakuna njia nyingine!

Sasa wewe unataka mfanyakazi TanZania alipwe kipato cha juu wakati nchi yetu ni ya kipato cha chini hiyo hela ya kulipa hiyo mishahara mikubwa muwekaji ataitoa wapi? Kumbuka huyu aliyewekeza kama ni kiwanda au sijui Hoteli amekopa fedha kwa ajili ya uwekezaji na ni lazima alipe dani, sasa atalipaje deni kama hakuna Uzalishaji?

Hivyo basi ni lazima kwanza sisi kama WatanZania tukubali kujifunga mkanda tufanye kazi kwa mshahara mdogo na kwa bidii bila ya kuchoka ili tuongeze uzalishaji, uzalishaji ukiongezeka ina maana Kampuni/Kiwanda chetu kitakuwa na fedha ambazo sasa inaweza kumudu kutuongeza mshara pmj na mapato mengine ya serikali pia kuendelea kuajili watu!

Hakuna njia nyingine wote hao unawaona kama ni Ujapani, Ulaya au Marekani wamepita huko, huwezi kudai Mshahara mkubwa kwenye nchi kama TanZania ambayo hakuna kitu kinafanya kazi, huyu muwekezaji inabidi atumie jenereta yake kuzalisha Umeme anunue mafuta ya jenereta, akienda Air port hakuna ndege na wakati mwingine maua yanaharibika kwa maana ni lazima yasafirishwe kwa wakati, hakuna Maji inabidi atafute ya kwake kwa kuwa hakuna hiyo miundo mbinu, madawa ambayo anayatumia kwenye mimea yake kama mbolea, au kuuwa vijidudu ni lazima aagize ktk nje ya nchi kwa maana TanZania hakuna mtu anayetengeneza hizo dawa, kwa kifupi ni lazima aimport kila kitu kuanzia viatu, gloves, mpaka nguo za kazi sasa hizo fedha za kulipa mishahara mkubwa atazitoa wapi?
Usisahau pia TanZania watu skilled hakuna au ni wachache sana mtu anamaliza Chuo hakuna anachojua na inabidi wewe mwenye Kampuni uingie gharama ya kumfundisha hii itakuchukuwa miaka 2-3 ili aweze kufanya kazi independently hii yote ni kwa gharama ya muwekezaji sasa hiyo fedha ya kumlipa mfanyakazi mshahara mkubwa itatoka wapi?

Acha tu kuongea kwa hamaki jaribu kuangalia mambo kwa uhalisia wake nchini kwetu ni ngumu sana kufanya biashara na kufanikiwa vizingiti ni vingi sana, jaribu tu hata kufungua ofisi ya stationary, wiki nzima hauna Umeme inakubidi ili uuze utafute jenereta na kununua mafuta sasa hiyo fedha itatoka wapi? Kumbuka hapo umekopa CRDB au TIB na unatakiwa ulipe deni, halafu hapo hapo mfanyakazi anakudai mshahara mkubwa wakati unapata umeme mara mbili au tatu kwa wiki wewe utatoa wapi fedha ya kumlipa mshahara mkubwa?



 
Yaani, kwa vile ni Mzungu ndio lazima akutane na Rais; haya mambo yanahusiana na Wizara ya Kilimo au chombo cha kulobby kuhusu masuala ya kilimo ndio kiwakilishe. Kama kila mtu mwenye matatizo na mawazo akitaka kwenda Ikulu kukutana na RAis ili matatizo yake yatatuliwe tutaanza kurudi kule kule kwa kwenda kupokea baskeli Ikulu!

Alipofagia si kwamba hakukuwa na watu wa chini kufanya usafi.
 
Hiyo hesabu siyo mkuu ..siku hizi watu wako irresponsible hakuna tena na usishangae kuambiwa hao wote ni familyless ..yaani wapo wapo tu, familia isikie tu.

Watu wanaogopa kuoa kama hawana kipato. Si kweli kwamba hesabu ya huyo bwana imekosewa. Huwezi kupuuza extended family za kiafrika na hazikwepeki.
 
Ni watu wachache tu kama BARBAROSA wanaofahamu umuhimu wa hili. Wengi, kwa vile ni mzungu, wanaandika upuuzi tu. Hizi fikra chafu za ubaguzi, hasa kwa wazungu, ni mabaki ya Ujamaa- Kibanga ampiga mkoloni type of thinking.
Watu hawajui kama kuna nchi duniani, kama Kazakhstan, watu kama hawa, wawekezaji, wanalipwa hasa na serikali ili waendelee kuwekeza na kutoa ajira! Angalia katika Google Kazakhstan na Tanzania wapi na wapi! Acheni ujinga wa kutosoma anzeni kusoma ulimwengu vilivyo.
Ni viwanda vichache vya umma kama vipo, vinavyoajiri watu 800.

