Mafisadi wengine ni hawa

MmasaiHalisi

Senior Member
Jan 15, 2009
192
23
napenda kuchua fursa hii kuwajulisheni watanzania wenzangu mafisadi wengine ambao wanatuibia bila sisi kujua si wengine bali PPF au Parastatal Pension Fund,shirika hili linatuibia sana sisi wanachama wake, kwa mfano kuna mmoja wa wastaafu amestaafu kwa cheo fulani kikubwa mafao aliyolipwa Tsh 3,000,0000/= wakati mstaafu mwingine amestaafu kwa cheo kama cha huyo wa awali amelipwa 45,000,000 kutoka mfuko mwingine wa pension(tunauhifadhi)sasa huu sio wizi na monthly pension unamlipa 25,000.pesa zetu wanakopeshwa akina Manji wakati sio wanachama au wanajenga magorofa makubwa, sisi wastaafu tunataabika sasa tunataka kujua hao PPF wataumia formular gani kucalculate mafao ya wastaafu,kama sio wizi nini?
 
1. Angalia tovuti(website) yao utaona formula wanayotumia!!! Nadhani mifuko yote ya hifadhi za jamii wana tovuti zao, bila shaka hata PPF ipo na utaona kila kitu ili ulinganishe na huyo mwingine. Kinachotumika ni mishahara na muda uliofanya kazi katika fomula zao-hivyo hata kama mna cheo kimoja bado mwaweza kutofautinana kutokana na vigezo hivyo viwili .
2. Lakini kwa nini usiongee nao kwenye jambo la wazi kama hili????
 
PPF ni wadhulumaji sana hata sasahivi public universities wanajadili namna ya kuhamisha wafanyakazi wao kuwapeleka mifuko mingine. pension yao ni ndogo sana hata kama una mshahara mkubwa
 
Ni kweli ndugu yangu. PPF inanyonya wanachama na kunufaisha wasio wanachama kama huyo uliyemtaja. Imulikwe.
Lakini angalia usijeburuzwa kortini kwa kutaja majina hata kama utadaiwa shilingi moja kama Bwana Mengi.
Pia chunga wazee wa Yanga wasikuweke kwenye luninga ukashindwa kuwajibu!
 
napenda kuchua fursa hii kuwajulisheni watanzania wenzangu mafisadi wengine ambao wanatuibia bila sisi kujua si wengine bali PPF au Parastatal Pension Fund,shirika hili linatuibia sana sisi wanachama wake, kwa mfano kuna mmoja wa wastaafu amestaafu kwa cheo fulani kikubwa mafao aliyolipwa Tsh 3,000,0000/= wakati mstaafu mwingine amestaafu kwa cheo kama cha huyo wa awali amelipwa 45,000,000 kutoka mfuko mwingine wa pension(tunauhifadhi)sasa huu sio wizi na monthly pension unamlipa 25,000.pesa zetu wanakopeshwa akina Manji wakati sio wanachama au wanajenga magorofa makubwa, sisi wastaafu tunataabika sasa tunataka kujua hao PPF wataumia formular gani kucalculate mafao ya wastaafu,kama sio wizi nini?

LAPF
NSSF
PPF

Wote hao wana namna ya kufanya mahesabu ya uzeeni, kati ya hizo kuna mmoja analipa vizuri kuliko wengine. All in All NSSF Wizi mtupu, unarudishiwa hela zilezile na interst KIDUCHU waka mihela yako imezaa na kuzalisha SANA
 
Kidumu Chama Cha Mapinduzi! Zidumu fikra sahihi za mwenyekiti wake!
 
Back
Top Bottom