Mafisadi CCM wageuka mbogo

Mafisadi CCM wageuka mbogo

Ukweli EL ameshika mpini na wao makali, hamshangai kwanini anamwambia Msekwa nilijiuzulu uwaziri mkuu kwaajili ya kunusuru chama na serikali, yeye kama waziri mkuu asingejiuzulu kwasababu ya makamu mwenyekiti au kiongozi mwingine yeyote wa ccm ila mwenyekiti na pia asingejiuzulu kwasababu ya waziri wa nishati au mwingine yeyote ila mkuu wa kaya - kwa utashi wangu hiyo ndio tafsiri sahihi sasa hawa jamaa wa ikulu sijui wamelisoma hili gazeti? Kama ndivyo tunasubiri walitolee ufafanuzi au kukanusha

Watakanusha kwa kulifungia,kuwa linaleta/chafua hali ya hewa kwenye GAMBA jipyaaaaaa!!!
 
Hakika chama legelege kimetuletea serikali legege. Yaani pamoja na mamlaka makubwa kisheria aliyonayo rais bado anatishiwa na Chenge kwamba akizongwa atahamia upinzani? Chenge anatakiwa awe kizuizini si kuhamia upinzani!
 
kinachonisumbuwa mimi ni mawasiliano ya Raisi kikwete na Edward Lowasa,kwani yaonekana mwenyekiti wa chama Taifa hana mawasiliano na Mzee Msekwa
Mzee Lowasa
Anasema mbali na kueleza hilo, Lowassa alisikika akisema, "nilikutana na Rais Kikwete. Aliyonieleza si haya."

kwa hiyo mzee msekwa anajisumbuwa tu kwani anayo yasema hayafanani na yale anayoelezwa Mzee Lowasa na Mwenyekiti wa chama Taifa

hapo kazi ipo
 
- Duh!'

William @ NYC, USA.
Ndicho chama chenu, unachokitetea kila siku. Chama cha baba yako. Tangu bajaji liangushe trecta, naona trekta halijanyanyuka tena lisaidie chama kutoanguka. Mzee mnafiki yule, alafu kwa nini hashibi? Mahela yote ya utumishi wake bado haridhiki tuu.
 
Hii habari imekaa kama vile mwandishi wa Mwanahalisi ndie aliyeandika minutes za vikao hivyo, nina shaka hawa mafisadi wanalitumia gazeti hili kujaribu kujisafisha.

Kawaida ya mikutano ya kusutana ya ccm, huwa tunaletewa taarifa iliyopakwa rangi lakini haya tunayoona hapa ni kama hawa jamaa waliwekwa kitimoto halafu walipotoka wakapika hii habari ili kuonyesha kama vile bado ngoma nzito.
 
- Duh!'

William @ NYC, USA.
kaka bado usishangae hiyo ndio bongo kila kitu kinawezekana kwa style tofauti tofauti na hakuna mwanaume wa kumtoa RA, EL, Chenge? maana wanajua kila mkuu alichofanya kabla na baada hapa kikwete ndie ajihudhuru wala sio lingine chama chako kitakuwa pambaya wasipofanikisha hilizoezi.
 
Back
Top Bottom