GE2025 Magazeti nchini ni kibogoyo, hakuna lililothubutu kuandika kuhusu maoni ya Humphrey Polepole uteuzi wa Rais Samia kuwania urais

GE2025 Magazeti nchini ni kibogoyo, hakuna lililothubutu kuandika kuhusu maoni ya Humphrey Polepole uteuzi wa Rais Samia kuwania urais

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mwizukulu wa Buganda

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2024
Posts
638
Reaction score
1,771
Ujasiri kwa Upinzani, Kimya kwa CCM

Jana, kupitia ukurasa wake wa Facebook, Balozi Humphrey Polepole alitoa maoni bila kupepesa macho kuhusu uteuzi wa Rais Samia kuwania tena urais na kuvunjwa kwa baadhi ya desturi za Chama cha Mapinduzi (CCM). Hata hivyo, magazeti nchini yameshindwa kuripoti moja kwa moja kauli hizo, tofauti na jinsi yalivyo mstari wa mbele kuripoti taarifa za vyama vya upinzani, hata pale zinapokuwa na ladha ya kuharibu taswira ya vyama hivyo.

Sababu kuu ya hali hii ni uoga uliokita mizizi ndani ya vyombo vya habari vya Tanzania. Magazeti na redio nyingi huogopa kuchapisha taarifa zinazoweza kutafsiriwa kama ukosoaji kwa Serikali au chama tawala kwa kuhofia kufungiwa, kupokonywa leseni, au kupewa onyo na mamlaka za udhibiti kama TCRA. Matokeo yake, vyombo hivi vinachagua ukimya pale ambapo hoja zinagusa misingi ya chama tawala, huku vikitoa nafasi kubwa kwa taarifa za upinzani, bila kujali madhara au ukweli wake.

Hali hii inaibua maswali juu ya uhuru wa vyombo vya habari na nafasi yake katika kuelimisha umma kwa kuandika ukweli bila hofu wala upendeleo. Kauli za Polepole, ambazo zilihusu uhalali wa mchakato wa uteuzi ndani ya CCM, ni mfano wa taarifa ambazo zingepaswa kujadiliwa kwa uwazi, lakini zimezuiliwa na hofu ya kisiasa.

habari leo.jpg
Jamvi.jpg
mwananchi.jpg
Nipashe.jpg
uhuru.jpg
 
  • Kicheko
Reactions: Lax
Si mnawaonaga wapinzani hawana juhudi za kupambana🤣
 
Alafu wanalalamika kuwa soko limekuwa guru vyombo vya habari vinafilisika kumbe vinajiua vyenyewe kwa kuendekeza uchawa.
 
Wa Hariri hawaandiki mapumba.

Hizi nywele zinaweza kuashiria ugonjwa gani?
Screenshot_20250811-113240.jpg
 
Alafu wanalalamika kuwa soko limekuwa guru vyombo vya habari vinafilisika kumbe vinajiua vyenyewe kwa kuendekeza uchawa.
Mlitaka kudanganywa ¿¿

kama Mambo ya michezo.

Wachungaj wanawadanganya kila uchao si mtosheke bado mnataka na habari itumike kuwapa danganya toto. Mshangilie na mapambio

sisi tuliowengi ndio hatutaki kudanganywa RAIS SAMIA SULUHU HASSAN 25 to 30
 
Unaandkaje hisia za pole pole ambazo haziwezi kuthbitika?
Kupayuka tu tayari unaandka?
 
Back
Top Bottom