Magufuli haonekani kuwa na mzuka na Dodoma

Ki Mun

JF-Expert Member
Oct 6, 2014
3,442
4,388
Nikitazama 'lugha ya mwili'(body language) ya Rais Magufuli, namwona ni mtu mwingine tu ambaye kwa lugha maarufu ya wadau humu JF, amekuja "kupita" tu bila ya kuwa na dhamira ya kuhakikisha kuwa kweli Dodoma inakuwa Makao Makuu ya nchi.Itaendelea kubaki makao makuu ya chama chao - nao na kiherehere chao sijui nani aliwadanganya kuwa Dodoma itafika wakati itakuwa kweli makao makuu ya nchi. Kwa hiyo Dodoma itabidi wasubiri sana kuwa makao makuu ya kweli,labda itokee Juma Nkamia akawa Rais,au kwa maana hiyo mtu mzaliwa wa Dodoma....

Nina sababu mbili:

Moja,Rais Magufuli inaonekana amepania kuing'arisha Dar kwa "mabarabara" ya kupita juu na yenye mbwembwe za kila aina,naye hupenda sana kuzindua miradi ya mabarabara na madaraja.

Pili,yeye si mkereketwa kindakindaki wa CCM na bila shaka hana "jumba bovu" mjini mle - waliomtangulia walipapenda maana wana "magofu" ya kila namna kule,na walilipenda pia chama lao.Magufuli hana mzuka wa kuzurura-zurura kwenye mji huo wenye jua kali.

Magu hana mzuka na Dodoma, Magufuli anapapenda Dar, na kwao Chatooo...Dodoma nawaona bado watakuwepo-kuwepo kwa muda mrefu kidogo kabla ya kuwa Capital City kweli,kama si kufutiliwa mbali kabisa,who knows?
 
Nikitazama 'lugha ya mwili'(body language) ya Rais Magufuli, namwona ni mtu mwingine tu ambaye kwa lugha maarufu ya wadau humu JF, amekuja "kupita" tu bila ya kuwa na dhamira ya kuhakikisha kuwa kweli Dodoma inakuwa Makao Makuu ya nchi.Itaendelea kubaki makao makuu ya chama chao - nao na kiherehere chao sijui nani aliwadanganya kuwa Dodoma itafika wakati itakuwa kweli makao makuu ya nchi. Kwa hiyo Dodoma itabidi wasubiri sana kuwa makao makuu ya kweli,labda itokee Juma Nkamia akawa Rais,au kwa maana hiyo mtu mzaliwa wa Dodoma....

Nina sababu mbili:

Moja,Rais Magufuli inaonekana amepania kuing'arisha Dar kwa "mabarabara" ya kupita juu na yenye mbwembwe za kila aina,naye hupenda sana kuzindua miradi ya mabarabara na madaraja.

Pili,yeye si mkereketwa kindakindaki wa CCM na bila shaka hana "jumba bovu" mjini mle - waliomtangulia walipapenda maana wana "magofu" ya kila namna kule,na walilipenda pia chama lao.Magufuli hana mzuka wa kuzurura-zurura kwenye mji huo wenye jua kali.

Magu hana mzuka na Dodoma, Magufuli anapapenda Dar, na kwao Chatooo...Dodoma nawaona bado watakuwepo-kuwepo kwa muda mrefu kidogo kabla ya kuwa Capital City kweli,kama si kufutiliwa mbali kabisa,who knows?
Dodoma itakuwa mji mkuu endapo kibajaji angekuwa Rais na Nina Imani CDA ingevunjwa na wale waliokula pesa tokea Enzi za Mwalimu wangefungwa hata Le Mutuz Sasa Hivi angekuwa Jela maana hapendi kwao yeye anapenda Dsm gheto ili Usiku anawanyemelea Ma-House girls , mijutu Kama hii ndiyo imelisababisha jiji la Dsm kuwa na foleni baada ya Serikali kugoma kuhamia Dodoma na kubakia kuleta foleni kubwa na misafara Yao, Nigeria, malawi walijifunza CDA jinsi ya kuhamia miji mipya cha ajabu wao tayari wamehamia miji mipya lakini Tanzania wamebakia kupitishia pesa CDA kila Bajeti zinaliwa na wajanja wachache Huku wakiendelea kubanana Dsm na kuidanganya Dunia kuwa mji mkuu ni Dodoma .
 
Ni bora Kama hawataki kuhamia Dodoma watamke wazi kuwa Hilo wazo limekufa Sasa Serikali wataangalia upya mji mwingine wa kuhamia ili kulipunguzia jiji mzigo wa kubanana , wabunge wote wanaishi Dsm hawataki kuishi majimboni kwao hiki kioja cha Dunia na Afrika, Uganga , Kenya , Rwanda na Burundi wabunge wengi wanaishi huko huko majimboni kwao hawapendi kuhamia miji mikuu kubanana , hiki kituko kipo Tanzania pekee , Rais mwenyewe hawapendi Dodoma kule ikulu ya chamwino pamegeuka kuwa makazi ya panya na ndege hataki kutoa mfano ili maendeleo yapanuke mikoani Nchi ipige Hatua haraka Kama South Africa kila mji ni mzuri watu hawakimbilii kwenda kubanana pritoria kuifuata Serikali ilipo.
 
Hivi unajua Dar es salaam, kuna watu wangapi?
jiji la Dsm Sasa Lina watu zaidi ya milion 7 ni moja ya miji yenye Watu wengi barani Afrika, Serikali wameshindwa kuiga hata kule Juba mji ni Mdogo lakini Serikali wameamua kukomaa humo humo wanaujenga vizuri utakuwa , Dodoma ikithaminiwa vizuri itakuwa Kwa kasi kubwa na kuufanya mji Dsm kupumua kidogo na kuleta maendeleo mikoani .
 
Watangaza nia ya Urais wote Kipindi cha kampeni hawakuwa na wazo la Serikali kuhamia Dodoma Bali woote walikuwa na fikra za kubanana Jiji Dsm umeme ufike pahala uweke Kama kibatari ndipo watashituka juu ya Ujenzi holela Uswahilini .
 
Dodoma hakuna potential yoyote ya uzalishaji, kwa hiyo kitakacho fanyika ni kuondoa watu kama laki nane ambao ni wafanyakazi wa serikali na kuwapeleka dodoma. Tatizo litakuwa halijaisha,bado uzalishaji na viwanda viko dar es salaam. Kuwarudisha watu mikoani ni ngumu maana huko mikoani kazi ya maana ni kilimo ambacho si wote wanakiweza. Maana yake serikali inabidi irudi tena kuwekekza kwenye viwanda ,na hili nalo ni tatizo lingine. Lakini kinachotakiwa kifanyike sio hiki tunachokizungumza.
 
Back
Top Bottom