Eti wanalipa kidogo. Mtanzania na uvivu wake ataka afanye kazi kidogo alipwe malaki. Wamezoea kuwaona wanasiasa wao. Leo ni mbunge kesho milionea. Katika dunia ya kweli hizo ni ndoto.
 
Hata wewe pia kama mwenzako hauelewi capitalistic economic system inavyofanya kazi!
Ni hivi kipato cha mfanyakazi kinaendana na uzalishaji (productivity) yaani jinsi uzalishashaji unavyoongezeka ndivyo kipato kinavyoongezeka na ndio maana kuna nchi za kipato cha chini, cha kati na juu kabisa, ukienda Uchina hapo mwanzo ilikuwa ni nchi ya kipato cha chini wakapiga kazi bila ya kulala na sasa wamepanda na kuwa kipato cha kati na wanaedelea kupiga kazi kuelekea kipato cha juu!
Ukienda Uchina kuna watu wanalala kwenye mabweni asubuhi wanaamkia kazini jioni wanarudi bweni na hawa wametoka vijijini huko lkn wanafanya tena kwa kipato kidogo sana unajua ni kwanini bado wanafanya kazi kwa kujituma? Ni kwa sababu wanajua ili waweze kupata kipato kikubwa ni lazima kwanza waongeze uzalishaji ili kiwanda kiweze kupata fedha zaidi na hakuna njia nyingine!

Sasa wewe unataka mfanyakazi TanZania alipwe kipato cha juu wakati nchi yetu ni ya kipato cha chini hiyo hela ya kulipa hiyo mishahara mikubwa muwekaji ataitoa wapi? Kumbuka huyu aliyewekeza kama ni kiwanda au sijui Hoteli amekopa fedha kwa ajili ya uwekezaji na ni lazima alipe dani, sasa atalipaje deni kama hakuna Uzalishaji?

Hivyo basi ni lazima kwanza sisi kama WatanZania tukubali kujifunga mkanda tufanye kazi kwa mshahara mdogo na kwa bidii bila ya kuchoka ili tuongeze uzalishaji, uzalishaji ukiongezeka ina maana Kampuni/Kiwanda chetu kitakuwa na fedha ambazo sasa inaweza kumudu kutuongeza mshara pmj na mapato mengine ya serikali pia kuendelea kuajili watu!

Hakuna njia nyingine wote hao unawaona kama ni Ujapani, Ulaya au Marekani wamepita huko, huwezi kudai Mshahara mkubwa kwenye nchi kama TanZania ambayo hakuna kitu kinafanya kazi, huyu muwekezaji inabidi atumie jenereta yake kuzalisha Umeme anunue mafuta ya jenereta, akienda Air port hakuna ndege na wakati mwingine maua yanaharibika kwa maana ni lazima yasafirishwe kwa wakati, hakuna Maji inabidi atafute ya kwake kwa kuwa hakuna hiyo miundo mbinu, madawa ambayo anayatumia kwenye mimea yake kama mbolea, au kuuwa vijidudu ni lazima aagize ktk nje ya nchi kwa maana TanZania hakuna mtu anayetengeneza hizo dawa, kwa kifupi ni lazima aimport kila kitu kuanzia viatu, gloves, mpaka nguo za kazi sasa hizo fedha za kulipa mishahara mkubwa atazitoa wapi?
Usisahau pia TanZania watu skilled hakuna au ni wachache sana mtu anamaliza Chuo hakuna anachojua na inabidi wewe mwenye Kampuni uingie gharama ya kumfundisha hii itakuchukuwa miaka 2-3 ili aweze kufanya kazi independently hii yote ni kwa gharama ya muwekezaji sasa hiyo fedha ya kumlipa mfanyakazi mshahara mkubwa itatoka wapi?

Acha tu kuongea kwa hamaki jaribu kuangalia mambo kwa uhalisia wake nchini kwetu ni ngumu sana kufanya biashara na kufanikiwa vizingiti ni vingi sana, jaribu tu hata kufungua ofisi ya stationary, wiki nzima hauna Umeme inakubidi ili uuze utafute jenereta na kununua mafuta sasa hiyo fedha itatoka wapi? Kumbuka hapo umekopa CRDB au TIB na unatakiwa ulipe deni, halafu hapo hapo mfanyakazi anakudai mshahara mkubwa wakati unapata umeme mara mbili au tatu kwa wiki wewe utatoa wapi fedha ya kumlipa mshahara mkubwa?




