Sina ubaya wowote, kinyongo na wala sifahamiani na Salum Mkambala wa Magic FM. Lakini nimeshindwa kujizuia kusema kuwa huyu bwana ananikwaza saana nikiwa nafuatilia mijadala mbalimbali katika studio za Magic FM, hasa vipindi vya asubuhi.
Kwanza: Uelewa wake uko wazi kuwa chini ya viwango vya akina Erast Kawau, Kibwana Dachi na Mary Edward.
Pili: Siyo mvumilivu wa kusikiliza asiyoyajua ili aongeze maarifa.
Tatu: Ni mlopokaji na mtu wa kudakia hoja ambazo wala hana uelewa nazo na kutaka kuchangia huku aki - hit off target.
Nne: Anaingilia mlolongo wa mjadala inayokuwa inajadiliwa na kuchomeka vitu tofauti kabisa na hoja iliyopo mezani na kuipindisha kabisa na kutunyima sisi wasikilizaji fursa ya kufika hitimisho halisi la mjadala husika.
Tano: Mbishi tu hata kama hana sababu za msingi za kufanya ubishi huo.
Pendekezo: Mkambala apandishwe cheo akasimamie mausala mazima ya Magic FM, asiendelee kukaa katika meza za majadiliano. A some taarifa za Habari na kutangaza mpira.
Atafutwe mtu mwingine, kijana Mwenye uelewa mithili ya Kibwana Dachi ili aongeze nguvu katika team ya Magic FM, vipindi vya asubuhi. (succession plan ni muhimu).
Kwanza: Uelewa wake uko wazi kuwa chini ya viwango vya akina Erast Kawau, Kibwana Dachi na Mary Edward.
Pili: Siyo mvumilivu wa kusikiliza asiyoyajua ili aongeze maarifa.
Tatu: Ni mlopokaji na mtu wa kudakia hoja ambazo wala hana uelewa nazo na kutaka kuchangia huku aki - hit off target.
Nne: Anaingilia mlolongo wa mjadala inayokuwa inajadiliwa na kuchomeka vitu tofauti kabisa na hoja iliyopo mezani na kuipindisha kabisa na kutunyima sisi wasikilizaji fursa ya kufika hitimisho halisi la mjadala husika.
Tano: Mbishi tu hata kama hana sababu za msingi za kufanya ubishi huo.
Pendekezo: Mkambala apandishwe cheo akasimamie mausala mazima ya Magic FM, asiendelee kukaa katika meza za majadiliano. A some taarifa za Habari na kutangaza mpira.
Atafutwe mtu mwingine, kijana Mwenye uelewa mithili ya Kibwana Dachi ili aongeze nguvu katika team ya Magic FM, vipindi vya asubuhi. (succession plan ni muhimu).