Special agent.
Senior Member
- Aug 25, 2015
- 101
- 71
Lazima Tushinde, tutashinda hata kwa bao la mkono, hizo ni kauli za CCM ambazo kwa mtu mwenye akili zake timamu anajua fika hawa watu wanaweweseka na tayari hakuna ushindi kwao.
Lowassa amewakalia kooni na ndo maana ili kutoa aibu wanatembea na Diamond ili kupata mkusanyiko wa watu,kama Magufuli akijaribu kutembea peke yake bila Diamond atadharirika sana, hakuna ushindi kwa CCM mwaka huu, huu ni mwaka mgumu sana kwa taifa la Tanzania.
Ni mwaka wa machozi na damu, mkuu wa kaya ameapa hataikabidhi ikulu kwa mpinzani, viapo hivyo ni dalili ya kutambua ukweli kuwa kaelemewa.
Lowassa naye kaapa hatakubali kuporwa ushindi, hakika ni mwaka mgumu kwa taifa la Tanzania, kuna tetesi wakuu wa usalama wameamrishwa kufanya kila wawezalo kuhakikisha wanamdhibiti ipasavyo Lowassa.
Magufuli naye anaujua ukweli mzito kuwa hatashinda, watanzania wamekichoka hiki chama, Magufuli kaivua nguo serikali ya JK wakati wa uzinduzi wa kampeni pale alipohoji kwanini nchi haina hata kiwanda cha kusindika nyama na samaki? miaka 54 ya CCM ikulu tusubiri.
Lowassa amewakalia kooni na ndo maana ili kutoa aibu wanatembea na Diamond ili kupata mkusanyiko wa watu,kama Magufuli akijaribu kutembea peke yake bila Diamond atadharirika sana, hakuna ushindi kwa CCM mwaka huu, huu ni mwaka mgumu sana kwa taifa la Tanzania.
Ni mwaka wa machozi na damu, mkuu wa kaya ameapa hataikabidhi ikulu kwa mpinzani, viapo hivyo ni dalili ya kutambua ukweli kuwa kaelemewa.
Lowassa naye kaapa hatakubali kuporwa ushindi, hakika ni mwaka mgumu kwa taifa la Tanzania, kuna tetesi wakuu wa usalama wameamrishwa kufanya kila wawezalo kuhakikisha wanamdhibiti ipasavyo Lowassa.
Magufuli naye anaujua ukweli mzito kuwa hatashinda, watanzania wamekichoka hiki chama, Magufuli kaivua nguo serikali ya JK wakati wa uzinduzi wa kampeni pale alipohoji kwanini nchi haina hata kiwanda cha kusindika nyama na samaki? miaka 54 ya CCM ikulu tusubiri.