Magufuli anachekesha walionuna

Magufuli anachekesha walionuna

kisiri mwihechi

Senior Member
Joined
Jun 8, 2015
Posts
135
Reaction score
24
Leo akiwa kinondoni anasema yeye anakwenda kufanya maamuzi sahihi si maamuzi magumu kama ya lowasa. Eti maamuzi magumu yanafanywa vibaka na majambazi.

Maamuzi sahihi yapi? Ya kukamata meli tunakuja kulipa matrilioni kama fidia? Maamuzi sahihi ya kubomoa visima vya mkafuta mahakama inakataa. Maamuzi sahihi ya kuhonga malaya wake nyumba za serikali, maamuzi sahihi ya kubomoa nyumba za wananchi bila fidia. Bora anyamaze lasiongelee maamuzi magumu ya lowasa.
 
Sijawahi kuona Dr fake kama magufuli. Yaani yeye kila msemo anaiga tu. Atabuni misemo yake lini?
 
Sio kosa lake ni kiwewe cha kushindwa kabla hata ya uchaguzi
Maana hata msaada wa wale wana CHANDIMU 32 hawaonekani.
 
Ameona slogani yake ya hapa ni kazi tu haiwezi kumvusha sasa anaparamia kila kilicho cha ukawa. Mara Aseme kuzungusha mikono yeye anaweza kuzungusha mara mia tano. Huyu baba vp?
 
Magufuli atakuwa kachanganyikiwa.Jana nilibahatika kuangalia mkutano wake akiwa Geita.
Hajui anatakiwa aongee nini kama mgombea wa urais,hana ushawishi kabisa.
Alipoteza zaidi ya lisaa kwa kujisifia,mara awaambie akina mama wapige vigelegele!
Nilishangaa sana.
 
Huyu akiwa Rais itakuwa maajabu ya 8 haya
 
magufuli hafai kuongoza nchi.... hana hulka ya utawala.... mtawala akiwa mbabe ni pigo kwa wananchi wake.... kujivika u-mungu mtu alivokuwa wazir... je urais???? ASHINDWE KABISA
 
Utamsikia piga kelele, piga miluzi, piga vifijo hahahah
 
kumbe mnafatilia mikutano ya magufuli...halafu mnasema hana ushawishi na mvuto...robot ndio anao mvuto?
 
magufuli hafai kuongoza nchi.... hana hulka ya utawala.... mtawala akiwa mbabe ni pigo kwa wananchi wake.... kujivika u-mungu mtu alivokuwa wazir... je urais???? ASHINDWE KABISA

Kweli pia hana haiba ya kiongozi. Tuwe makini watanzania, Magufuli sio.
 
Back
Top Bottom