Mzee nimekuelewa
 
Afadhari hata mzungu wa maua je vipi wale wa GGM? yule mzee malofiii aliwapa bure kabisa eti kisa walimpatia pete ya dhahabu 100% na mche wa sabuni wa dhahabu 100% jamaa akachanganyikiwa akatia mkataba 100yrs kwa watz kubakiwa na 3% na mkaburu 97% kisha kutangaza msamaha wa ushuru na baadaye kakomaa na viushuru vya machinga na vioski. badala ya kuwakusanya wafanya biashara wakubwa wa tz na kuwajoint kwa hao makaburu ili wafanye kama partnership jamaa akaona ni vema kaburu ale shavu lote nayeye kuishia hako kapete na kamche. Bora huyo wa maua akutane na Rais na huko ndo watapanga na jinsi ya kulipa kodi na kuboresha salary la labours. sasa unataka akutane na waziri? huyo waziri akilamba dume la mzungu kama tuvyoshuhudia maliasili na utalii?

Kwa kuonyesha hana imani saaaana na hao mawaziri ndo maana Rais ameamua kuiongoza yeye mwenyewe TAMISEMI maana huko ndiko jamaaa walikuwa wapiga trioni za mafuba halafu watuaminisha eti serikali haina hela za kukizi mahitaji ya nchi nzima eti kwakuwa nchi yetu ni kubwa mno, upuuzi mtupu.

na ingewezekana kila mwekezaji akutane na Rais kwanza ili JPM ajue kila kitu kisha waziri aagizwe tu kutekeleza na kutoa tasrifa ya yaliyofikiwa. Kwasababu kwanza JPM anamda wa kutosha tu maana yeye siyo vasco dagama, ukiamua kufanya biashara na kufanikiwa, kama inawezekana kukutana na wateja wako wadogo kwa wakubwa fanya hivyo kabisa maana in business hata yule mwenye shilingi mia moja ni wa muhimu mno kwako.

Mtu aliyetoa ajira kwa watu 800 niwamuhimu sana tu, kutana naye ili uone namna ya kumfanya ifike watu 8000. sasa kati ya watz 50, 000, 000 ukiwa na watu 5000 tu watakaoajili watu 800 mathalani hata kama wanawalipa 180000 je hauoni kuwa ni dalili za kukua kwa uchumi.

Wahusika wamkutanishe huyu mtu na Rais wakadili na namna ya mishara pamoja na kupunguza landing ili kuongeza uzalishaji na mauzo huko ng' ambo
 
Huyu mzungu ni shetani. Anawalipa wafanyakazi wake shiling elf 75 kwa mwez. Hii ndio ile mikwepa kodi. Wafanya kazi wanakuwa tasa nakupata saratan kutokana na kemikali za sumu name hawavai protective clothes.
 
Capenhagen kwa kumwita shetani hakutasaidia kitu; jambo la maana ni yeye akutanishwe hata kama na Raisi au basi na waziri wakae na kuzumza ili kutatua tatizo. Sasa kama anawalipa labours 75 huku mamlaka zinazohusika zimekaa kimy unadhani nini kifanyike ili kusaidia?

Mambo ya mishahara ni kazi ya NSSF, PPF na chama cha wafanyakazi, kisheria hawa ndo wanatakiwa kufatilia mishahara ya wafanyakazi kama ilivo pangwa, wanatakiwa wajue mwekezaji anazalisha nini na anapata faida kiasi gani, na je hiyo faida inaendana na kima cha chini kama serikali inavyoagiza?

kwasababu hata sisi kwa sisi hatutimizi hicho kiwango, je mishahara wanayolipwa baa medi;

je wewe copenhagen house girl au house boy wako unamlipa kima cha chini? chamsingi wamfatilie huyu mzungu kisha warekebishe hizo kasoro ndogondogo na kazi iendelee.
 
Hapa wa kulalamikiwa ni serikali yenu na si mzungu. Mwaka 2013 ilitengeneza mwongozo wa mishahara ya private sector "wage order" ambayo inasema wafanyakazi wa mashambani watalipwa Tsh, 512.85 kwa saa, tsh. 3846.50 kwa siku, tshs.23078.70 kwa wiki, tshs. 46,147.40 kila baada ya wiki mbili na tshs. 100,000 kwa mwezi so kama tujuavyo bepari anamaximize profit so anawalipa within legal acceptable standard hivyo havunji sheria yeyote ya nchi hii kwani hii wage order orderimetengenezwa under labour institutions act CAP no. 300 under section number 39.
So chamaana ni serikali kuupitia upya huu muongozo ili uweze kuwabana hawa wawekezaji waklipe wafanywkazi kulingana na hali halisi ya maisha hilo lisipofanyika bepari ataendelea kunyonya hawa watu. Nawasilisha
 
