Magufuli baba wa Afrika?

Magufuli baba wa Afrika?

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2016
Posts
16,099
Reaction score
24,338
Dr John Joseph Pombe Magufuli hakuwa Shujaa wa Afrika.

Kama alikuwa shujaa wa Afrika naomba kujibiwa maswali yafuatayo.

Mosi; Rais Magufuli ametatua migogoro au kutatua matatizo ya Afrika kwa kiwango gani?

Pili; Rais Magufuli amewahi kuhutubia mara ngapi Umoja wa Afrika kuhusu Afrika?

Tatu; Rais Magufuli amewahi kuhutubia mara ngapi Umoja wa Mataifa au kuhudhuria mkutano mkuu wa Umoja huo kuhusu Afrika na misimamo ya Afrika mbele ya mabeberu?

Nne; Rais Magufuli alimteua Hayati Benjamin William Mkapa kutatua matatizo ya Burundi na Mkapa alijitoa , unajua kwanini?

Tano; Rais Magufuli alikuwa anaipigania Afrika kupitia nini? Vyombo vya habari,mikutano au safari mbalimbali za Afrika?

Sita; Misimamo ya Rais Magufuli ilikuwa kwa maslahi ya Afrika au Tanzania?

Saba; Rais Magufuli amewahi kuwezesha jambo gani kuhusu uchumi wa nchi za Afrika?

Nane; Rais Magufuli amefanya Jambo gani ambalo bara zima litamkumbuka?

Nadhani vyombo vya habari vinavyoripoti ushujaa wa Rais John Joseph Pombe Magufuli Afrika wanapaswa kutupa mifano anuai na uthibitisho.

Msimamo wangu ni kwamba Rais Magufuli hakuwa Shujaa wa Afrika


Njoo na hoja huna kaa kimya


Mandela ni Icon wa Africa.

1.Aliwasamehe waliomfunga miaka 27 Gerezani (Roben Islan0.

2.Aliunda kamati ya maridhiano iliyoongozwa na Askof Desmond tutu na kupewa tuzo ya Nobel.

3:Alikuwa akisafiri anamwachia Chifu Mangosutu Buthelelezi wa Inkatha Freedom Fighter(yaani mpinzani)ikulu na hakuwahi kumwambia aunge mkono juhudi.

4;Alikaa madarakani kipindi kimoja tu akawaachia wengine.

5:Aliwaita wapinzani wake tena waliontesa jela kuja kula nao chakula na kwaambia wasahau yaliyopita..tena unaambiwa wengine walikuwa wanamkojolea kichwa akiomba maji ya kunywa.

Mandela ni zaidi ya kuitwa shujaa wa Africa bali ni shujaa wa dunia.
 
Utatajiwa miradi ambayo utaambiwa haipo nchi zingine Afrika
 
Marehemu alikuwa mbaguzi ambaye alijivunia hiyo tabia kila anaposimama mbele za watu, kwake yeye Chato na wana CCM ndo walikuwa kipaombele hivyo niseme tu marehemu alikuwa mbinafsi na mchoyo. huyu hakuwa na tofauti na King James 2 kwenye zile Devine theoriez zake
 
Back
Top Bottom