Magufuli bado hajanishawishi

katusyo

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2013
Posts
1,455
Reaction score
434
Nikiri kwamba kaanza vizuri sana lakini bado hajanishawishi, watanzania tunahitaji maisha bora na yenye uhakika, tunataka uchumi wa nchi ukae vizuri, tunataka vifaa vya ujenzi vishuke bei, tunataka pembejeo za kilimo zishuke bei, tunataka vyakula vishuke bei, tunataka mafuta yashuke bei ili kushusha gharama za usafiri, tunataka umeme wa uhakika na wa kiwango cha chini, tunataka maji ya uhakika, tunataka elimu ya uhakika ikiwemo kuboresha maslahi ya walimu, tunataka madawati na majengo kwa uhakika, tunataka huduma bora za afya nchi nzima, hapo nitaanza kukuunga mkono.
 
Hahahaa, eti Vyakura vishuke bei,fanya edit andiko lake ndo tuchangie
 
Tushawishi ww kwanza kwa kuandika vizuri,,,vyakura na masrai ndio nn? Kama hujashawishika ww basi kausha tu lakini wengi wetu hajatushawishi bali tumemkubali kabisa,,,
 
hayo yote aliahidi atafanya, we tulio tuli uone mwanaume anavopiga kazi.
Hivi sasa yuko hatua ya awali kukusanya pesa
 
Alagi tigo uyo mzee..ww tuliza machepele...
 
Vyakura = Vyakula
masrai = maslahi
elim =elimu
walim = walimu
Vinginevyo mawazo yako ni mzuri na ya msingi pia, Hapa unawakilisha matarajio ya Watanzania walio wengi, Lakini kumbuka kuwa huu sio mwanzo mbaya! muheshimiwa ameanza vizuri, tumpe support na tumuombee.
 
Sidhani kama kushawishi ni moja ya majukumu ya rais.
 
Bado mapema, na utashawishika tu mkuu. Ngoja akusanye kodi zote kwa uhakika afu utapenda mwenyewe.

Ungekuwa wewe ndie yeye, ungeweza kuboresha hayo yote uliyoorodhesha within 30 days only? Acha mawazo mgando, think beyond!
 

Wewe mwenyewe umeshasema kaanza vizuri halafu unasema huungi mkono, unadhani maji, Elimu Afya nk...... Kwa hali nchi ilipokuwa imefika vinaweza kuanza Kuja bila mwanzo mzuri, na ukumbuke bado hana wasaidizi ulitakiwa kuyasema haya baada ya mwaka.
 
Mwache kwanza atumbue majipu serikali ipate fedha za kutosha ili itimize hayo mambo uliyoyataja,kumbuka kakabidhiwa Nchi ikiwa Haina pesa kabisa.
 
Ndio vizuri, hawezi akashawishi wote!
 
Nafikiri ni mapema mno kutimiza yote hayo kwa muda mfupi huu alioingia madarakani! hata Roma haikujengwa kwa mara moja jamani hata mwezi bado! nashukuru umekiri kuwa ameanza vizuri nchi ilisha oza ndugu yangu tumuombee tunaweza tukawa tumepata masiha
 


Hata wewe unapoamka asubuhi lazima uanze kwa kukiinua moja ya viungo vyako mwilini, huwezi inuka kama vile umevutwa na sumaku, kwa hiyo naye anatekeleza action plan yake, ina pa kuanzia na pa kumalizia
 

K?ka unakula mirungi nini kwa siku 25 tuu unataka hayo,!
 
Hata mimi bado hajanishawishi achukue ile mitambo ya iptl tuache kuingia hasara au anamwogopa seth!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…