Sector ya mbogamboga na matunda inaweza kuleta hela nyingi zakigeni kama wizara ya kilimo inaweza kuifanyia dharula ya kutosha ili kuiletea tija ya kwa sekta hii. Tunahitaji kuongeza wataalamu wa mbogamboga na matunda, kuongeza uthibiti wa mbegu na madawa, kupunguza au kuondoa kodi kwenye technolojia za uzalishaji kama green house, irrigation kits eg drips, cold rooms, kununua ndege za mizigo za kuanzia mbili, kuimarisha mazingira ili maji yaongezeke kwa ajili ya umwagiliaji.

Uzalishaji wa mbogamboga ni miezi 4 tu, hivyo kwa mwaka mkulima anavuna mara mbili, jambo ili litaisukuma sana nchi kimapato kwani nchi nyingi zinahitaji mazo ya bustani.

Wazekezaji ni wajanja kama wenye nchi wamezubaa, hakuna mwekezaji anaye wekeza mahali bila kujua mazingira yakazi, kukwepa kodi ni faida ya ziada, lakini kila mwekezaji anapiga gharama halisi kabla ya kuwekeza, akiamua kuwekeza ujue amekubaliana na mazingira, kukwepa kodi na tozo zingine na kuongeza faida zaidi na mara nyingi ni baada ya kujua wenyenchi bongo lala na ni watu wa kitu kidogo. lakini watendaji wakikomaa kodi italipwa bila shaka.

Ni kweli kwenye ofsi nyingi za serikari kuna njoo kesho zisizo na maana yoyote na haziongezi tija, bila kitu kidogo au memo kutoka kwa boss hakiendi kitu.

Pia ni muhimu kuunganisha kodi, kama hujawahikufanya biashara huwezi jua, ukijaribu kuanzaasha ndiyo utajua kuna kodi kila mahali hadi kodi ya maandishi yakibao cha karibu mteja dukani.
 
Asilimia kubwa ya hoja zake zilikuwa zinaongelewa sana na marehemu Mgimwa, juzi katika mkutano wa TAHLISO uliofanyika chuo kikuu msemaji wa mmoja wa chuo kikuu (yule mwalimu wa UDSM ambaye ni mjumbe wa bodi ya Tanzania Investment Centre pia) alikuwa akielezea jambo hili hili kuhusu uhalisia wa hotuba ya raisi kwenye kutekeleza ahadi ya zama za viwanda lazima vitu kadhaa vibadilike.

Heck mimi mwenyewe nimekuwa nikisema jambo hili from the time nimejiunga JF sasa subiri mambo ya Zanzibar yaishe Saada Mkuya aje katika zama hizi za mawaziri vijana labda atalifanyia kazi maana vipanga wizarani wamekosa mikakati mingine na apparently there is no one better in the whole of Tanzania for now despite several scholars and expert advisor saying the same thing on what is needed for some time now.
 
Kuna taasisi ya Serikali inaitwa OSHA kirefu chake ni Occupation health and safety inahusika na kuangalia kama mwajiri anacomply na usalama mahala pa kazi lakini pia mwajiri analazimika kumpima afya mwajiriwa sheria iliyoanzisha mamlaka hii inalazimisha na ikiwa mfanyakazi hujapimwa ulipoanza kazi na ukapata ugonjwa ambao umesababishwa na kazi ulisozifanya kwa mwajiri nenda mahakamani utalipwa vizuri tukwa mwajiri kukusababishia ugonjwa km hajakupima ulipoanza kazi hilo ni kosa lake.
 
...huwa najiuliza wabongo walilogwa na nani!1...kwamba hata maua waje wazungu TZ kuzalisha na kuuza kwa dola nje...yani TZ kila kitu ukigusa ni pesa...huko SUA kila kukicha wana graduate watu wa horticulture....sasa sijui huwa wanaishia wapi???...yani arusha na moshi yote ni rutuba tupu ya maua na mboga...hadi mbinga ni hivyo lakini mabonde mengi yameishia kulisha mifugo na misitu isiyozalisha....alafu watu wanalialia wazungu wakija kuchukua madini kwetu!...nchi imejaa ardhi tele yenye rutuba...madini....maji....gesi..samaki...wanyama.....ngo'mbe....kuku...mbuzi...kondoo....nguruwe...n.k n.k..yoote hiyo ni pesa tu...lakini wabongo hawachoki kulialia....kama watu wamelala waacheni wazungu watuvune...maana hii nchi ilishageuzwa shamba la bibi na watawala waliopita...
 
Back
Top Bottom