Kalamu Nzito
JF-Expert Member
- Aug 13, 2015
- 376
- 850
Kuna baadhi ya mafundisho yanaenea katika Ukristo ambayo hayana msingi wowote kwenye Biblia
1. KUAMURU MALAIKA (COMMANDING THE ANGELS)
Kuna baadhi ya watumishi wanafundisha waumini kuamuru Malaika kufanya mambo fulani. Jambo hili ni kinyume kabisa na maandiko kwani Malaika ni watumishi wa Mungu (Servants of God) na sio watumishi wa wanadamu. Mungu ndo anaamuru Malaika wake na sio mwanadamu.
2. TOA SADAKA INAYOKUUMA.
Kuna watumishi wanafundisha kwamba ili ubarikiwe na Mungu, lazima utoe sadaka inayokuuma. Hata hivyo, Biblia haifundishi kitu kama hiki. Maandiko yanahimiza kutoa kwa moyo mkunjufu (2 Wakorintho 9: 7) ukiona unaumia kwa kile unachotoa tayari unakua umekiuka kanuni ya utoaji.
3. KUOMBA KWA WATAKATIFU WALIOKUFA
Kuna mafundisho kwamba watakatifu waliokufa wanasikia maombi yetu na wanayasogeza mbele za Mungu. Hata hivyo, kwenye Biblia hakuna mafundisho ya aina hiyo. Wengi wanatumia mstari kutoka Ufunuo wa Yohana 5:8 kuteta hoja hii. Hata hivyo, msitari huo hautoi ufafanuzi wala mamlaka ya moja kwa moja kwamba tunaweza kuomba kwa watakatifu waliolala. Kitabu cha Ufunuo kimekua kikitumika kuhalalisha taratibu ambazo kimsingi zimepotoshwa ili kuendana na matakwa ya kibinadamu.
Yesu Kristo alishaweka mamlaka juu ya jina lake na akasisitiza kuomba kupitia yeye (Yohana 14: 14). Roho Mtakatifu ambaye Yesu alituachia ndiye muombezi wetu ambaye hutusaidia kuomba kwa kuugua kusikoweza kutamkwa (Warumi 8: 26-27).
Hata kama watakatifu wapo Mbinguni, hawana jukumu la kupokea wala kusikia maombi. Hakuna mtu yoyote kwenye Biblia aliwahi kuomba kwa Mitume waliokufa. Haya ni mapokeo ya kibinadamu.
BARIKIWA!
1. KUAMURU MALAIKA (COMMANDING THE ANGELS)
Kuna baadhi ya watumishi wanafundisha waumini kuamuru Malaika kufanya mambo fulani. Jambo hili ni kinyume kabisa na maandiko kwani Malaika ni watumishi wa Mungu (Servants of God) na sio watumishi wa wanadamu. Mungu ndo anaamuru Malaika wake na sio mwanadamu.
2. TOA SADAKA INAYOKUUMA.
Kuna watumishi wanafundisha kwamba ili ubarikiwe na Mungu, lazima utoe sadaka inayokuuma. Hata hivyo, Biblia haifundishi kitu kama hiki. Maandiko yanahimiza kutoa kwa moyo mkunjufu (2 Wakorintho 9: 7) ukiona unaumia kwa kile unachotoa tayari unakua umekiuka kanuni ya utoaji.
3. KUOMBA KWA WATAKATIFU WALIOKUFA
Kuna mafundisho kwamba watakatifu waliokufa wanasikia maombi yetu na wanayasogeza mbele za Mungu. Hata hivyo, kwenye Biblia hakuna mafundisho ya aina hiyo. Wengi wanatumia mstari kutoka Ufunuo wa Yohana 5:8 kuteta hoja hii. Hata hivyo, msitari huo hautoi ufafanuzi wala mamlaka ya moja kwa moja kwamba tunaweza kuomba kwa watakatifu waliolala. Kitabu cha Ufunuo kimekua kikitumika kuhalalisha taratibu ambazo kimsingi zimepotoshwa ili kuendana na matakwa ya kibinadamu.
Yesu Kristo alishaweka mamlaka juu ya jina lake na akasisitiza kuomba kupitia yeye (Yohana 14: 14). Roho Mtakatifu ambaye Yesu alituachia ndiye muombezi wetu ambaye hutusaidia kuomba kwa kuugua kusikoweza kutamkwa (Warumi 8: 26-27).
Hata kama watakatifu wapo Mbinguni, hawana jukumu la kupokea wala kusikia maombi. Hakuna mtu yoyote kwenye Biblia aliwahi kuomba kwa Mitume waliokufa. Haya ni mapokeo ya kibinadamu.
BARIKIWA!